Israel yaua watu wengine 72 na kujeruhi 400 Lebanon, Hizbullah yajibu mapigo kwa makombora
Utawala wa Kizayuni wa Israel umewaua shahidi watu wasiopungua 72 na kuwajeruhi wengine 400 nchini Lebanon katika siku ya tatu mtawalia ya mashambulizi ya kiwendawazimu unayofanya katika ardhi ya nchi hiyo sambamba na makabiliano yanayoendelea baina yake na harakati ya Muqawama ya Hizbullah.
Katika upande mwingine, Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Lebanon, Hizbullah imetangaza kuwa imerusha kombora la balestiki lililofika Tel Aviv kwa mara ya kwanza.
Hizbullah imeeleza pia kuwa, imefanya mashambulio ya makombora yaliyolenga Sa'ar kibbutz karibu na Nahariya kaskazini mwa Israel, na kujeruhi watu kadhaa, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya ndani.
Tangu harakati ya Muqawama ya Palestina Hamas ilipofanya Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa mnamo Oktoba 7, 2023, Hizbullah na Israel zimekuwa zikikabiliana kwa mashambulio ya mpakani.
Mnamo Septemba 23, jeshi la utawala wa Kizayuni lilifanya shambulio la kinyama kusini na mashariki mwa Lebanon, na kuwaua shahidi zaidi ya watu 550, ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya watu kuuawa katika siku moja tangu vita vya mwaka 2006.../