-
Iran yaihutubu UN kuhusu 'mwenendo haramu endelevu' wa Trump
Jan 03, 2026 07:01Iran imeuonya rasmi Umoja wa Mataifa kuhusu "mwenendo haramu endelevu" wa Marekani, kufuatia matamshi ya vitisho ya Rais Donald Trump ambayo Jamhuri ya Kiislamu imeyashutumu na kuyaeleza kama ya uingiliaji wa mambo yake ya ndani na tishio la wazi la utumiaji nguvu.
-
Nchi za Waislamu zataka kuruhusiwa misaada ya kibinadamu Gaza
Jan 03, 2026 06:12Mawaziri wa Mambo ya Nje wa mataifa manane ya Waislamu wameitaka jamii ya kimataifa kuishinikiza Israel, kama dola linalokalia kwa mabavu ardhi za Palestina, kuondoa mara moja vizingiti na vikwazo vya kuingia kwa misaada ya msingi na ya dharura katika Ukanda wa Gaza.
-
Iran, ulimwengu wa Kiislamu waadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa Imam Ali AS
Jan 03, 2026 06:04Wananchi Waislamu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wamejiunga na wenzao kote duniani kuadhimisha siku ya kukumbuka kuzaliwa Amirul Muumin Ali (AS) Imam wa Kwanza wa Waislamu wa Kishia ulimwenguni.
-
Somalia yapokezwa uenyekiti wa kiduru wa Baraza la Usalama la UN
Jan 03, 2026 06:03Somalia jana Ijumaa ilichukua urais wa zamu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kipindi cha mwezi huu wa Januari, ikiwa ni mara ya kwanza kwa nchi hiyo kushikilia wadhifa huo tangu ilipohudumu mara ya mwisho katika baraza hilo mwaka 1971-72.
-
Chuki dhidi ya Waislamu yaongezeka Australia baada ya shambulio la Bondi
Jan 03, 2026 06:01Afisa mmoja wa Australia ametoa tahadhari kuhusu ongezeko la chuki dhidi ya Waislamu tangu kujiri shambulio la Bondi mwezi uliopita, ambalo lililenga jamii ya Wayahudi wa nchi hiyo katika tamasha la Hanukkah.
-
Araghchi amjibu Trump: Vikosi vya Iran viko tayari kujibu mapigo
Jan 03, 2026 02:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amemuonya Rais wa Marekani, Donald Trump dhidi ya kuingilia masuala ya ndani ya Jamhuri ya Kiislamu, akikosoa matamshi yake ya hivi karibuni na kuyaeleza kuwa "yasiyo na busara na hatarishi," na kusisitiza kwamba vikosi vya jeshi la Iran vimejiandaa kikamilifu kulinda mamlaka ya kujitawala nchi hii.
-
Kwa nini Marekani imepoteza nafasi yake ya kimataifa?
Jan 03, 2026 02:38Gazeti la The Wall Street Journal limeandika katika ripoti yake kwamba: "Marekani imepoteza hadhi yake ya kimataifa kwa kiasi kikubwa katika miaka 25 ya kwanza ya karne ya 21, kutokana na utawala mbaya, vita vya gharama kubwa na migogoro ya ndani."
-
Al-Jazeera: Israel inajiandaa kuanzisha tena mashambulizi makali Gaza
Jan 03, 2026 02:37Waziri wa Vita wa Israel, Israel Katz ameliagiza jeshi la utawala huo haramu kujiandaa kurejea kwenye mapigano makali dhidi ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas katika Ukanda wa Gaza, hayo yameripotiwa na kanali ya televisheni ya al-Jazeera ikinukuu gazeti la Kizayuni la The Jerusalem Post.
-
Sheikh Mayunga, mwanazuoni mashuhuri wa Kiislamu Afrika Mashariki ameaga dunia
Jan 02, 2026 13:28Jamii ya Kiislamu Afrika Mashariki na hasa nchini Tanzania imekumbwa na msiba mkubwa kufuatia kufariki dunia kwa mwanazuoni mashuhuri, na mfasiri wa Qur'ani Tukufu, Sheikh Ali Jumaa Mayunga, aliyefariki dunia tarehe 1 Januari 2026, jijini Dar es Salaam, Tanzania.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa: Adui anatamani kuyageuza matatizo ya kiuchumi kuwa mgogoro wa kiusalama
Jan 02, 2026 12:55Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema maadui wa Iran wanajaribu kutumia matatizo ya kiuchumi ili kuibua mzozo wa kiusalama nchini