-
Nchi za Waislamu zataka kuruhusiwa misaada ya kibinadamu Gaza
Jan 03, 2026 02:42Mawaziri wa Mambo ya Nje wa mataifa manane ya Waislamu wameitaka jamii ya kimataifa kuishinikiza Israel, kama dola linalokalia kwa mabavu ardhi za Palestina, kuondoa mara moja vizingiti na vikwazo vya kuingia kwa misaada ya msingi na ya dharura katika Ukanda wa Gaza.
-
Al-Jazeera: Israel inajiandaa kuanzisha tena mashambulizi makali Gaza
Jan 02, 2026 23:07Waziri wa Vita wa Israel, Israel Katz ameliagiza jeshi la utawala huo haramu kujiandaa kurejea kwenye mapigano makali dhidi ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas katika Ukanda wa Gaza, hayo yameripotiwa na kanali ya televisheni ya al-Jazeera ikinukuu gazeti la Kizayuni la The Jerusalem Post.
-
Jackie Chan amwaga machozi kuwalilia watoto wa Ghaza
Jan 02, 2026 03:27Jackie Chan, muigizaji maarufu wa Hollywood na filamu za Hong Kong, amewaga machozi kuwalilia watoto wa Ghaza akielezea huzuni yake kubwa kutokana na hali mbaya ya kibinadamu katika ukanda huo akitangaza kwamba alipotazama video ya mahojiano na mtoto wa Palestina alilia na kumkumbusha tena mateso yasiyoisha ya watoto wa Ghaza.
-
Fat’h: Hatua zozote za kikanda bila ya kutatua kadhia ya Palestina zitashindwa tu
Jan 02, 2026 03:24Mmoja wa viongozi waandamizi wa harakati ya ukombozi wa Palestina ya Fat’h amesema kuwa, Makubaliano ya Abraham ni udanganyifu wa kisiasa na hayatoleta utulivu katika eneo hili maadamu yanapuuza kadhia ya Palestina.
-
Baraza la Makanisa Duniani lataka kuwekewa vikwazo Israel kutokana na vita vya Gaza
Jan 01, 2026 23:18Baraza la Makanisa Duniani (WCC) limeutaka Umoja wa Ulaya (EU) kuiwekea Israel vikwazo vikiwemo vya silaha kutokana na mauaji ya kimbari yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni huko Gaza, na ukiukaji wa haki dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu.
-
Kwa nini kiwango cha kujiua katika jeshi la Israel kimefikia kiwango cha juu zaidi?
Jan 01, 2026 23:06Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Isarel, kwa kukiri kujiua kwa makumi ya wanajeshi wake, limekubali kuwa jumla ya wanajeshi 151 wamepoteza maisha katika mwaka huu wa sasa.
-
2025, mwaka mbaya zaidi kwa Wapalestina kufuatia mauaji ya kimbari ya Israel
Jan 01, 2026 08:51Ofisi Kuu ya Takwimu ya Palestina imeripoti kuwa mwaka 2025 ulikuwa mwaka mbaya zaidi katika uga wa kibinadamu na idadi ya jamii ya watu huko Palstina kutokana na vita vya Israel dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza na kuongezeka kwa ukiukaji wa sheria katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikiwa ni pamoja na Quds Mashariki.
-
Israel yakemewa, yalaaniwa kimataifa kwa kupiga marufuku asasi 37 zinazotoa misaada Ghaza
Jan 01, 2026 02:33Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani marekebisho ya sheria yaliyopitishwa na Bunge la utawala wa kizayuni wa Israel, Knesset Desemba 29, yanayohusu kusitishwa shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA).
-
Kuenea wimbi la mapambano ya umma ya Wapalestina Ukingo wa Magharibi; changamoto ambayo utawala wa kizayuni haujawahi kuishuhudia
Jan 01, 2026 00:47Wachambuzi wa Kizayuni wamekiri kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel hauna uwezo wa kukabiliana na makundi mapya ya Muqawama wa Palestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Israel yasitisha shughuli za mashirika ya misaada zaidi ya 30 huko Gaza chini ya sheria mpya za usajili
Dec 31, 2025 22:55Israel imesimamisha shughuli za mashirika ya kimataifa 30 ya masuala ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza. Waandishi wa habari na watetezi wa haki za binadamu wamekosoa na kulaani vikali hatua hiyo ya utawala wa Kizayuni.