-
Yoweri Museveni ataka viongozi wa "maisha" watawale Afrika, wapinzani wapinga
May 13, 2019 09:58Rais Yoweri Museveni wa Uganda ameyataka mataifa ya Afrika yaondoe sheria zinazowazuia viongozi wenye umri mkubwa na waiotawala muda mrefu kuwania urais katika nchi zao. Ametoa mwito huo mwezi mmoja baada ya Mahakama ya Juu nchini Uganda kuunga mkono hatua ya bunge la nchi hiyo ya kuondoa ukomo wa kuwania urais nchini humo, ili kumpa nafasi Museveni ya kuendelea kuwa rais.
-
Iran na Afrika Kusini kuimarisha ushirikiano wao wa kiulinzi
May 06, 2019 06:35Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Afrika Kusini zimetoa mwito wa kuimarishwa ushirikiano wa muda mrefu wa kiulinzi na kijeshi baina yao.
-
Viongozi wa dunia washiriki Kongamano la Barabara ya Hariri, China; Marekani yatengwa
Apr 27, 2019 03:08Zaidi ya viongozi 40 na wajumbe elfu tano kutoka nchi mbalimbali duniani wanakongamana katika Mkutano wa "Ukanda Mmoja na Njia Moja" katika mji mkuu wa China, Beijing uliong'oa nanga hapo jana.
-
IOM: Maelfu ya wahajiri wa Kiafrika wanazuiliwa katika uwanja wa soka Yemen
Apr 26, 2019 09:56Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limeripoti kuwa, maelfu ya wahajiri wa Kiafrika wanazuiliwa katika uwanja wa mpira wa miguu katika mji wa Aden kusini mwa Yemen ambao unadhibitiwa na vikosi vya Imarati (UAE) na Saudi Arabia.
-
Reuters: Marekani na Ulaya 'zinaiba dhahabu Afrika' kupitia Imarati
Apr 24, 2019 23:50Uchunguzi uliofanywa na shirika la habari la Reuters umefichua kuwa, tani za dhahabu zenye thamani ya mabilioni ya dola zinasafirishwa kila mwaka kwa njia za magendo kutoka Afrika kuelekea Marekani na nchi za Ulaya, huku Umoja wa Falme za Kiarabu ukitajwa kuwa lango kuu la biashara hiyo haramu.
-
Ukimwi unaua Waethiopia 16,000 kila mwaka
Mar 28, 2019 03:29Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa Waethiopia zaidi ya elfu 16 wanafariki kila mwaka kutokana na ugonjwa wa Ukimwi.
-
Kesi za kipindupindu zaripotiwa huku baa la njaa, maradhi yakiwanyemelea manusura wa kimbunga Afrika
Mar 23, 2019 03:11Kesi kadhaa za watu waliokumbwa na ugonjwa wa kipindupindu zimeripotiwa katika mji wa Beira nchini Msumbiji, hivyo kuzidisha uwezekano wa ugonjwa huo hatari kuwakumba mamia ya maelfu ya watu wanaotaabika kutafuta hifadhi, chakula na maji kufuatia mafuriko ya gharika yaliyosababishwa na kimbunga cha Idai.
-
Idadi ya waliokufa katika kimbunga cha Idai kusini mwa Afrika yafikia watu 215
Mar 18, 2019 11:03Idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na kimbunga cha Idai kilichopiga katikati ya Msumbiji wiki iliyopita imeshafikia 215. Kimbunga hicho kimefika pia Zimbabwe na Malawi na kusababisha mafuriko na uharibifu mkubwa.
-
Afrika yataka kupanua ushirikiano wa kielimu na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Mar 11, 2019 13:21Kamishna wa Umoja wa Afrika Anayeshughulikia Rasilimali Watu, Sayansi na Teknolojia amesema kuna haja ya kuweko ushirikiano wa kieliimu na Iran katika sekta ya teknolojia ya Nano, sayansi ya mazingira, teknolojia ya mawasiliano, kozi za stadi, ajira na uboreshaji wa kiwango cha elimu.
-
Kamati ya Pamoja ya Iran na Afrika Kusini; kikao kwa ajili ya mashauriano ya kisiasa na kiuchumi
Mar 09, 2019 08:17Kamati ya Tisa ya Kisiasa kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Afrika Kusini imefanya kikao nchini Afrika Kusini na kuhudhuriwa na Sayyid Abbas Araqchi, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Bi Reginah Mhaule, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini Anayehusika na Masuala ya Ushirikiano na Uhusiano wa Kimataifa.