-
Hamas: Upinzani wa Israel wa kuundwa taifa huru la Palestina ni batili
Jul 19, 2024 03:58Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) imekiona kitendo cha Bunge la utawal;a wa Kizayuni wa Israel cha kuidhinisha rasimu ya azimio dhidi ya kuasisiwa taifa la Palestina kuwa ni batili na kubainisha kwamba, hatua hiyo inatokana na dhati na asili ya uvamizi wa Wazayuni.
-
Ansarullah: Tumeshambulia meli 170 zilizokuwa zikielekea Israel
Jul 19, 2024 03:57Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen ametangaza kuwa, idadi ya meli zilizoshambuuliwa na ambazo zinazohusiana na meli za Marekani, Israel na Uingereza katika Bahari Nyekundu zilizokuwa zikielekea katika bandari za ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina imefikia meli 170.
-
UNICEF: Asilimia 90 ya wakaazi wa Gaza wamekimbia makazi yao
Jul 19, 2024 03:56Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, asilimia 90 ya wakaazi wa Ukanda wa Gaza wameyakimbia makazi yao baada ya hujuma na uvamizi wa jeshi la Israel dhidi ya eneo hilo.
-
Oman: Wahusika wa shambulio la Muscat walikuwa ndugu 3 raia wa Oman
Jul 19, 2024 00:20Polisi ya Utawala wa Kisultani wa Oman imetangaza kwamba watu watatu waliofanya shambulio kwenye msikiti wa Waislamu wa madhehebu ya Shia huko Muscat juzi katika siku ya Ashura ya kukumbuuka mauaji ya mjukuu wa Mtume Muhammad (saw), Imam Hussein bin Ali bin Abi Twalib (as) walikuwa ndugu wenye utaifa wa Oman.
-
Lavrov: Hizbullah, serikali ya Lebanon hawataki vita kamili na Israel
Jul 18, 2024 23:56Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergei Lavrov, amesema harakati ya Hizbullah ya Lebanon na serikali ya nchi hiyo hawataki "vita kamili" na Israel lakini baadhi ndani ya utawala huo wa Israel wanataka vita.
-
Shambulio la wanajeshi wa Israel kwenye Msikiti wa Al-Aqsa
Jul 18, 2024 06:38Idara ya Wakfu wa Kiislamu ya Palestina katika mji wa Quds Tukufu unaokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel imetangaza kuwa wanajeshi wa utawala huo wamewazuia Waislamu kuingia katika eneo hilo takatifu kwa kuvamia Msikiti wa Al-Aqsa.
-
Mashambulio ya Hizbullah ya Lebanon katika vitongoji vya walowezi wa Kizayuni
Jul 18, 2024 06:08Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Lebanon Hizbullah imetangaza kufanya shambulio la makombora katika vitongoji vya walowezi wa Kizayuni kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Russia: Migogoro ya Asia Magharibi inasababishwa na sera mbovu za Marerkani
Jul 18, 2024 05:49Sergey Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa, hali mbaya katika eneo la Asia Magharibi ni matokeo ya kushindwa sera mbovu za Marekani katika eneo.
-
Wazayuni wazidi kupapurana, sasa ni zamu ya mkuu wa MOSSAD
Jul 18, 2024 02:20Mkuu wa shirika la kijasusi la utawala wa Kizayuni MOSSAD amemshambulia kwa maneno makali waziri mkuu wa utawala huo dhalimu, Benjamin Netanyahu, kwa kukwamisha tena mazungumzo ya kusimamisha vita Ghaza. Kabla ya hapo, mkuu wa majeshi ya Israel naye alikuwa amemshambulia vikali Netanyahu kwa sababu hiyo hiyo.
-
Uingereza na Marekani zaendelea kushambulia Yemen kuunga mkono Wazayuni
Jul 18, 2024 02:18Mapema leo Alkhamisi asubuhi, televisheni ya Al Mashirah ya Yemen imeripoti kuwa, ndege za madola vamizi ya Marekani na Uingereza zimefanya mashambulizi matatu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa al Hudaidah, magharibi mwa nchi hiyo ya Kiarabu.