-
Ripota wa Umoja wa Mataifa akosoa vitendo vya kibaguzi vya utawala wa Israel
Jul 22, 2024 22:55Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu huko Palestina amekosoa mienendo ya kikatili ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina.
-
UN: Utapiamlo unatishia maisha ya wajawazito na vichanga Gaza
Jul 22, 2024 07:28Mfuko wa Idadi ya Watu wa Umoja wa Mataifa (UNPF) umetahadharisha kuhusu taathira hasi za utapiamlo zinazowakodolea macho wanawake wajawazito na watoto wachanga katika Ukanda wa Gaza; huku vita vya kikatili na vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina katika eneo hilo vikishadidi.
-
Hizbullah ya Lebanon yashambulia vitongoji vya Wazayuni
Jul 21, 2024 23:01Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon kwa mara nyingine tena imekishambulia kwa makombora kitongoji cha walowezi wa Kizayuni cha Dona, kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel).
-
Wanamuqawama wa Palestina watoa kipigo kikali kwa wanajeshi wa Kizayuni huko Rafah
Jul 21, 2024 08:01Wanamapambano wa Palestina wametoa kipigo kikali kwa wanajeshi wa utawala wa Kizayuni katika mapigano makali yaliyojiri katika mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
-
Yemen yashambulia Bandari ya Eilat kwa makombora ya balestiki
Jul 21, 2024 07:33Vikosi vya Wanajeshi wa Yemen vimeipiga kwa makombora ya balestiki Bandari ya Eilat, kusini ya maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel, katika operesheni ya kulipiza kisasi.
-
Utayarifu wa makundi ya Muqawama kwa ajili ya kukabiliana na utawala wa Kizayuni wa Israel
Jul 21, 2024 04:06Baada ya operesheni iliyofanywa na Jeshi la Yemen katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) kwa kutumia ndege isiyo na rubani, makundi ya Muqawama katika eneo la Magharibi mwa Asia yametangaza uungaji mkono wao kwa hatua hiyo na kuuonya utawala wa Kizayuni kuhusu kuendeleza vita.
-
Saudia yakanusha kuhusika na shambulio la Israel Hudaydah; Iran yalaani
Jul 21, 2024 03:20Wizara ya Ulinzi ya Saudi Arabia imekadhibisha ripoti za vyombo vya habari vya Israel kuwa Riyadh imeshiriki katika mashambulizi ya anga yaliyofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya mji wa al-Hudaydah, magharibi mwa Yemen.
-
Mufti wa Oman: Kuiunga mkono Yemen ni wajibu wa kila Muislamu
Jul 21, 2024 03:19Mufti Mkuu wa Oman amelaani vikali hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuushambulia mji wa magharibi mwa Yemen wa al-Hudaydah, huku akiwataka Waislamu kote ulimwenguni kuliunga mkono na kulisaidia kwa hali na mali taifa hilo la Kiarabu linalosumbuliwa na ukata na umaskini mkubwa.
-
Yemen: Tuko tayari kwa vita vya muda mrefu na Israel, ni baada ya Israel kushambulia al-Hudaydah
Jul 20, 2024 23:35Vikosi vya Jeshi la Yemen vimeapa kuendeleza operesheni zinazoiunga mkono Palestina baada ya utawala haramu wa Israel kushambulia maeneo ya raia katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Mzayuni: Baada ya Yemen kushambulia Tel-Aviv, anga ya "Israel" si salama tena
Jul 20, 2024 23:04Kiongozi mmoja wa ngazi za juu wa jeshi la utawala wa Kizayuni amekiri kwamba jeshi la Israel limeshindwa vibaya katika kukabiliana na droni ya Yemen iliyopiga Tel Aviv na kusisitiza kuwa, kuanzia sasa anga yote ya "Israel" si salama tena; na eneo lolote la utawala wa Kizayuni linaweza kushambuliwa bila ya kuwa na nguvu za kujikinga.