-
UNRWA: Hakuna taasisi yoyote inayoweza kujaza nafasi yetu Ghaza
Nov 19, 2024 07:40Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) amesema kuwa, hakuna taasisi yoyote inayoweza kujaza nafasi ya shirika hilo katika kuwahudumia na kuwafikishia misaada wakazi wa Ghaza.
-
Onyo la duru za kiusalama za Israel kwa Netanyahu
Nov 19, 2024 04:13Duru za usalama za utawala wa Kizayuni zimemtumia ripoti waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netnyahu, na kumuonya kuhusu nguvu za Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS na wajibu wa kutodharau nguvu hizo.
-
Hizbullah yashambulia Tel Aviv kwa makombora ya balestiki
Nov 19, 2024 02:53Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon inaendelea kutumia mkakati wake wa kujihami wa "Moto Kwa Moto, Beirut kwa Tel Aviv" katika kukabiliana na hujuma za kinyama za utawala katili wa Israel dhidi ya Lebanon.
-
Wanajeshi 30 wa Kizayuni waangamizwa kaskazini mwa Ukanda wa Gaza
Nov 18, 2024 23:14Kwa akali wanajeshi 30 wa utawala haramu wa Israel wameangamizwa na wanamuqawama kaskazini mwa Ukanda wa Gaza katika majuma ya hivi karibuni.
-
Yemen yatoa taarifa kuhusu mashambulizi iliyofanya dhidi ya ngome za utawala wa Kizayuni
Nov 18, 2024 03:45Jeshi la Yemen limetoa taarifa kuhusu mashambulizi liliyofanya dhidi ya baadhi ya maeneo nyeti na muhimu sana ya kijeshi ya adui Mzayuni katika maeneo ya Jaffa na Ashkelon huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu iliyopachikwa jina bandia la Israel.
-
Hamas yalaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Beit Lahiya
Nov 17, 2024 23:06Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imelaani mashambulizi makali yaliyofanywa na jeshi la utawala ghasibu wa Israel dhidi ya jengo la makazi ya raia na kuua makumi ya watu katika Ukanda wa Gaza. Taarifa iliyotolewa na Hamas imesisitiza kwamba vitendo hivyo vya kichokozi havitavunja irada na azma thabiti ya watu wa Palestina.
-
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani atoa mwito wa uchunguzi wa mauaji ya kimbari Gaza
Nov 17, 2024 23:05Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani ametoa mwito wa kufanyika uchunguzi wa jamii ya kimataifa kuhusu "mauaji ya halaiki" ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza.
-
Bin Salman aakhirisha kushiriki mkutano wa G20 kwa matatizo ya kiafya
Nov 17, 2024 23:05Shirika la Habari la Bloomberg limetangaza kuwa, Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman ameghairi safari yake iliyokuwa imepangwa ya kushiriki mkutano wa kilele wa viongozi wa kundi la mataifa tajiri na yale yanayostawi kiuchumi la G20, unaoanza leo (Jumatatu) huko Rio de Janeiro, Brazil.
-
Human Rights Watch yakiri kuhusika utawala wa Kizayuni wa Israel na jinai za kivita
Nov 17, 2024 23:04Katika ripoti yake ya hivi karibuni zaidi, shirika la kuteteta haki za binadamu la Human Rights Watch kwa mara nyingine tena limetangaza kuwa utawala haramu wa Israel umefanya jinai za kivita dhidi ya binadamu na mauaji ya kikabila huko Gaza, kuharibu vyanzo vya maisha na kuwafanya kuwa wakimbizi mara kadhaa asilimia 90 ya wakaazi wa Gaza.
-
Msemaji wa Hizbullah auawa shahidi katika shambulio la kinyama la Israel
Nov 17, 2024 11:19Mohammad Afif, afisa wa habari wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ameuawa shahidi katika shambulio la utawala wa Kizayuni huko Ras al-Naba, Beirut mji mkuu wa Lebanon.