-
Iran na Oman zajadili utaratibu mpya wa kusimamia Lango-Bahari la Hormuz
Jun 23, 2026 10:49Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf na Waziri wa Mambo ya Nje Abbas Araghchi wamekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Sayyid Badr bin Hamad al-Busaidi, kujadili utaratibu mpya wa kusimamia Lango-Bahari la kimkakati la Hormuz.
-
Pezeshkian: Kuwajibika kwa Marekani ndio sharti la kuendelea mazungumzo
Jun 23, 2026 10:33Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametilia mkazo umuhimu wa kutekelezwa makubaliano yaliyofikwa baina ya Iran na Marekani kwa ajili ya kuendelezwa mazungumzo kati ya pande hizo kuhusu utekelezaji wa mkataba wa maelewano uliosainiwa hivi karibuni.
-
Mazishi ya Imam Khamenei kufanyika kwa siku sita nchini Iran na Iraq
Jun 23, 2026 03:06Makao makuu ya kumbukumbu ya Kiongozi aliyeuawa shahidi wa Iran, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei yametangaza ratiba ya mazishi ya siku sita katika miji mitano, ikianza na shughuli ya kuaga mwili wake kwa siku mbili mjini Tehran mnamo Julai 4 na kumalizika kwa maziko yake katika mji mtakatifu wa Mash'had, tarehe 9 Julai.
-
Jenerali Qaani awaambia Wazayuni: Muondoke wenyewe kusini mwa Lebanon la sivyo mtafukuzwa kwa mateke
Jun 23, 2026 02:59Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amewaambia wavamizi wa Kizayuni kwamba ikiwa hawataondoka kusini mwa Lebanon kwa miguu yao wenyewe, watafukuzwa kwa fedheha hali ya kuwa wameshindwa.
-
Ugonjwa wa Ebola DRC: Visa 1003, vifo 254 vyasajiliwa
Jun 23, 2026 02:57Maambukizi 1,003 ya Ebola yamerekodiwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo mlipuko wa hivi karibuni umesababisha pia vifo vya watu wasiopungua 254.
-
Zaidi ya wakimbizi milioni moja wa Sudan wanaishi nchini Misri kwa hofu na wasiwasi
Jun 23, 2026 02:43Zaidi ya wakimbizi milioni 1.3 wa Sudan wanaishi Cairo, mji mkuu wa Misri kwa hofu na wasiwasi mkubwa, na licha ya mabilioni ya dola ya misaada yanayotumwa kwa nchi hiyo, wengi wao wanaendelea kufanya jitihada za kuondoka Misri kutokana na hofu ya kukamatwa na kufungwa.
-
Waziri Mkuu wa Italia amwambia Trump: Pilipili usioila inakuwashia nini?
Jun 22, 2026 14:09Waziri Mkuu wa Italia, Giorgia Meloni amemshauri Rais wa Marekani, Donald Trump kujalia ya kwake mwenyewe badala na kufuatilia ya wengine baada ya kudai kwamba kiongozi huyo wa Italia anajaribu kuongeza umaarufu na viwango vyake vya kukubalika ndani ya nchi kwa kurekebisha uhusiano na Washington.
-
Kamati ya utendaji ya PUIC yakaribisha mpango wa Iran wa kuimarisha mshikamano wa nchi za Kiislamu
Jun 22, 2026 11:12Pendekezo la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran la kuimarisha mshikamano katika mchakato wa kumchagua Rais mpya wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) limepitishwa katika mkutano wa Kamati ya Utendaji ya PUIC.
-
Kenya: Muswada wa fedha 2026 kutiwa saini kuwa sheria
Jun 22, 2026 10:31Muswada wa fedha 2026 nchini Kenya unatarajiwa kutiwa saini na kuwa sheria.
-
Mataifa ya Ulaya yakabiliwa na wimbi la joto kali
Jun 22, 2026 09:58Mataifa ya Ulaya yanakabiliwa na wimbi la joto kali huku yakilazimika kuchukua hatua kadhaa ili kuepusha maafa.