Oct 25, 2023 07:36
Rais Isaac Herzog wa Israel amedai kuwa, utawala huo wa Kizayuni hauna azma ya kuingia vitani na Harakati ya Hizbullah ya nchini Lebanon katika upande wa kaskazini, siku chache baada ya viongozi wa Marekani kuwatahadharisha watawala wa Israel kuhusu ugumu na hatari ya kuendesha vita viwili kwa wakati mmoja; upande wa kusini na Harakati ya Hamas ya Palestina na upande wa kaskazini na harakati yenye nguvu kubwa ya kijeshi, Hizbullah.