-
Mashambulio ya makombora na ndege zisizo na rubani ya Iran dhidi ya Israel, mwisho wa zama za "kushambulia na kukimbia" kwa Israel.
Jun 15, 2025 12:15Baada ya utawala wa Kizayuni kuishambulia Iran kwa ushirikiano wa Washington asubuhi ya Ijumaa, Juni 13, na kupelekea kuuawa shahidi idadi kubwa ya makamanda waandamizi wa kijeshi na wanasayansi, pamoja na raia wa kawaida, Iran, kama ilivyoahidi awali, ilianza kutoa jibu kali kwa jinai hiyo na mauaji ya kimbari Ijumaa usiku kupitia operesheni ya mashambulio ya makombora na ndege zisizo na rubani, iliyopewa jina la Ali ibn Abi Talib.
-
Kwa nini Marekani imewawekea vikwazo majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai?
Jun 08, 2025 06:45Marekani mnamo Alhamisi, Juni 5, iliwawekea vikwazo majaji wanne wa kike wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai kwa kushughulikia kesi zinazohusiana na Israel na hatua za Marekani nchini Afghanistan. Vikwazo hivyo, ambavyo mara nyingi huwekewa maafisa kutoka nchi zinazopinga Marekani, sasa vimewalenga maafisa wa mahakama ya kimataifa.
-
Kwa nini nchi za Amerika ya Latini zimejiunga na safu ya wakosoaji wa Israel?
Jun 04, 2025 02:27Rais Lula da Silva wa Brazil amesisitiza katika matamshi yake kwamba kinachoendelea Gaza si vita bali ni mauaji ya halaiki. Alifafanua: Tunachoshuhudia huko Gaza hivi sasa si vita kati ya majeshi mawili hata kidogo, bali kuna jeshi moja tu lenye weledi kamili ambalo linaua wanawake na watoto wa Ukanda wa Gaza.
-
Je, uhusiano wa serikali ya Julani na utawala wa Kizayuni unaelekea wapi?
May 31, 2025 03:40Vyanzo vya habari vimetangaza kuwa ujumbe unaohusiana na serikali ya mpito ya Syria umefanya mazungumzo ya siri na viongozi wa utawala haramu wa Israel.
-
Je, kwa nini Ujerumani, muungaji mkono mkubwa zaidi wa Ulaya kwa utawala wa Kizayuni, sasa inaonekana kuukosoa utawala huo?
May 29, 2025 06:18Friedrich Mertz, Kansela wa Ujerumani alibadilisha sauti yake kuhusiana na utawala wa Kizayuni mnamo Jumanne, Mei 27 na kusema: "Mashambulio makubwa ya kijeshi ya Waisraeli katika Ukanda wa Gaza hayana mantiki tena kwangu."
-
Amnesty International yataka mataifa ya Ulaya yaisusie kikamilifu Israel
May 22, 2025 12:51Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International limetoa wito wa kususiwa kabisa utawala wa Kizayuni wakati huu ambapo baadhi ya mataifa ya bara Ulayaa yanachukua hatua za kuutenga utawala huo kutokana na jinai zake huko Gaza.
-
Kwa nini Uhispania imeongeza mashinikizo dhidi ya Israel?
May 22, 2025 02:18Bunge la Uhispania limepitisha muswada unaoitaka serikali ya nchi hiyo kuacha kuuzia utawala ghasibu wa Israel zana zozote za kijeshi.
-
Kharrazi: Dunia ya kambi moja imeyoyoma, kuna haja ya mazungumzo ya kikanda
May 21, 2025 07:33Mkuu wa Baraza la Mahusiano ya Kigeni la Iran amesisitiza kuwa mfumo wa kambi moja umeyoyoma na sasa kumeibuka madola yenye nguvu ya kikanda na kusema: "Suluhisho pekee la changamoto za Mashariki ya Kati ni mazungumzo ya moja kwa moja kati ya nchi za eneo hilo bila ya uingiliaji wa madola ya nje ya kanda hiyo."
-
Yair Golan: Vita vya Gaza lazima visitishwe haraka iwezekanavyo
May 14, 2025 06:30Mkuu wa Chama cha Kidemokrasia cha utawala wa Kizayuni wa Israel ametaka kusimamishwa vita haraka iwezekanavyo dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza.
-
Katibu Mkuu wa Hizbullah: Muqawama utaendelea hadi ushindi kamili
May 09, 2025 07:39Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon amesema Muqawama utaendelea hadi ushindi kamili utakapopatikana na kuangamizwa kikamilifu utawala ghasibu na vamizi wa Kizayuni wa Israel.