-
Kupitishwa maazimio mawili katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu vita vya Gaza na UNRWA
Dec 13, 2024 11:19Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, limepitisha kwa wingi wa kura maazimio mawili yanayotoa wito wa kusitishwa mara moja vita vya Gaza na pia kuunga mkono shughuli za Shirika la Misaada na Ajira kwa Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA).
-
Hamas yakaribisha azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu kusitisha mapigano Gaza
Dec 13, 2024 06:32Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) "imekaribisha" azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linalotaka kusitishwa kwa mapigano mara moja na bila masharti huko Gaza, na kuitaka jamii ya kimataifa kuilazimu Israel isitishe vita vya mauaji ya kimbari kwenye ukanda huo.
-
Hamas: Muqawama katika Ukingo wa Magharibi unaendelea kwa nguvu zote
Dec 13, 2024 03:19Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imelaani jinai za kinyama za utawala wa Kizayuni katika maeneo mbalimbali ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kusisitiza kuwa, mashambulizi hayo ya Wazayuni hayawezi kuteteresha imani na irada ya wananchi wa Palestina na kwamba operesheni dhidi ya wavamizi hao zinaendelea.
-
Al-Houthi: Utawala wa Kizayuni una pupa ya kuteka maeneo zaidi hadi nje ya Syria
Dec 13, 2024 03:19Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen ameeleza kuwa, utawala wa Kizayuni unakodolea macho ya tamaa maeneo yote yanayopakana na ardhi za Palestina inayokaliwa kwa mabavu yakiwemo ya Syria na Misri na kusema kuwa, Netanyahu anatumia vibaya matukio ya Syria ili kutimiza njama hizo za muda mrefu za Kizayuni.
-
Ripoti: Wapalestina 4000 wameuawa kaskazini mwa Gaza katika kipindi cha miezi miwili
Dec 13, 2024 00:09Kwa akali Wapalestina 4000 wameuawa shahidi kaskazini mwa Ukanda wa Gaza katika kipindi cha miezi miwili iliyopita kufuatia hatua za kikatili na hujuma za jeshi la utawala ghasibu wa Israel katika maeneo hayo.
-
Mradi wa Wazayuni na Marekani wa kubadilisha jina la mashariki ya Palestina kuwa "Yuda na Samaria" utaishia wapi?
Dec 12, 2024 23:28Kadiri wakati wa kuapishwa rasmi Donald Trump kuwa rais wa Marekani unavyozidi kukaribia, ndivyo mipango na njama za Washington za kuunga mkono sera za kujitanua zaidi utawala ghasibu wa Israel zinavyohiri na kuonekana wazi zaidi.
-
Zaidi ya Wapalestina 40 wauawa shahidi mapema leo asubuhi Ghaza
Dec 12, 2024 02:59Televisheni ya Al-Jazeera ya Qatar imetangaza leo Alkhamisi kwamba Wapalestina 42 wameuawa shahidi na makumi ya wengine kujeruhiwa katika mashambulizi ya alfajiri ya leo yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Mgogoro wa kibinadamu Gaza katika kivuli cha kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel
Dec 12, 2024 02:46Huku zikikosoa hatua ya utawala wa Kizayuni ya kukwamisha upelekaji misaada ya kibinadamu huko Gaza, taasisi za kimataifa zimeeleza wasiwasi zilionao kutokana na kuendelea kuongezeka mgogoro wa kibinadamu katika Ukanda huo.
-
Mwanasayansi wa Syria auawa mjini Damascus, hofu yatanda baada ya kuondolewa madarakani Assad
Dec 12, 2024 00:41Watu wenye silaha wamemuua mwanasayansi mashuhuri wa Syria mjini Damascus huku kukiwa na hofu ya kufanyika msako dhidi ya wasomi wa nchi hiyo baada ya kuondolewa madarakani serikali ya Syria hivi karibuni na makundi yenye silaha yanayoungwa mkono na mataifa ya kigeni, hasa madola ya Magharibi.
-
Dheifullah al-Shami: Muqawama umeimarika kwa waranti wa ICC dhidi ya Netanyahu
Dec 11, 2024 08:52Waziri wa zamani wa Intelijensia wa Yemen amesema kuwa, muqawama umepata nguvu zaidi kufuatia waranti wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wa kumtia mbaroni Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala ghasibu wa Israel itatekelezwa.