-
Wapiga picha wa Gaza washinda Tuzo ya Kalamu ya Dhahabu ya Uhuru
Jun 15, 2026 11:19Jumuiya ya Wachapishaji Habari Duniani imetangaza kwamba tuzo ya Kalamu ya Dhahabu ya Uhuru 2026 itatolewa kwa wapiga picha na wakurugenzi wa video kutoka Ukanda wa Gaza ulioharibiwa na vita.
-
Araqchi: Iran itaiwajibisha Marekani kwa ajili ya utekelezaji wa makubaliano
Jun 15, 2026 10:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi amejadili makubaliano Iran na Marekani na wenzake wa Uturuki, Iraq, Misri, Japani na Saudi Arabia, akisisitiza wajibu wa Marekani wa kutekeleza makubaliano hayo.
-
Washington Post: Trump anasherehekea kurudi katika hali ya kabla ya vita na Iran
Jun 15, 2026 10:09Gazeti la Washington Post, katika ripoti yake kuhusu hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani, limekejeli hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kusherehekea kurejea Washington kwenye hali ya kabla ya Februari 28, hatua ambayo baadhi ya wataalamu wanaamini ni kurudi nyuma kwa maana halisi ya neno hilo mkabala wa Iran.
-
Iran yatangaza kufikiwa makubaliano ya kumaliza vita na Marekani
Jun 15, 2026 04:29Sekretarieti ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) imethibitisha kuwa Iran na Marekani zimekamilisha maandishi ya hati ya makubaliano (MoU) yanayolenga kumaliza vita, kusimamisha mara moja na kwa kudumu operesheni zote za kijeshi katika nyanja zote, ikiwemo Lebanon, na pia kuondoa mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani dhidi ya Iran.
-
Viongozi wa dunia wakaribisha makubaliano ya kumaliza vita vya Marekani dhidi ya Iran
Jun 15, 2026 04:28Viongozi mbalimbali duniani wamekaribisha hati ya makubaliano (MoU) kati ya Iran na Marekani, ambayo inahitimisha mara moja vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran, kuondoa mzingiro wa baharini, na kufungua tena Lango Bahari la Hormuz kwa usafiri wa kimataifa.
-
Jezi za Kombe la Dunia zilizopewa jina la mtoto wa Kipalestina aliyeuawa na Isral zazinduliwa
Jun 15, 2026 04:27Fulana za michezo zenye jina la "Jezi ya Kombe la Dunia ya Hind Rajab" zimezinduliwa rasmi sambamba na mashindano ya kombe hilo yanayoendelea katika nchi za Marekani, Canada na Mexico; jezi ambazo zimebuniwa na kutengenezwa kwa idhini ya mama wa "Hind Rajab", mtoto wa Kipalestina aliyeuawa shahidi na askari wa Israel.
-
Sudan: RSF inafanya biashara haramu ya viungo vya binadamu
Jun 15, 2026 04:24Serikali ya Sudan imelituhumu kundi la Rapid Support Forces (RSF) kuwa linaendesha mtandao wa biashara haramu ya viungo vya binadamu ndani ya magereza ya Daqris na Shala huko El Fasher, mji mkuu wa jimbo la Darfur Kusini, ambalo kwa mujibu wa makadirio ya serikali ya Khartoum, lina wafungwa karibu 20,000 wa kijeshi na raia.
-
Makumi ya magaidi, majasusi na wachochezi wa ghasia wamekamatwa wakati wa uvamizi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran
Jun 15, 2026 04:20Wizara ya Intelijensia ya Iran imesema imefanikiwa kutekeleza operesheni za kupambana na ugaidi, ujasusi na hujuma nchini wakati wa uvamizi wa siku 39 wa Marekani na Israel ambao ulisitishwa mapema Aprili.
-
Hamas yalaani safari ya "rais wa Somaliland" huko Israel, yasema ni dhambi ya kisiasa
Jun 15, 2026 04:12Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imeitaja safari ya rais wa jimbo lililotangaza kujitenga na Somalia la Somaliland huko Israel kuwa ni "dhambi ya kisiasa, ukiukaji wa kanuni na sheria zote za kimataifa, na kupuuza msimamo wa Waarabu na Waislamu kuhusu suala la Quds tukufu."
-
Jenerali wa IRGC: Iran inajitayarisha kujibu vitendo vya uchokozi
Jun 14, 2026 12:05Kamanda mwandamizi wa Jeshi la Iran laWalinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema vikosi vya ulinzi vya Iran viko tayari kikamilifu kukabiliana na hatua yoyote ya uadui, akionya maadui kwamba nchi hiyo iko tayari kutoa jibu la haraka kwa shambulio lolote.