-
Walimwengu walaani Wazayuni kuchoma moto msikiti katika Ukingo wa Magharibi
Nov 16, 2025 03:36Hatua ya kundi la walowezi wa Kizayuni wenye misimamo ya kufurutu ada ya kuchoma msikiti wa Hajja Hamida katika Ukingo wa Magharibi huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu imelaaniwa katika kila kona ya dunia.
-
Hamas yatahadharisha kushadidi janga la kibinadamu Ukanda wa Gaza
Nov 16, 2025 03:35Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeonya kuhusiana na kushadidi janga la kibinadamu katika Ukanda wa Gaza.
-
Jihadul-Islami: Muqawama hautaitambua Israel, hakutakuwa na suluhu bila Palestina kupata haki zake
Nov 15, 2025 22:59Mwakilishi wa harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina hapa mjini Tehran amesema: "sisi katika mavuguvugu ya Muqawama wa Kiislamu hatutambui uwepo wa utawala wa Kizayuni na hatulazimiki kuutambua, hasa kwa vile utawala huu hautambui hata uwepo wa watu wa Palestina."
-
WHO: Wapalestina 900 wameaga dunia Gaza kutokana na kuchelewa kupata huduma za matibabu
Nov 15, 2025 08:56Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, kushindwa kupata vibali vya kuondoka mara moja kwa wagonjwa kutoka Gaza kumesababisha vifo vya wagonjwa 900 hadi sasa.
-
HAMAS: Kwa msaada wa Iran, Muqawama una nguvu zaidi hivi sasa katika kukabiliana na adui Mzayuni
Nov 15, 2025 01:52Mmoja wa makamanda wa Harakati ya Muqawama wa Ghaza amesema kuwa: Maadui walitaka kusambaratisha Muqawama kupitia vikwazo na mashinikizo, lakini kwa msaada wa Iran, Muqawama una nguvu zaidi hivi sasa za kupambana na adui Mzayuni kuliko hata ilivyokuwa huko nyuma.
-
Lieberman: Israel si lolote si chochote bila ya msaada wa Marekani
Nov 14, 2025 23:04Waziri wa zamani wa fedha wa utawala wa Kizayuni amekiri kwamba hivi sasa Israel inapitia kipindi kibaya mno cha kiuchumi na kusisitiza kwamba inabidi waishukuru Marekani kwa msaada wake kwani bila ya msaada huo, Israel si lolote si chochote, bali itaangamia.
-
Maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la kizayuni zagunduliwa Ghaza
Nov 14, 2025 04:13Timu za uokoaji za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimegundua na kufukua maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Vitisho vya mzayuni vyaifanya serikali ya Al-Jolani ifute maadhimisho ya Kimbunga cha Al-Aqsa
Nov 14, 2025 04:08Duru za habari zimeripoti kuwa kongamano la Operesheni ya Muqawama wa Palestina dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel ya Kimbunga cha Al-Aqsa, lililokuwa limepangwa kufanyika katika mji wa Aleppo nchini Syria limefutwa baada ya mwandishi mmoja wa habari wa Kizayuni kutoa vitisho kwa kiongozi wa mpito wa nchi hiyo, Al-Jolani na serikali yake.
-
Maafa ya vita vya kinyama vya Israel yamepelekea Wapalestina 6,000 wa Ghaza kukatwa viungo
Nov 13, 2025 23:07Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Ghaza imetoa ripoti inayoonyesha kuwa, Wapalestina 6,000 wamekatwa viungo katika eneo hilo tangu utawala wa kizayuni wa Israael ulipoanzisha vita vya kinyama Oktoba 2023 ambavyo vimeendelea kwa muda wa miaka miwili.
-
UN: Raia 114 wameuawa Lebanon katika ukiukaji wa usitishaji vita uliofanywa na Israel
Nov 13, 2025 23:07Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema ukiukaji wa usitishaji vita uliofanywa Israel uliotokana na makubaliano yaliyofikiwa kati ya utawala huo wa kizayuni na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon ya Hizbullah mnamo Novemba 2024 umesababisha vifo vya raia 114 wa nchi hiyo.