-
Jeshi la Yemen lashambulia meli na manuwari za kivita za Marekani, Ghuba ya Aden
Mar 09, 2024 07:20Msemaji wa jeshi la Yemen, Yahya Saree amesema kuwa kundi hilo limefanya operesheni za aina yake ambazo zimelenga meli ya Marekani katika Ghuba ya Aden kwa kutumia makombora kadhaa, na manuari za kivita za Marekani katika Bahari Nyekundu na Ghuba ya Aden kwa kutumia ndege 37 zisizo na rubani.
-
HAMAS: Tume ya kimataifa isiyo na upendeleo ichunguze tuhuma za ukatili wa kingono wa Oktoba 7
Mar 09, 2024 03:52Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetaka "tume ya kimataifa ya uchunguzi isiyo na upendeleo" iundwe ili kuchunguza madai kwamba wapiganaji wake walihusika na ukatili wa kingono walipotekeleza Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa dhidi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel Oktoba 7, 2023.
-
Kuhani wa Kiyahudi ahamasisha Wazayuni wafanye mauaji ya kimbari Ghaza
Mar 09, 2024 03:43Kuhani mwanamgambo na mhubiri wa mahubiri ya Kizayuni ya utoaji vitisho, Eliyahu Mali, ametoa wito wa kufanywa mauaji ya kimbari ya Wapalestina waliowekewa mzingiro huko Ghaza, akidai kuwa kufanya hivyo kunaendana na Halakha, yaani sheria ya Kiyahudi.
-
Hizbullah yaipiga komandi ya kijeshi ya Israel kwa makombora ya mizinga
Mar 08, 2024 23:27Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imejibu jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Ghaza kwa kukitwanga kwa makombora kituo kilichoanzishwa karibuni tu cha komandi ya kijeshi ya Israel kaskazini mwa ardhi za Palestina zilizopachikwa jina bandia la Israel.
-
Wazayuni waendeleza jinai za mauaji na uteketezaji wa miundombinu katika maeneo tofauti ya Ghaza
Mar 08, 2024 07:45Kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza kumepelekea kuongezeka idadi ya Wapalestina wanaouawa shahidi na miundombinu inayobomolewa na kuteketezwa katika eneo hilo.
-
Hofu ya Wazayuni ya kuibuka Intifadha nyingine Palestina
Mar 08, 2024 05:00Utawala wa Kizayuni wa Israel una wasi wasi mkubwa wa kuanzishwa Intifadha (mwamko) nyingine ya Palestina katika hali ambayo hauna nguvu na umeonyesha udhaifu mkubwa mkabala wa operesheni ya kimbunga cha Al-Aqsa na makundi ya mapambano ya ukombozi wa Papalestina.
-
HAMAS: Israel imetibua juhudi zote za kusitisha vita Gaza
Mar 08, 2024 03:53Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema utawala haramu wa Israel umevuruga jitihada zote za wapatanishi za kufikiwa makubaliano ya usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Kusambaratishwa mtandao mwingine wa kijasusi wa Israel huko Uturuki
Mar 07, 2024 22:50Utawala wa kibaguzi wa Israel bado unaendeleza operesheni zake za kijasusi dhidi ya Waislamu wa Uturuki.
-
Vyombo vya habari vya Uingereza vinawaonyesha Waisraeli waathiriwa zaidi kuliko Wapalestina
Mar 07, 2024 08:43Imebainika kuwa "upendeleo mkubwa" unafanywa na vyombo vya habari vya Uingereza katika utangazaji wa matukio ya Ukanda wa Ghaza tangu Oktoba 7, kutokana na kutumia "lugha ya hisia" inayowaonyesha Waisraeli kuwa ni wahanga na waathiriwa wa mashambulizi mara 11 zaidi kulinganisha na Wapalestina.
-
Watu 7 wameuawa na kujeruhiwa katika shambulizi la Yemen dhidi ya meli ya Marekani
Mar 07, 2024 03:23Taasisi ya kigaidi ya CENTCOM ya Marekani mapema leo Alhamisi imethibitisha kwamba watu 3 wameuawa na wengine 4 wamejeruhiwa katika shambulio la jeshi la Yemeni dhidi ya meli ya Marekani katika Bahari Nyekundu au Bahari ya Sham.