-
Russia: Mashambulizi yasiyo na sababu ya US na Israel dhidi ya Iran ni hujuma dhidi ya mfumo wa usalama wa kanda na kimataifa
Mar 25, 2026 11:37Sergei Shoigu Katibu wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia amesema: Mashambulizi yasiyo na sababu ya Marekani na Israel dhidi ya Iran ni hujuma dhidi ya mfumo wa usalama wa kanda na kimataifa.
-
Araqchi: Ukosefu wa usalama katika Ghuba ya Uajemi ni matokeo ya uchokozi wa adui
Mar 25, 2026 11:29Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China wamezungumza kwa simu na kujadili matukio ya hivi sasa kuhusiana na Vita vya Ramadhani.
-
CENTCOM: Wanajeshi wetu waliojeruhiwa katika vita dhidi ya Iran wamefika 290
Mar 25, 2026 11:19Kamandi Kuu ya jeshi gaidi la Marekani (CENTCOM) imetangaza kuwa karibu wanajeshi 290 wa nchi hiyo wamejeruhiwa katIka vita vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran.
-
Umeme wakatwa kaskazini mwa Tel Aviv kufuatia mashambulizi ya makombora ya Iran
Mar 25, 2026 11:09Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimeripoti kuwa huduma ya umeme imekatwa katika moja ya miji ya kistratejia ya kaskazini mwa Israel kufuatia mashambulizi ya makombora ya Iran.
-
Manuwari ya USS Abraham Lincoln yalengwa kwa makombora ya Cruise ya jeshi la Iran
Mar 25, 2026 11:01Makombora ya Qadir ya baharini ya Jeshi la Wanamaji la Iran yameshambulia kundi la meli za kivita za Marekani linaloongozwa na manowari ya Abraham Lincoln na kulilazimisha kukimbia na kubadilisha eneo lake.
-
Jenerali wa Marekani: Wairani wanaweza kukabiliana na uchokozi wa Marekani na Israel kwa miaka mingi
Mar 25, 2026 11:00Jenerali mstaafu wa Marekani amezungumzia mashinikizo ya kiuchumi na kisiasa yanayoongezeka kwa serikali ya Washington kutokana na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran, na kukiri kwamba Wairani wanaweza "kukabiliana na mashambulizi haya kwa miaka mingi."
-
Waziri Mkuu wa Uhispania: Vita dhidi ya Iran ni janga na maafa makubwa
Mar 25, 2026 11:00Waziri Mkuu wa Uhispania ametangaza kwamba vita vya sasa vya Marekani na Wazayuni katika Mashariki ya Kati ni "vibaya zaidi" kuliko vita vya Iraq mwaka 2003 na ni "janga kubwa," na kusema: Utawala wa Kizayuni wa Israel unataka kurudia "uharibifu" uleule wa Gaza nchini Lebanon.
-
Makombora ya Iran yalenga Kamandi ya Kijeshi ya Israel na Manoari na Marekani ya Abraham Lincoln
Mar 25, 2026 10:05Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeilenga kamandi ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni iliyoko katika eneo la kaskazini la Safed katika wimbi jipya la mashambulizi ya makombora.
-
Jenerali Abdollahi: Jeshi la Iran litaendeleza mapambano ya kujihami hadi ushindi kamili
Mar 25, 2026 09:24Kamanda wa Kamandi ya Khatam al‑Anbiya (SAW) katika Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika ujumbe wake kwamba: “Vikosi vyenye nguvu vya ulinzi vya Iran ya Kiislamu, kwa utiifu kamili kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, vimesimama imara katika ahadi yao ya kulinda taifa tukufu na lenye ushindi la Iran, na vitaendeleza njia hii tukufu kwa msaada wa watu wenye ufahamu na ushujaa wa Iran ya Kiislamu hadi ushindi kamili.”
-
Msemaji wa Jeshi la Iran: Msiite kushindwa kuwa ni makubaliano
Mar 25, 2026 08:27Msemaji wa Kamandi ya Khatamul Anbiya (SAW) ya Jeshi la Iran amewahutubu watawala wa Marekani na kuwaambia kuwa, wasiite kushindwa kuwa ni makubaliano.