-
Wazayuni milioni 2 wakimbilia kwenye mashimo kukwepa mashambulizi ya Yemen mjini Tel Aviv
Sep 26, 2024 23:35Zaidi ya walowezi milioni mbili wamekimbilia kwenye mashimo na harakati za uwanja wa ndege wa Ben Gurion mjini Tel Aviv zimesimamishwa baada ya wanamapambano wa Kiislamu wa Yemen kuutwanga kwa makombora mji mkuu huo wa utawala wa Kizayuni.
-
Watoto 625,000 wenye umri wa kwenda shule Gaza wanakabiliwa na sonona
Sep 26, 2024 23:34Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limeripoti kuwa, zaidi ya watoto 625,000 wenye umri wa kwenda shule katika Ukanda wa Gaza wanaandamwa na kiwewe, sonona na msongo mkali wa mawazo huku wakiishi katika magofu na majengo yaliyoharibiwa na mabomu ya Wazayuni.
-
Viongozi wa nchi tofauti wasisitiza ulazima wa kusimamishwa vita vya Gaza
Sep 26, 2024 23:05Suala la Israel kuivamia Gaza na kusikitishwa viongozi wa dunia na kuendelea jinai za utawala huo ghasibu dhidi ya Wapalestina wanaoishi Gaza ni moja ya mada muhimu za hotuba za viongozi wa nchi mbalimbali katika kikao cha 79 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York.
-
Israel yaua watu wengine 72 na kujeruhi 400 Lebanon, Hizbullah yajibu mapigo kwa makombora
Sep 26, 2024 03:17Utawala wa Kizayuni wa Israel umewaua shahidi watu wasiopungua 72 na kuwajeruhi wengine 400 nchini Lebanon katika siku ya tatu mtawalia ya mashambulizi ya kiwendawazimu unayofanya katika ardhi ya nchi hiyo sambamba na makabiliano yanayoendelea baina yake na harakati ya Muqawama ya Hizbullah.
-
Mamlaka za Ghaza zairejeshea Israel miili 88 ya Wapalestina isiyo na 'utambulisho' wowote
Sep 26, 2024 01:42Mamlaka za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimeurejeshea utawala wa Kizayuni wa Israel kontena lililobeba miili ya Wapalestina 88 ambayo haitambuliki kutokana na kutoambatanishwa na taarifa zozote kuhusu utambulisho wao.
-
Netanyahu aogopa kwenda nje ya Israel kwa vipigo vya makombora vya Hizbullah
Sep 25, 2024 10:29Ofisi ya waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni imetangaza kuakhirishwa tena safari ya Benjamin Netanyahu huko New York Marekani kwa ajili ya kushiriki katika mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Uakhirishaji huo umekuja huku Hizbullah ya Lebanon ikiutwanga kwa mara ya kwanza kwa kombora la balestiki, mji mkuu wa Israel, Tel Aviv.
-
Hizbullah yapiga Tel Aviv kwa mara ya kwanza kwa kombora la balestiki
Sep 25, 2024 04:30Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetumia kombora la balestiki kupiga Tel Aviv ikiwa ni kwa mara ya kwanza, suala lililosababisha wahka mkubwa na ving'ora katika mji huo na maeneo mengine ya Israel ikiwa ni pamoja na Netanya.
-
Duru mpya ya mashambulizi ya Wazayuni dhidi ya Lebanon
Sep 25, 2024 04:24Jeshi la utawala katili wa Israel limeendeleza jinai zake kwa shambulia kwa mabomu maeneo ya raia mashariki mwa Lebanon.
-
Haja ya kuchukuliwa hatua dhidi ya mpango wa Netanyahu wa kuifanya Lebanon kuwa Gaza nyingine
Sep 24, 2024 22:47Katika siku za hivi karibuni, utawala wa Kizayuni umepanua wigo wa jinai zake kutoka Gaza hadi Lebanon na kwa kutumia vibaya uzembe wa taasizi za kieneo na kimataifa, unatekeleza siasa zake katili za kuangamiza kila kitu katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Sambamba na Lebanon, jeshi la Israel linaendelea kuteketeza roho za Wapalestina wa Ghaza
Sep 24, 2024 07:43Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel linaendeleza mashambulizi na mauaji ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza mbali na vita vingine vya kinyama lilivyoanzisha dhidi ya Lebanon, ambako hadi sasa limeshaua watu wapatao 500, 100 miongoni mwao wakiwa ni wanawake na watoto.