-
Makubaliano ya makundi ya Palestina kwa ajili ya mshikamano na kuimarisha umoja
Jul 24, 2024 22:59Kwa kuwa mwenyeji wa makundi ya Wapalestina, China imefanikiwa kufanikisha maridhiano kati ya makundi hayo, ambayo mwendelezo wake unaweza kuwa na taathira chanya sio tu kwa Palestina, bali pia kwa eneo na ulimwengu mzima kwa ujumla.
-
Daktari Myahudi awaumbua Wazayuni kwa jinai zao dhidi ya watoto wa Palestina
Jul 24, 2024 02:57Daktari mmoja Mmarekani ambaye pia ni Myahudi amewafedhehesha Wazayuni kwa kufichua jinai kubwa zinazofanywa na wanajeshi makatili wa Israel dhidi ya watoto wadogo wa Palestina.
-
Israel yaendeleza mashambulizi kusini, katikati na kaskazini mwa Gaza; Wapalestina 85 wauawa shahidi
Jul 23, 2024 23:20Duru za habari za Palestina zimetangaza kuwa, jeshi la utawala wa Kizayuni limezidisha jinai na mashambulizi yake katika maeneo ya kaskazini, kusini na katikati mwa Ukanda wa Gaza na hivyo kuifanya idadi ya mashahidi wa Kipalestina waliouliwa hadi sasa huko Gaza kuongezeka.
-
Radiamali za asasi za kimataifa kuhusiana na hali mbaya ya kibinadamu Gaza
Jul 23, 2024 23:02Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Idadi ya Watu na Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka wameonya kuhusu hali mbaya ya kibinadamu na mgogoro katika Ukanda wa Gaza, hasa hali ya wanawake na watoto.
-
Kufanyika kura ya maoni Palestina; mkakati na suluhisho la Iran
Jul 23, 2024 10:29Nasser Kanani, msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, "suluhisho bora zaidi la kuhitimisha hali haramu ya sasa katika Palestina inayokaliwa kwa mabavu ni kufanyika kura ya maoni jumuishi kwa kushirikisha wakaazi wote na raia asili wa ardhi hiyo."
-
Hamas yatangaza mapatano ya 'umoja wa kitaifa' na makundi mengine ya Palestina
Jul 23, 2024 10:11Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, yenye makao yake huko Gaza imesema imetia saini makubaliano mjini Beijing na makundi mengine ya Palestina, ikiwa ni pamoja na Fat'h, kufanya kazi pamoja kwa ajili ya "umoja wa kitaifa."
-
Ansarullah yasema itachukua hatua kali za kulipiza kisasi dhidi ya Israel
Jul 23, 2024 10:04Afisa wa ngazi ya juu wa Yemen amesema nchi hiyo italipiza kisasi kwa shambulio baya la hivi karibuni la anga dhidi ya al-Hudaydah, na kwamba Israel lazima iwe tayari kwa matukio yasiyotarajiwa katika siku zijazo.
-
Rais Assad atilia mkazo kuimarishwa zaidi uhusiano wa kimkakati kati ya nchi yake na Iran
Jul 23, 2024 03:48Rais wa Syria Bashar Assad ametilia mkazo kuimarishwa zaidi uhusiano na kuimarishwa ushirikiano na uratibu baina ya nchi yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyuga mbalimbali.
-
Hatimaye utawala wa Kizayuni wakiri kuwa umeua mateka wake Ghaza
Jul 23, 2024 03:02Baada ya siku 290 za vita, hatimaye jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel limekiri kuwa makumi ya mateka wa Kizayuni wameuliwa katika ukanda wa Ghaza na askari wa utawala huo.
-
Palestina yaomba utawala wa Kizayuni uondolewe katika michezo ya Olimpiki ya Paris
Jul 23, 2024 03:01Kamati ya Olimpiki ya Palestina imemwandikia barua Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki, ikitaka utawala wa Kizayuni uondolewe katika Michezo ya Olimpiki ya Paris.