-
Iravani akanusha vikali azimio la Arab League dhidi ya Iran, asema ni la upendeleo
May 06, 2026 10:43Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amejibu azimio la kikao cha Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab Legue) dhidi ya Iran kilichofanyika mjini Cairo akisema kuwakingia kifua wavamizi hakuwezi kubadili ukweli wa kisheria.
-
BBC: Uingereza ni mwathirika mkubwa zaidi wa kiuchumi wa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran
May 06, 2026 10:29Ripoti ya BBC inasema Uingereza inakabiliwa na pigo kubwa zaidi kwa ukuaji wa uchumi miononi mwa nchi za kundi la 20 (G20), kutokana na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran na kufungwa Mlango Bahari wa Hormuz.
-
Afrika Kusini yabaini maambukizi ya virusi vya Hanter vinavyohusishwa na meli ya utalii
May 06, 2026 10:24Afrika Kusini imebaini virusi kwa jina la Hanter aina ya Andes ambavyo hueneza maambukizi kutoka kwa binadamu kwenda kwa binadamu katika watu wawili waliotoka kwenye meli iliyokumbwa na mlipuko wa ugonjwa huo. Haya yameelezwa leo bungeni na Waziri wa Afya wa nchi hiyo.
-
Iran yazindua utaratibu mpya wa kudhibiti meli zinazopita Mlango Bahari wa Hormuz
May 06, 2026 08:07Iran imezindua rasmi mfumo mpya wa udhibiti wa usafiri wa majini katika Mlango Bahari wa Hormuz.
-
Marekani yatuhumiwa kulazimisha makubaliano ya afya na mikataba ya madini nchini Zambia
May 06, 2026 08:04Zambia imeishutumu Marekani kwa jaribio la kuhusisha makubaliano ya ufadhili wa sekta ya afya na mikataba ya uchimbaji madini yake ya kimkakati. Hayo yamebainika baada ya balozi wa Marekani anayemaliza muda wake kuikosoa serikali ya Zambia kwa madai ya ufisadi, udhaifu wa utawala, na ukosefu wa ushirikiano na programu za misaada ya Marekani.
-
Qalibaf: Hali katika Mlango Bahari wa Hormuz imekuwa “isiyovumilika” kwa Marekani
May 06, 2026 07:57Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu yaani Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ameonya kwamba hali inayoendelea katika Mlango Bahari wa Hormuz imekuwa “isiyovumilika” kwa Marekani, huku akisisitiza kuwa Tehran “bado haijaanza hata hatua zake halisi.”
-
Njozi za Marekani Kujiona Dola Lenye Nguvu za Kipekee Zimefikia Ukingoni?
May 05, 2026 14:02Profesa Jeffrey Sachs wa Chuo Kikuu cha Columbia amesema: "Vita vya Iran ndio wakati ambapo dhana ya Marekani kuwa dola lenye nguvu za kipekee ilikumbana na ukweli halisi."
-
Iran yatibua mpango wa Trump kuhusu Kombe la Dunia
May 05, 2026 11:51Iran imevuruga mipango ya Rais wa Marekani, Donald Trump, si tu katika nyanja za uchumi, siasa na masuala ya kijeshi kufuatia mvutano kati ya pande hizo mbili, bali pia katika mradi unaohusiana na Kombe la Dunia FIFA 2026.
-
Trump ataka kufichwa picha za vituo vya Marekani vilivyoharibiwa na Iran
May 05, 2026 11:44Donald Trump, Rais wa Marekani, amezitaka kampuni za satalaiti kuficha picha za vituo na kambi za kijeshi za Marekani zilizoharibiwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika eneo la Asia ya Magharibi.
-
Sudan yazituhumu Imarati na Ethiopia kushambulia uwanja wa ndege wa Khartoum
May 05, 2026 11:41Sudan leo Jumanne imrudisha nyumbani balozi wake nchini Ethiopia kwa mashauriano na kuzituhutumu Ethiopia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kuwa zimehusika na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) katika uwanja wa ndege wa Khartoum.