-
Abu Torabi Fard: Jihadi ni ufunguo wa mabadiliko na ulinzi wa haki katika Qur'ani Tukufu
Oct 17, 2025 12:00Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa: Jihadi ni nguzo muhimu na yenye kuleta mabadiliko katika dini ya Kiislamu ambayo inatilia mkazo ushirikiano na Muqawama wa pamoja katika kupambana na dhulma mbali na kuhimiza jitihada za mtu mmoja mmoja.
-
Ushindi Mpya wa Ghaza; Hamas na Jihadul Islami dhidi ya magenge ya Shin Bet
Oct 17, 2025 12:00Baada ya kusitishwa mapigano na utawala wa Kizayuni, vikosi vya Muqawama vya Ghaza vimeingia katika vita vipya vya kupambana na magenge ya mamluki wa shirika la kijasusi la Israel Shin Bet kwenye Ukanda wa Ghaza ili kuwazuia majambazi hao kuunda maeneo yaliyojitenga chini ya uongozi wa utawala wa Kizayuni.
-
Viongozi wa nchi za kigeni waanza kuwasili Nairobi kwa mazishi ya Raila Odinga
Oct 17, 2025 11:59Matayarishao ya maziko ya mwanasiasa mashuhuri wa Kenya Raila Odinga, aliyefariki dunia juzi Jumatano akiwa na umri wa miaka 80 alipokuwa anatibiwa nchini India, yanaendelea na tayari viongozi wa nchi za kigeni wameanza kuwasili mjini Nairobi kushiriki kwenye maziko hayo yanayotarajiwa kufanyika kashokutwa Jumapili jimboni kwake Bondo.
-
Kanali Randrianirina aapishwa kuwa rais mpya wa Madagacar, SADC yaunda timu
Oct 17, 2025 11:59Kanali wa kijeshi, Michael Randrianirina, ameapishwa leo Ijumaa kuwa rais wa Madagascar katika mji mkuu, Antananarivo huku umuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ikimteua Rais wa zamani wa Malawi Joyce Banda kuongoza ujumbe wa kutafuta ukweli nchini Madagascar kufuatia matukio ya hivi karibuni ya kisiasa na kiusalama nchini humo.
-
Majeshi ya Nigeria yaua makumi ya waasi katika operesheni za nchi nzima
Oct 17, 2025 11:59Jeshi la Nigeria limetoa taarifa na kutangaza kuwa makumi ya waasi wameuawa na wengine 62 kukamatwa na vikosi vya serikali katika operesheni za nchi nzima kwenye kipindi cha wiki mbili zilizopita.
-
Afisa mwandamizi wa usalama wa Iran akutana na Putin, ampa ujumbe wa Kiongozi Muadhamu
Oct 17, 2025 07:28Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Ali Larijani amekutana na Rais Vladimir Putin wa Russia mjini Moscow, na kumkabidhi ujumbe wa moja kwa moja kutoka kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei.
-
Mripuko wa homa ya Bonde la Ufa waua watu 33 Senegal, Mauritania
Oct 17, 2025 07:17Watu wasiopungua 33 wamefariki dunia kutokana na homa ya Bonde la Ufa nchini Senegal na Mauritania tangu kuzuka kwa mripuko wa homa hiyo nadra mwishoni mwa Septemba, afisa wa Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC) alisema hayo jana Alkhamisi.
-
Putin amuonya Trump kuhusu kuipa Ukraine makombora ya Tomahawk
Oct 17, 2025 07:05Rais wa Russia, Vladimir Putin amemuonya Rais wa Marekani, Donald Trump katika mazungumzo yao ya simu kwamba, kuipa Ukraine makombora ya masafa marefu ya Tomahawk kutaharibu zaidi uhusiano kati ya Moscow na Washington.
-
Mkuu wa majeshi ya Yemen auawa katika mashambulizi ya Israel
Oct 17, 2025 06:56Mkuu wa Majeshi ya Yemen, Meja Jenerali Mohammad Abd al-Karim al-Ghamari ameripotiwa kuuawa shahidi katika mashambulizi ya anga ya Israel, pamoja wapamba wake kadhaa na mtoto wake wa kiume aliyekuwa na umri wa miaka 13, Hussein al-Ghamari.
-
Unyanyuaji Uzani; Muirani avunja rekodi ya dunia, ashinda dhahabu Misri
Oct 17, 2025 06:50Ali Akbar Gharibshahi, bingwa wa mchezo wa kunyanyua vitu vizito wa Iran ameweka rekodi mpya ya dunia na kushinda medali ya dhahabu katika kategoria ya kilo wanamichezo wenye 107, kwenye Mashindano ya Dunia ya Kunyanyua Uzani ya 2025 nchini Misri.