-
Ufaransa yaendea kuingilia mambo ya ndani ya Afrika, yatuma mamia ya askari eneo la Sahel
Feb 02, 2020 10:16Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa ametangaza kuwa nchi hiyo itatuma wanajeshi wengine 600 katika eneo la Sahel barani Afrika, hatua ambayo imetajwa na wafuatiliaji wa mambo kuwa ni katika kuendeleza sera za mkoloni huyo wa zamani za kuzidisha ushawishi na satua yake barani humo.
-
Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) inalenga kupanua wigo wa makabiliano na Russia, China
Jan 29, 2020 03:10Katika zama za utawala wa Rais Donlad Trump, Marekani imekithirisha makabiliano na Russia na China ambazo ni washindani wake wakuu katika uga wa kimataifa. Sera hiyo ya utawala wa Trump ilitiliwa mkazo katika Waraka wa Kistratijia wa Usalama wa Taifa la Marekani mwaka 2018.
-
Museveni akiongea kwa hasira: Haikupasa nchi za Kiafrika ziruhusu nchi za Magharibi ziishambulie Libya
Jan 23, 2020 04:47Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda amesema, haikupasa nchi za Kiafrika ziruhusu nchi za Magharibi ziishambulie kijeshi Libya na kupelekea kuuawa aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi.
-
Wacomoro washiriki uchaguzi wa Bunge uliosusiwa na vyama vya upinzani
Jan 19, 2020 10:51Wananchi wa visiwa vya Comoro leo Jumapili wameshiriki katika awamu ya kwanza ya zoezi la uchaguzi wa Bunge uliosusiwa na vyama vya upinzani.
-
Watu milioni 45 wakabiliwa na njaa ambayo haijawahi kushuhudiwa kusini mwa Afrika
Jan 18, 2020 01:28Watu zaidi ya milioni 45 wengi wakiwa wanawake na watoto katika nchi 16 za Kusini mwa Afrika wanakabiliwa na hali mbaya ya kutokuwa na uhakika wa chakula kufuatia kujirudia kwa hali ya ukame, kusambaa kwa mafuriko na kuyumba kwa uchumi.
-
Ghana: Tuko tayari kujiunga na mfumo wa sarafu moja ya eco ya nchi za Afrika Magharibi
Dec 30, 2019 23:16Ghana imetangaza kuwa, imeamua kujiunga na Muungano wa Kiuchumi na Kifedha wa Afrika Magharibi (UEMOA) wa kutumia sarafu moja itakayojulikana kama eco.
-
Ufaransa iliua makumi ya maelefu ya raia wa Cameroon katika zama za ukoloni
Dec 28, 2019 23:22Askari wa utawala wa kikoloni wa Ufaransa waliua makumi ya maelfu ya raia wa Cameroon katika zama za ukoloni wake katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
-
Kuongezeka harakati za makundi ya kigaidi magharibi mwa Afrika
Dec 28, 2019 23:22Makundi ya kigaidi ya Boko Haramu na Daesh yamezidisha harakati zao katika eneo la magharibi mwa Afrika.
-
Uamuzi wa nchi 8 za magharibi mwa Afrika wa kuacha kutumia sarafu ya Ufaransa
Dec 24, 2019 23:26Baada ya mashauriano yaliyodumu kwa muda mrefu, hatimaye nchi nane kati ya 15 wanachama wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Magharibi mwa Afrika (ECOWAS) zimejitoa katika muungano wa sarafu ya pamoja ya Ufaransa (Franc) na kutangaza kwamba, kuanzia sasa zitaanza kufanya miamala yao yote kwa kutumia sarafu ya Eco ili zisalimike madhara ya kifedha yaliyokuwa yakisababishwa na sarafu ya Franc.
-
Kikao cha 33 cha viongozi wa Umoja wa Afrika kujadili 'kuzima milio ya risasi'
Dec 24, 2019 23:25Mkutano wa 33 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika unatarajiwa kufanyika kuanzia Januari 21 hadi Februari 10 mwakani kwenye makao makuu ya Umoja huo mjini Addis Ababa, Ethiopia, ukiwa na kauli mbiu ya "Kuzima Milio ya Risasi: Kuanzisha Mazingira Mazuri kwa ajili ya Maendeleo ya Afrika."