-
Netanyahu adai mabaki ya mwili yaliyorejeshwa si ya Shiri Bibas, HAMAS yamjibu
Feb 21, 2025 07:24Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel amedai kuwa harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imekiuka masharti ya makubaliano ya kubadilishana mateka kwa sababu imekabidhi mwili wa mwanamke asiyejulikana kutoka Ghaza badala ya ule wa mateka wa Kizayuni Shiri Bibas.
-
Askofu Mkuu wa Quds: Palestina, kamwe haitomsahau Nasrullah
Feb 21, 2025 03:21Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiorthodoksi la Ugiriki katika mji mtukufu wa al-Quds unaokaliwa kwa mabavu, Atallah Hanna, amemuenzi na kumsifu aliyekuwa Kiongozi wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah nchini Lebanon, Sayyid Hassan Nasralluh, akisisitiza kuwa watu wa Palestina daima wataendelea kuwa waaminifu kwake kwa namna alivyojitolea muhanga.
-
Ripoti ya Human Rights Watch yafichua jinai ya kutisha ya Israel
Feb 20, 2025 22:54Shirika la haki za binadamu la Humar Rights Watch limetoa ripoti mpya inayoonesha ukatili na jinai kubwa ya kuchupa mipaka iliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Hamas: Israel iliua mateka wake kwa kulipua vituo walikokuwa wamezuiliwa
Feb 20, 2025 07:59Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema leo Alkhamisi kwamba, tawi lake la kiijeshi Izuddin al Qassam na muqawama kwa ujumla vina wamefanya kila liwezekanalo kulinda heshima ya maiti wakati wa shughuli ya kukabidhi miili ya matekka hao, ilhali utawala vamizi wa Isarel haukuheshimu uhai yao walipokuwa hai.
-
Oxfam: Tunaanza kuelewa kina cha uharibifu uliofanyika Gaza
Feb 20, 2025 07:55Shirika la Oxfam la Uingereza limetangaza kuwa utawala wa Israel umeharibu zaidi ya asilimia 80 ya mitandao ya maji na maji taka ya Gaza na kusababisha hali mbaya ya kiafya.
-
Euro-Med: Israel inatumia drone kuwatia hofu watu wa Gaza, inawatisha kwa 'Nakba ya 2, ya 3'
Feb 20, 2025 07:50Shirika la kutetea haki za binadamu la Euro-Mediterranean Human Rights Monitor limeonya kuwa utawala wa Kizayunii wa Israel unatumia ndege zisizo na rubani kama silaha ya kisaikolojia kuwatia hofu na wahka Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, na hivyo kuzidisha mashinikizo kwa wakazi wa eneo hilo ili wakubali mpango wa Marekani na Israel unaowalazimisha kuhama makazi yao.
-
Errea nayo yabatilisha mkataba wake na Shirikisho la Soka la utawala wa Kizayuni
Feb 20, 2025 04:08Kampuni nyingine ya udhamini wa vifaa vya michezo ya Ulaya imefuta mkataba wake na Shirikisho la Soka la utawala wa Kizayuni wa Israel na hivyo kutoa pigo jingine kwa utawala huo haramu.
-
Vikosi vya Israel vimevamia nyumba ya mhubiri wa Msikiti wa Al-Aqsa
Feb 19, 2025 23:13Wakati mashambulizi ya jeshi katili la utawala haramu wa Israel katika sehemu mbalimbali za Ukingo wa Magharibi yakiendelea kwa siku ya 30 mfululizo, vikosi vya utawala huo ghasibu vimevamia nyumba ya mhubiri wa Msikiti wa Al-Aqsa, Sheikh Ekrima Sabri.
-
Rais Aoun: Israel lazima iache kukalia kwa mabavu kusini mwa Lebanon
Feb 19, 2025 23:06Rais wa Lebanon, Joseph Aoun, ameitaka Marekani kuushinikiza utawala wa Israel kuacha kukalia kwa mabavu eneo la kusini mwa Lebanon.
-
Kuendelea kushtakiwa jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina
Feb 19, 2025 23:04Gideon Sa’ar Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa utawala vamizi wa Israel ameshtakiwa kwa kutenda jinai za kivita katika Ukanda wa Gaza.