-
Makundi ya Muqawama yatoa tamko kuhusu uamuzi wa nchi za Ulaya kuitambua nchi ya Palestina
May 24, 2024 06:50Makundi ya Muqawama ya Palestina yametoa mjibizo kwa utayarifu uliotangazwa na nchi kadhaa za Ulaya wa kuitambua nchi huru ya Palestina kwa kueleza kwamba hatua hiyo ni mabadiliko makubwa katika msimamo wa nchi mbalimbali duniani katika kuunga mkono piganio tukufu la taifa la Palestina.
-
Hizbullah, Harakati ya Muqawama Iraq zashambulia ngome za Israel
May 24, 2024 03:52Wanamapambano wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Iraq wamefanya operesheni tofauti dhidi ya kambi na ngome za kijeshi za utawala wa Kizayuni wa Israel, katika maeneo yaliyokaliwa kwa mabavu mwaka 1948, kwa ajili ya kulipiza kisasi cha vita vya umwagaji damu vya Israel dhidi ya Gaza.
-
Wapalestina wengine 60 wauawa na jeshi la Israel huko Gaza
May 23, 2024 23:30Makumi ya watu wakiwemo watoto wadogo na wanawake wanaripotiwa kuuawa shahidi na jeshi la utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Kuendelea kujiuzulu viongozi wa kijeshi na kiusalama wa Israel sambamba na kukiri kushindwa katika vita vya Gaza
May 23, 2024 23:05Mwenendo wa kujiuzulu viongozi wa kijeshi na kiusalama wa utawala wa Kizayuni unaendelea sambamba na kuendelea kushindwa utawala huo ghasibu katika vita na mauaji yake ya kimbari huko Ukanda wa Gaza.
-
Waarabu wazipongeza nchi za Ulaya zilizolitambua taifa la Palestina
May 23, 2024 06:58Mataifa ya Kiarabu yamekaribisha hatua ya baadhi ya nchi za Ulaya ya kutangaza rasmi kulitambua taifa la Palestina.
-
Jeshi la Kizayuni laendelea kumwaga damu za Wapalestina katika kila pembe ya Ghaza
May 23, 2024 04:14Mashambulio ya kinyama ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel yangali yanaendelea katika maeneo tofauti ya ukanda wa Ghaza.
-
Jinai baada ya jinai huko Gaza
May 23, 2024 00:49Pamoja na kuwa Netanyahu anakabiliwa na hatari ya kukamatwa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kutokana na jinai kubwa za kivita anazofanya huko Gaza, lakini bado anaendelea kufanya jinai hizo bila kujali lolote kutokana na msaada na uungaji mkono mkubwa anaopata kutoka kwa Marekani.
-
Marekani ina wasiwasi wa Israel kushindwa katika vita vya Ghaza
May 23, 2024 00:48Gazeti la mtandaoni la Politico limeeleza katika ripoti yake kwamba, Marekani ina wasiwasi wa utawala wa Kizayuni wa Israel kushindwa katika vita vya Ghaza.
-
Wanasheria wa The Hague waunga mkono ombi la kukamatwa viongozii wa Israel
May 22, 2024 03:37Wataalamu na mawakili wa kujitegemea mjini The Hague wameunga mkono uamuzi wa Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ya kuomba hati ya kukamatwa maafisa wa utawala ghasibu wa Israel.
-
Sayyid Nasrallah asema Rais Raisi alikuwa mujahid
May 21, 2024 22:54Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon ametuma salamu za rambirambi kufuatia kufa shahidi Rais wa Iran Sayyid Ebrahim Raisi na Waziri wa Mambo ya Nje Hossein Amir-Abdollahian na ujumbe walioandamana nao.