-
Makumi ya askari wa Marekani walioko Iraq wakumbwa na corona
Apr 11, 2020 10:34Makumi ya askari wa jeshi vamizi la Marekani nchini Iraq wameambukizwa ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona.
-
Kukiri Masoud Barzani; Iran na shahidi Soleimani ndio waliongoza mapambano dhidi ya Daesh
Apr 11, 2020 05:39Masoud Barzani, Mkuu wa chama cha Demokrasia cha Kurdistan huko Iraq amefanya mahojiano na televisheni ya MBC ya nchini Saudi Arabia na kukiri kuwa Iran na Luteni Jenerali shahidi Qassem Soleimani aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH walikuwa wa awali kabisa kulisaidia eneo la Kurdistan ya Iraq kuendesha vita dhidi ya kundi la kigaidi la Daesh.
-
Kuendelea mashambulizi ya jeshi la Uturuki katika ardhi za Syria
Apr 11, 2020 02:39Katika hali ambayo serikali ya Uturuki inawalazimisha raia wake kukaa karantini majumbani, jeshi la nchi hiyo na vibaraka wake, sambamba na kuzivamia ardhi za kaskazini na mashariki mwa Syria limewasababishia hasara kubwa raia wa nchi hiyo ikiwa ni pamoja na kubomoa nyumba zao.
-
Barzani: Luteni Jenerali Soleimani alikuwa mtu wa kwanza kuwasaidia Wakurdi wa Iraq kupambana na ISIS
Apr 11, 2020 02:26Mkuu wa chama cha Democrat cha Kurdistan ya Iraq jana aliiambia televisheni ya MBC ya Saudi Arabia kwamba Iran na Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ndio waliokuwa watu wa kwanza kabisa kwenda katika eneo la Kurdistan nchini Iraq kuwasaidia wananchi wa eneo hilo kupambana na genge la kigaidi la Daesh (ISIS).
-
Usitishaji vita wa uongo, Saudia yaendeleza mashambulizi Yemen
Apr 11, 2020 02:17Msemaji wa Majeshi ya Yemen jana usiku alisema kuwa, muungano vamizi unaoongozwa na Saudi Arabia unaendelea kufanya mashambulio katika maeneo mbalimbali ya Yemen licha ya kudai kuwa umesitisha mashambulizi.
-
Saudia inawatuma Yemen watu walioathirika na virusi vya Corona
Apr 10, 2020 23:55Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Uratibu wa Masuala ya Haki za Binaadamu nchini Yemen amesisitiza kuwa, Saudi Arabia imekuwa ikituma waathirika wa virusi vya Corona Yemen na kwamba vyombo vya usalama vya nchi hiyo vinafanya juhudi kubwa kuweza kuwatambua watu hao.
-
Waziri Mkuu mteule wa Iraq: Mamlaka ya kitaifa ya kujitawala ni mstari mwekundu kwangu
Apr 10, 2020 23:45Waziri Mkuu mpya mteule wa Iraq Mustafa al-Kadhimi amesema, mafanikio ya nchi hiyo katika mahusiano ya kimataifa yatapatikana kwa "kuheshimiana na kushirikiana".
-
Russia: Ripoti ya shirika la upigaji marufuku silaha za kemikali inapotosha ukweli kuhusu Syria
Apr 10, 2020 23:45Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema, ripoti iliyotolewa na shirika la upigaji marufuku silaha za kemikali kuhusu Syria inapotosha ukweli halisi wa kinachojiri nchini humo.
-
Ismail Haniya: Siasa za mauaji za Marekani na Israel zimeongeza nguvu ya kambi ya muqawama
Apr 10, 2020 07:30Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema kuwa, siasa za Wazayuni za kuwaua viongozi wa muqawama na mauaji yaliyofanywa na Marekani dhidi ya Luteni Jenerali Qassim Soleimani aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) hazijakuwa na natija nyingine ghairi ya kuongeza nguvu na adhama ya kambi ya muqawama.
-
Muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudia waendelea kukiuka usitishaji vita nchini Yemen
Apr 10, 2020 07:29Huku Martin Griffiths, Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Yemen na Nayef Falah al Hajraf, Katibu Mkuu wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi wakipongeza uamuzi wa kusitisha vita na mapigano nchini Yemen, muungano vamizi unaoongozwa na Saudia katika vita huko Yemen umeendelea kukiuka usitishaji vita huo.