-
Msemaji wa jeshi la Yemen: Katu Ukanda wa Gaza hautakuwa peke yake
Jul 20, 2024 09:35Msemaji wa jeshi la Yemen amesema: Gaza haijawahi kuwa peke yake, ina washirika kutoka taifa kubwa ambalo ni tiifu kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
-
Bunge la Kiarabu: Uamuzi wa Mahakama ya Haki ni ushindi kwa haki za Wapalestina
Jul 20, 2024 07:41Bunge la Kiarabu na nchi za Kiarabu zikiwemo Iraq, Misri, Jordan na Kuwait zimekaribisha uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) wa kuvitaja vitongoji ya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) kuwa ni kinyume cha sheria.Taarifa ya mataifa hayo imeeleza kuwa, uamuzi wa mahakama ya ICJ ni ushindi kwa uadilifu na haki za Wapalestina.
-
Riyadh yaipongeza ICJ kuvitaja vitongoji vya Wazayuni kuwa haramu
Jul 20, 2024 04:24Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudi Arabia imekaribisha uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) wa kuvitaja vitongoji ya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) kuwa ni kinyume cha sheria.
-
Wapalestina wapongeza uamuzi wa ICJ dhidi ya Israel
Jul 20, 2024 02:52Makundi ya kisiasa na kijamii ya Palestina yamepongeza uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) wa kutazama ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu na Israel la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kuwa haramu na kinyume cha sheria.
-
Mtaalamu wa kijeshi: Shambulizi la al Huothi mjini Tel Aviv linaiweka Israel katika mtanziko
Jul 19, 2024 22:50Mtaalamu wa masuala ya kijeshi na kimkakati, Meja Jenerali Mohammed Al-Samadi, amesema kuwa shambulizi la kundi la Ansarullah la Yemen katikati mwa mji wa Tel Aviv kwa kutumia ndege isiyo na rubani ni miongoni mwa operesheni hatari zaidi zilizoikabili Israel tangu tarehe 7 Oktoba mwaka jana.
-
Kufeli njama za kuleta fitna baina ya Waislamu nchini Afghanistan
Jul 19, 2024 22:48Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Afghanistan ametangaza kuwa, katika kipindi cha miaka 20 iliyopita, kumefanyika njama nyingi za kuzusha fitna baina ya Waislamu wa Kisuni na Kishia nchini humo lakini zote zimefeli.
-
HAMAS, Jihadul Islami zaitaka PLO iache kuitambua Israel
Jul 19, 2024 07:38Harakati za Muqawama wa Kiislamu za Palestina za HAMAS na Jihadul Islami zimeitaka Mamlaka ya Ndani ya Palestina ibatilishe uamuzi wake wa kuutambua utawala haramu wa Israel.
-
Jeshi la Yemen laipiga Tel Aviv kwa droni mpya ya 'Yafa', taharuki yatanda
Jul 19, 2024 07:21Mtu mmoja ameuawa huku wengine zaidi ya 10 wakijeruhiwa baada ya mfumo wa ulinzi wa anga wa Israel kushindwa kutungua shambulio la ndege isiyo na rubani (droni) lililofanywa na jeshi la Yemen dhidi ya mji wa bandari wa Yafa (Tel Aviv) unaokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel, viungani mwa Tel Aviv.
-
Sisitizo la viongozi wakuu wa Iran na Saudia la kuimarisha uhusiano baina ya nchi zao
Jul 19, 2024 05:26Mohammed bin Salman, mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia na Massoud Pezeshkian, rais mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wamezungumza kwa simu na kutilia mkazo umuhimu wa kuendeleza ushirikiano kati ya Tehran na Riyadh.
-
Hamas: Upinzani wa Israel wa kuundwa taifa huru la Palestina ni batili
Jul 19, 2024 03:58Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) imekiona kitendo cha Bunge la utawal;a wa Kizayuni wa Israel cha kuidhinisha rasimu ya azimio dhidi ya kuasisiwa taifa la Palestina kuwa ni batili na kubainisha kwamba, hatua hiyo inatokana na dhati na asili ya uvamizi wa Wazayuni.