-
Tume ya haki za binadamu Palestina yatahadharisha kuhusu mgogoro wa kibinadamu Gaza
Jul 17, 2024 23:02Tume huru ya haki za binadamu ya Palestina imetangaza kuwa kuendelea kuzingirwa Ukanda wa Gaza kutapeleke eneo hilo la ardhi ya Palestina kuathiriwa mgogoro wa kibindamu ambayo haujawahi kushuhudiwa.
-
Kiongozi wa Hamas asisitiza kudumisha utulivu huko Lebanon
Jul 17, 2024 23:00Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas amesisitiza juu ya kudumisha amani na usalama huko Lebanon.
-
Mzozo baina ya jeshi na serikali ya Israel; mgogoro wa kisiasa unaorindima kati ya Wazayuni
Jul 17, 2024 22:58Mkuu wa Majeshi ya utawala wa Kizayuni amemtaka waziri mkuu wa utawala huo pandikizi, Benjamin Netanyahu aombe radhi kutokana na matamshi yake dhidi ya jeshi la Israel. Hili linazidi kuthibitisha kuweko mzozo mkubwa baina ya jeshi katili la Israel na serikali yenye misimamo mikali ya Kizayuni inayoongozwa na nduli wa Ghaza, Benjamin Netanyahu.
-
Mrithi wa Ufalme wa Saudia ampongeza Rais mteule wa Iran
Jul 17, 2024 10:16Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia, Mohammad Bin Salman amemnyooshea mkono wa pongezi Masoud Pezeshkian, Rais Mteule wa Iran kwa kuibuka mshindi katika duru ya pili ya uchaguzi wa 14 wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Daesh: Tumehusika na shambulio la siku ya Ashura lililoua 6 Oman
Jul 17, 2024 09:47Kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) limekiri kuhusika na shambulizi la kigaidi lililolenga Waislamu wa madhehebu ya Shia waliokuwa wamekusanyika katika msikiti mmoja nchini Oman, kwa ajili ya maombolezo ya Ashura ya kukumbuka siku ya kuuliwa shahidi mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW), Imam Hussein bin Ali bin Abi Twalib (a.s).
-
Sayyid Nasrullah: Waislamu hivi sasa wameshikamana kutokana na Kimbunga cha al Aqsa
Jul 17, 2024 07:33Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, mshikamano unaoonekana hivi sasa na kupungua mivutano katika safu za Waislamu ni katika mafanikio makubwa ya operesheni ya Kimbunga cha al Aqsa iliyoongozwa na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS.
-
Kambi ya anga ya Marekani nchini Iraq yashambuliwa na ndege zisizo na rubani
Jul 17, 2024 03:37Kambi ya jeshi la anga ya Ain al-Asad inayohifadhi wanajeshi wa Marekani nchini Iraq imeshambuliwa kwa ndege zisizo na rubani, wiki moja kabla ya ziara inayotarajiwa ya ujumbe wa ngazi ya juu wa jeshi la Iraq mjini Washington kuendeleza mazungumzo ya kukomesha uwepo wa muungano wa kijeshi unaoongozwa na Marekani nchini humo.
-
Kiongozi wa Hizbullah: Israel ni uvimbe wa saratani, utaondolewa
Jul 17, 2024 03:16Kiongozi wa harakati ya muqawama ya Hizbullah ya nchini Lebanon amesema "uvimbe wa saratani" wa Israel utaondolewa na kizazi cha sasa cha Wapalestina.
-
Holocaust ya kukaririwa kila siku huko Gaza
Jul 17, 2024 00:13Wazayuni wenye itikadi kali za kufurutu ada wanaotawala huko Tel Aviv, wakiongozwa na Benjamin Netanyahu, licha ya kushindwa kufikia malengo yao ya kijeshi katika Ukanda wa Gaza, wanaendelea kufanya mauaji mapya ya holocaust kila siku katika ukanda huo.
-
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa: Kila eneo la Gaza ni uwanja wa mauaji
Jul 17, 2024 00:07Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, mashambulizi na jinai zinazoendelea kufanywa na jeshi la utawala ghasibu wa Israel katika kambi za wakimbizi wa Kipalestina huko Ukanda wa Gaza vimegeuza kila sehemu ya eneo hilo kuwa uwanja wa mauaji.