-
Wapinzani Zimbabwe waapa kupinga azma ya kurekebisha katiba
Jul 10, 2026 08:07Viongozi wa upinzani nchini Zimbabwe wameapa kupinga ndani na nje ya nchi marekebisho ya katiba yanayomruhusu Rais Emmerson Mnangagwa kuongeza muda wa utawala kwa miaka miwili na kufuta uchaguzi wa moja kwa moja wa rais.
-
Mamilioni wahudhuria mazishi ya Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei katika mji wa Mash'had
Jul 09, 2026 15:25Shughuli maalumu ya kuuaga na kuusindikiza mwili wa kiongozi shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei pamoja na mashahidi wa familia yake imefanyika leo katika mji mtakatufu wa Mash'had.
-
Iran yapeleka malalamiko ya kushambuliwa vituo vyake vya anga za mbali katika Umoja wa Mataifa
Jul 09, 2026 12:01Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali mashambulizi haramu ya utawala wa Kizayuni wa Israel na Marekani dhidi ya vituo vyake vya anga za mbali na kuwasilisha malalamiko yake rasmi kuhusu suala hilo katika kikao cha jopo kazi la Umoja wa Mataifa kuhusu kuzuia mashindano ya silaha katika anga za juu, ikitoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka na jamii ya kimataifa kwa ajili ya kukabiliana na matumizi ya silaha katika anga hizo.
-
Nigeria na Afrika Kusini zavutana kwa kifo cha raia katika seli za polisi
Jul 09, 2026 11:36Polisi ya Afrika Kusini imethibitisha kuwa kifo cha raia wa Nigeria akiwa korokoroni hakikutokana na maandamano dhidi ya wahamiaji wa kigeni nchini humo yaliyofanyika wiki iliyopita.
-
Saratani inaua 26,000 kwa siku, WHO yafichua pengo la maisha kati ya matajiri na maskini
Jul 09, 2026 10:42Ripoti mpya ya Shirika la Afya Duniani (WHO) imeonya kwamba saratani inaweka mzigo mkubwa wa kibinadamu na kiuchumi kwa jamii duniani kote, ikichukua uhai wa zaidi ya watu 26,000 kila siku na kudhihirisha ukosefu mkubwa wa usawa katika viwango vya maisha kati ya nchi tajiri na maskini.
-
Baada ya mamilioni kutoa heshima kwa Shahidi Khamenei nchini Iraq, Tehran yasema tukio hilo limetuma ujumbe wa umoja wa Umma
Jul 09, 2026 09:43Katika ujumbe uliotolewa mapema leo Alkhamisi, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) Brigedia Jenerali Esmail Qaani ametoa shukrani kwa taifa na serikali ya Iraq kwa maandalizi mazuri ya mazishi ya Kiongozi aliyeuawa shahidi wa Mapinduzui ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei na watu wa familia yake.
-
IRGC yashambulia miundombinu muhimu ya Marekani huko Kuwait, Bahrain kama sehemu ya majibu ya awali
Jul 09, 2026 08:48Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeshambulia miundombinu muhimu katika kambi nne za Marekani huko Kuwait na Bahrain katika awamu ya kwanza ya majibu yake dhidi ya ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha vita unaofanywa na Marekani.
-
Ni mabadiliko gani ya kisiasa na kiusalama yanayofuatiliwa na Marekani kwa kuendelea kukiuka makubaliano ya kusitisha vita?
Jul 09, 2026 07:07Katika saa za alfajiri ya Jumatano, Julai 8, 2026, jeshi la Marekani, kwa kukiuka waziwazi vifungu vya 2 na 4 vya Hati ya Umoja wa Mataifa na kifungu cha kwanza cha makubaliano ya kusitisha vita, limefanya mashambulizi ya kichokozi katika vituo vya ufuatiliaji na usimamzi katika pwani ya kusini mwa Iran.
-
Rais Pezeshkian: Mazishi ya Kiongozi wa Iran ni kielelezo cha umoja wa kitaifa
Jul 09, 2026 03:33Rais Masoud Pezeshkian amesema mahudhurio makubwa ya watu kutoka matabaka yote ya jamii katika mazishi makubwa yaliyofanyika kwa ajili ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ni kielelezo cha umoja wa kitaifa nchini Iran.
-
Pezeshkian: Unyanyasaji wa Marekani katika Kombe la Dunia unaakisi sera ya kigeni ya Washington
Jul 09, 2026 03:30Rais wa Iran Masoud Pezeshkian amesema Marekani imegeuza Kombe la Dunia FIFA la 2026 kuwa uwanja mwingine wa uonevu na mashinikizo ya kisiasa, akisisitiza kuwa mwenendo wa Washington kama mwenyeji wa michezo hiyo unaonyesha sera zile zile inazotekeleza kote duniani.