-
Afghanistan: Shambulio la Pakistan limeua watoto tisa na mwanamke mmoja mkoani Khost
Nov 26, 2025 03:00Msemaji wa serikali ya muda ya Afghanistan inayoongozwa na Taliban Zabihullah Mujahid, amesema watoto tisa na mwanamke mmoja wameuawa baada ya vikosi vya jeshi la Pakistan kushambulia nyumba moja katika jimbo la Khost kusini mashariki mwa nchi hiyo.
-
UNDP: Familia 9 kati ya 10 Afghanistan zinasamehe matibabu ili kupata mlo huku zikibeba madeni
Nov 12, 2025 11:11Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) limetangaza kuwa, familia tisa kati ya 10 nchini Afghanistan zinakabiliwa na njaa au zinalazimika kubeba madeni huku raia wakimbizi waliorejea hivi karibuni wakijikimu kimaisha kwa tabu katika maeneo yenye hali mbaya ya umaskini mashariki na kaskazini mwa nchi hiyo.
-
Utafiti: Kilimo cha mihadarati ya afyuni nchini Afghanistan kimepungua kwa 20% katika mwaka 2025
Nov 07, 2025 10:17Utafiti mpya uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Madawa ya Kulevya na Uhalifu UNODC umeonyesha kupungua kwa kiasi kikubwa kwa kilimo cha mmea wa afyuni (Opium) nchini Afghanistan katika mwaka huu wa 2025, hali inayoashiria mabadiliko makubwa katika uzalishaji na biashara ya mihadarati katika ukanda huo.
-
Madai yasiyo na msingi ya Trump ya eti ushindi wa Marekani katika vita vyote; ni kujisahaulisha matukio ya Afghanistan na Iraq?
Oct 31, 2025 03:13Rais wa Marekani, Donald Trump, amedai kwamba nchi hiyo itashinda kama itaingia vitani na nchi yoyote.
-
Mapigano makali yazuka kati ya majeshi ya Pakistan na Afghanistan kwenye mpaka wa nchi mbili
Oct 12, 2025 05:24Mapigano makali ya mpakani yamezuka kati ya majeshi ya Afghanistan na Pakistan huku vikosi vya nchi hizo mbili vikishambuliana kwa kutumia silaha nzito.
-
Afghanistan; kutoka kwenye medani ya vita hadi kugeuzwa uwanja wa ushindani wa kijiopolitiki
Oct 11, 2025 02:25Miaka minne tangu ilipojiondoa Marekani, kwa mara nyingine tena Afghanistan imegeuzwa nukta kuu inayoangaziwa na madola yenye nguvu duniani.
-
Mapitio ya jinai za Magharibi na Marekani katika kipindi cha miaka 20 ya kukaliwa kwa mabavu Afghanistan
Oct 08, 2025 02:41Moja ya jinai muhimu zaidi zilizofanywa na Marekani katika karne ya 21 ni kuikalia kwa mabavu Afghanistan kwa miaka 20 na uhalifu wake nchini humo.
-
Trump atoa vitisho dhidi ya Afghanistan endapo Taliban haitaikabidhi US kituo cha anga cha Bagram
Sep 21, 2025 03:24Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kuchukua hatua kali ambazo hakuzitaja iwapo serikali ya Taliban nchini Afghanistan itakataa kukabidhi kituo cha jeshi la anga cha Bagram, ambacho kilitelekezwa wakati majeshi ya Marekani. yalipoondoka kifedheha katika ardhi ya nchi hiyo.
-
Taliban yamjibu Trump: Tunaweza kuzungumza, lakini Marekani haitaruhusiwa kuwepo tena kijeshi Afghanistan
Sep 19, 2025 11:05Serikali ya Afghanistan inayoongozwa na Taliban imetupilia mbali wito wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kutaka jeshi la nchi hiyo lirejee Afghanista na kupatiwa tena kambi ya jeshi la anga ya Bagram.
-
Afghanistan yaendelea kuwasaka manusura huku walioaga dunia kufuatia zilzala nchini humo wakifika 1,100
Sep 02, 2025 11:21Idadi ya waliofariki dunia kutokana na tetemeko la ardhi lililoikumba Afghanistan imefikia 1,124. Taasisi ya Hilali Nyekundu la Afghanistan imeripoti kuwa timu za uokoaji zinaendelea kuzunguka eneo la milimani la nchi hiyo kutafuta manusura.