-
Idadi ya waliouawa shahidi Gaza yaongezeka na kufikia watu 8,306, watoto ni 3,457
Oct 30, 2023 11:10Wizara ya Afya katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa, hadi kufikia jioni ya leo idadi ya Mashahidi wa mashambulizi ya kinyama ya utawala wa Kizayuni katika eneo hilo imeongezeka na kufikia watu 8,306.
-
Msemaji wa HAMAS: Hatamu za udhibiti wa mapigano na adui mzayuni ziko mikononi mwa wanajihadi
Oct 30, 2023 09:20Msemaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kuwa, muqawama unao uwezo wa kudhibiti hatamu za mapigano na adui Mzayuni na kwamba mwenendo wa mapambano uko kwenye udhibiti wa wanajihadi.
-
Hatua mpya za Marekani katika fremu ya kuuunga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel
Oct 30, 2023 08:05Tangu kuanza duru mpya ya vita kati ya utawala wa Kizayuni na makundi ya muqawama ya Palestina na operesheni ya Kimbunga ya Al-Aqsa na radiamali kali ya Wazayuni dhidi ya hatua hiyo, Marekani ikiwa mshirika wa kistratijia wa Israel imetoa himaya kubwa ya kisiasa, kidiplomasia na kijeshi kwa utawala huo ghasibu. Filihali Washington imechukua hatua mpya katika mwelekeo huu.
-
Ndege za kivita za Russia zashambulia maficho ya magaidi Idlib na Latakia nchini Syria
Oct 30, 2023 08:04Naibu mkuu wa Kituo cha Maridhiano cha Russia nchini Syria ametangaza kuwa jeshi la anga la Russia limefanya shambulio dhidi ya maficho ya chini ya ardhi ya makundi ya kigaidi katika miji ya Idlib na Latakia kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
-
Mkuu wa Jumuiya wa kuihami Palestina: Watu wa Gaza watashinda
Oct 30, 2023 03:29Mkuu wa Jumuiya ya Kuihami Palestina ameeleza kuwa watu wa Gaza wamesimama imara na kwa nguvu zote katika kupigania haki yao na kusisitiza kuwa kwa hakika watu wa Gaza watashinda na hakuna shaka katika hilo.
-
Abu Ubaida: Netanyahu atakabiliwa na kipigo kikubwa kuliko kile anachohofia huko Gaza
Oct 29, 2023 22:59Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imemuonya Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu, kuhusu mipango yoyote ya kupanua mashambulizi ya nchi kavu ya utawala huo katika Ukanda wa Gaza baada ya zaidi ya wiki tatu za mashambulizi mtawalia ya mabomu na ndege za kivita za utawala huo katika eneo hilo lililo chini ya mzingiro.
-
Wanajeshi wa Kizayuni walioangamizwa tangu kuanza Kimbunga cha Al Aqsa wafika 311
Oct 29, 2023 10:56Msemaji wa jeshi la utawala wa Kizayuni amekiri kuwa hadi sasa wanajeshi 311 wa Israel wameangamizwa tangu kuanza oparesheni ya Kimbunga cha Al Aqsa.
-
Operesheni ya nchi kavu, kelele tupu za Israeli; raia ndio shabaha rahisi ya Netanyahu
Oct 29, 2023 08:34Ijapokuwa imekuwa vigumu kwa kiasi fulani kupata habari na ripoti kuhusu hali ya maafa na hasara inayosababishwa na mashambulio ya kinyama ya utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Ghaza, kufuatia hatua ya makusudi ya utawala huo ya kukata Intaneti na kuwalenga waandishi wa habari, lakini habari chache zinazotoka katika ukanda huo zinaashiria kuwa operesheni ya nchi kavu ya utawala huo imefeli pakubwa licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa nga na ushiriki wa majeshi ya Marekani katika operesheni hiyo.
-
Afisa mkuu wa Hizbullah; Israel ni mwoga na dhaifu mno kuweza kushinda mashambulizi ya nchi kavu huko Gaza
Oct 29, 2023 02:52Jeshi la Israel halina ujasiri na uwezo wa kupambana na kukabiliana na Hamas na vikosi vingine vya mapambano ya ukombozi huko Gaza kama Tel Aviv itaamua kufanya uvamizi wa ardhini katika eneo hilo linaozingirwa. Hayo yamesemwa na kiongozi wa ngazi ya juu wa harakati ya muqawama ya Lebanon Hizbullah.
-
Kukaribisha HAMAS azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
Oct 29, 2023 02:07Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imekaribisha azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu Gaza na kutangaza kuwa inataka Baraza Kuu la umoja huo na taasisi zingine husika za kimataifa kutekeleza hatua za lazima kwa ajili ya utekelezaji wa haraka wa azimio hilo ili vivuko vya Gaza vifunguliea tena na hivyo kuruhusu nishati ya mafuta na misaada ya haraka ya kibinadamu iwafikie watu wa eneo hilo.