-
Saudia yateua balozi wake nchini Syria baada ya zaidi ya muongo mmoja
May 27, 2024 08:27Saudi Arabia imetangaza kuteua balozi wake mpya nchini Syria ikiwa ni balozi wake wa kwanza baada ya zaidi ya muongo mmoja tangu ilipositisha uhusiano wake na serikali yar ais Bashar al-Assad.
-
UNFPA: Nusu ya watu wa Gaza wanakabiliwa na hatari ya njaa
May 27, 2024 02:21Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA) limetoa onyo kali kuhusu mgogoro wa kibinadamu unaoendelea katika Ukanda wa Gaza, likisema nusu ya wakazi wa eneo hilo wako katika hatari ya "njaa inayokaribia."
-
Wapalestina 35 wachomwa moto wakiwa hai katika shambulio la kinyama la Israel Rafah
May 26, 2024 23:50Jeshi katili la utawala wa Kizayuni wa Israel limeshambulia kwa makombora kambi ya watu waliolazimika kuhama makazi yao na kuhamia eneo lililotengwa kuwa na usalama huko Rafah, na kuwaua shahidi Wapalestina 35, wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto.
-
Al-Qassam: Tumeangamiza na kukamata mateka askari kadhaa wa Kizayuni + Video
May 26, 2024 04:13Abu Obeida, Msemaji wa Brigedi za Izzuddinul-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS ametangaza kuwa, wapiganaji wa brigedi hizo wamekinasa kwa kukiwekea chambo chini ya handaki kikosi cha jeshi la Kizayuni na kufanikiwa kuwaangamiza, kuwajeruhi na kuwakamata mateka askari kadhaa wa jeshi hilo katika eneo la kambi ya Jabalia kaskazini mwa Ukanda wa Ghaza.
-
UNICEF yatoa onyo kali kuhusu hatari ya vifo vya watoto wachanga katika Ukanda wa Gaza
May 26, 2024 03:27Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Watoto (UNICEF) umetahadharisha kuhusu hatari ya vifo vya watoto wachanga wa Kipalestina huko Ukanda wa Gaza kutokana na kuendelea mashambulizi ya utawala wa Kizayuni.
-
Takwa la Bunge la Kiarabu la kusimamishwa mara moja mauaji ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza
May 26, 2024 01:56Katika kikao kilichofanyika katika makao makuu ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu mjini Cairo, Spika wa Bunge la Kiarabu ametaka kusitishwa mara moja jinai na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Jeshi katili la Kizayuni linaziteketeza makusudi hospitali na vituo vya tiba vya Ghaza
May 26, 2024 01:10Msemaji a Wizara ya Afya ya Ukanda wa Ghaza amesema jeshi katili la utawala wa Kizayuni wa Israel linazibomoa na kuziteketeza kwa makusudi hospitali na vituo vya tiba vya ukanda huo.
-
Euro-Med HRM: Hukumu ya Mahakama ya ICJ ni ithibati kwamba Israel imeshavuka mipaka yote
May 26, 2024 01:09Maha Hussaini, Mkurugenzi wa Mkakati wa Shirika la kutetea haki za binadamu la Euro-Med Human Rights Monitor, amesema uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ wa kuutaka utawala wa Kizayuni wa Israel usimamishe mara moja mashambulio yake ya kijeshi katika mji wa Rafah ulioko kusini mwa Ukanda wa Ghaza ni hatua muhimu na yenye uzito mkubwa ambayo dunia imekuwa ikiingoja kwa miongo kadhaa, na wala si tangu tu yalipoanza "mauaji ya kimbari" mnamo Oktoba 7.
-
Maandamano ya watu milioni moja Sana'a Yemen kuunga mkono Wapalestina Gaza
May 25, 2024 03:47Mji mkuu wa Yemen, Sana'a, Ijumaa ulishuhudia maandamano ya watu milioni moja kwa ajili ya kuwaunga mkono wananchi wa Palestina, wakitaka kuendelea kuungwa mkono Wagaza hadi ushindi wao wa mwisho dhidi ya utawala wa Israel.
-
Jeshi la Yemen latekeleza oparesheni tatu za aina yake
May 24, 2024 22:35Msemaji wa jeshi la Yemen ametangaza kuwa jeshi hilo limetekeleza oparesheni tatu za aina yake dhidi ya mei tatu katika fremu ya awamu ya nne ya kushtadi mivutano.