-
HAMAS: Mateka watatu, akiwemo raia wa US, waliuawa katika shambulio la Israel Nuseirat
Jun 10, 2024 04:36Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema mateka watatu waliuawa akiwemo raia wa Marekani katika shambulio la kinyama lililofanywa hivi karibuni na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye kambi ya wakimbizi wa Kipalestina ya Nuseirat huko Ghaza, lililoua pia zaidi ya raia 270 wa Kipalestina.
-
Gantz ajiuzulu na kujitoa kwenye baraza la mawaziri la vita la utawala wa Kizayuni
Jun 10, 2024 03:20Benny Gantz, mjumbe wa baraza la mawaziri la vita la Israel, ametangaza rasmi kujiuzulu na kujitoa kwenye baraza hilo na kutoa wito wa kuitishwa uchaguzi wa mapema.
-
Jeshi la Yemen lashambulia meli ya kivita ya Uingereza
Jun 10, 2024 01:19Vikosi vya wanamaji vya Yemen vimefanya operesheni mbili tofauti dhidi ya meli ya kivita ya Uingereza na pia meli mbili za kibiashara katika pwani ya taifa hilo ikiwa ni hatua ya kuonyesha mshikamano na Wapalestina wa Gaza ambao wanakabiliwa na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na Israel kwa himaya ya Marekani na Uingereza.
-
Sababu za umuhimu wa kikao cha D-8 mjini Istanbul kuhusu vita vya Gaza
Jun 09, 2024 23:54Kikao cha dharura cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama wa Kundi la Nchi za Kiislamu Zinazostawi Kiuchumi D-8 kilifanyika Jumamosi mjini Istanbul kwa kuhudhuriwa na wawakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Uturuki, Malaysia, Indonesia, Misri, Nigeria, Pakistan na Bangladesh kwa lengo la kuchukua msimamo wa pamoja dhidi ya utawala ghasibu wa Israel.
-
Haniya: HAMAS haitasalimu amri, itaendeleza muqawama
Jun 09, 2024 23:53Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kundi hilo la muqawama katu halitasalimu amri, bali litaendeleza mapambano yake kwa nguvu zote.
-
Malaysia yaziasa nchi za D-8 zikate uhusiano wa kiuchumi na Israel
Jun 09, 2024 23:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Malaysia amezitaka nchi wanachama wa kundi la D-8 kuvunja uhusiano wao wa kiuchumi na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Kaskazini ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel) imekuwa Jahanamu kwa walowezi wa Kizayuni
Jun 09, 2024 05:59Mashambulio makali ya Muqawama wa Kiislamu wa Lebanon dhidi ya ngome na vituo vya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel na vitongoji vya walowezi wa Kizayuni huko kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu kulikopachikwa jina bandia la Israel yamelifanya eneo hilo kuwa jahanamu kwa Wazayuni.
-
Jenerali wa Israel: ‘Makubaliano tu’ na Hamas ndio yanayoweza kuwarudisha nyumbani mateka wengine
Jun 09, 2024 05:58Israel Ziv, mkuu wa zamani wa kitengo cha operesheni za jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel amesema, inapasa kuwepo na "mpango mpana na wa kina" wa kuwarudisha mateka waliosalia na kumaliza vita.
-
Jeshi la Israel lilijipenyeza kwenye kambi ya Nuseirat kwa kutumia lori la misaada ya kibinadamu
Jun 09, 2024 05:58Duru za Palestina zimeeleza kuwa, vikosi maalumu vya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel vilivyowakomboa mateka wanne wa Kizayuni katikati mwa Ukanda wa Ghaza, vilijipenyeza kwenye kambi ya wakimbizi ya Nuseirat kwa kutumia lori la misaada ya kibinadamu.
-
UNICEF yatoa onyo kali kuhusu kuzorota hali ya watoto Ukanda wa Gaza
Jun 09, 2024 04:06Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limeelezea wasiwasi wake kuhusu hali mbaya ya watoto katika Ukanda wa Gaza.