-
Mgombea wa chama cha Republican achoma Qur'ani ili kuunga mkono kampeni yake ya uchaguzi
Aug 26, 2025 11:45Mgombea wa chama cha Republican wa kiti cha Kongresi huko Texas, anayejulikana kwa uadui wake mkubwa dhidi ya Waislamu amewakasirisha Waislamu zaidi ya bilioni mbili duniani kwa kuchoma moto nakala ya kitabu hicho kitakatifu ili kuunga mkono kampeni yake ya uchaguzi.
-
Mwandishi habari ajiuzulu Reuters akilalamikia hatua ya shirika hilo kuhalalisha mauaji ya Israel dhidi ya waandishi habari
Aug 26, 2025 11:44Mpiga picha wa Canada, Valerie Zink, ametangaza kujiuzulu kutoka kwenye shirika la habari la Reuters, akipinga nafasi ya shirika hilo katika kuendeleza propaganda za Israel na kuhalalisha mauaji ya waandishi wa habari wa Palestina katika Ukanda wa Gaza.
-
UN, OIC, EU, RSF na hata waitifaki wa Israel walaani shambulio la kinyama lililoua wanahabari Ghaza
Aug 26, 2025 00:09Taasisi za kimataifa ukiwemo Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC, Umoja wa Ulaya, Shirika la Wanahabari Wasio na Mipaka (RSF) na hata nchi kadhaa za Magharibi waitifaki wa utawala wa kizayuni wa Israel zimelaani vikali shambulio la kinyama lililofanywa na jeshi la utawala huo katika Hospitali ya Nasser iliyoko Khan Younis katika Ukanda wa Ghaza.
-
Norway yalaani jinai za Israel Ukanda wa Gaza
Aug 25, 2025 23:17Norway imeutaja ukatili unaofanya utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza kuwa ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa, na kutangaza kwamba nchi hiyo ya Ulaya inafikiria kupiga marufuku makampuni ya Norway kushiriki katika shughuli zinazounga mkono upanuzi wa vitongoji vya walowezi katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
EU yasisitiza kuiunga mkono "kwa dhati" ICC baada ya US kuwawekea vikwazo waendesha mashtaka 2
Aug 25, 2025 03:08Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amesema "amesikitishwa sana" na uamuzi wa Marekani wa kuwawekea vikwazo maafisa wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC).
-
Ufaransa 'yamjia juu' balozi wa US Paris kwa kuituhumu kuwa inahatarisha maisha ya Mayahudi
Aug 25, 2025 03:08Ufaransa imemwita balozi wa Marekani nchini humo Charles Kushner, baada ya mwanadiplomasia huyo kumwandikia barua Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akidai kwamba Paris imeshindwa kuchukua hatua za kutosha kukomesha vitendo vya mabavu dhidi ya Mayahudi raia wa nchi hiyo.
-
UN: Mzozo wa Rohingya umezidi kuwa mbaya kwa zaidi ya miaka minane sasa
Aug 24, 2025 08:22Miaka minane baada ya Waislamu wa kabila la Rohingya nchini Mynmar kulazimika kuhama katika Jimbo la Rakhine, Umoja wa Mataifa umesema kuwa mzozo unaowakabili raia hao umezidi kuwa mbaya.
-
Russia yatungua droni ya Ukraine iliyokusudia kushambulia kinu cha nyuklia cha Kursk
Aug 24, 2025 07:23Vikosi vya ulinzi wa anga vya Russia vimeitungua ndege isiyo na rubani ya Ukraine (Droni) iliyokuwa imekusudia kutekeleza shambulizi katika kiwanda cha nguvu za nyuklia cha Kursk cha Russia (KNPP).
-
Maandamano yafanyika London kupinga mauaji ya kimbari yanayoendelezwa na Israel huko Gaza
Aug 24, 2025 04:24Maandamano makubwa yamefanyika nje ya ubalozi wa utawala wa Israel mjini London, Uingereza kulaani mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Hatua ya Trump dhidi ya Bolton; ulipizaji kisasi binafsi au utakaso wa kisiasa?
Aug 24, 2025 02:58Rais Donald Trump wa Marekani, daima amekuwa akimulikwa na vyombo vya habari kutokana na mtindo wake tata wa uongozi na mbinu za hujuma dhidi ya wapinzani wake wa kisiasa. Mojawapo ya mifano ya wazi zaidi ya tabia hii ni hatua yake ya karibuni dhidi ya John Bolton, Mshauri wake wa zamani wa Usalama wa Taifa, ambaye amekuwa ishara ya mivutano ya ndani katika utawala wake.