-
Walid Al-Muallim: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni mshirika katika ushindi wa Syria
Aug 02, 2017 14:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni mshirika katika ushindi unaopatikana kwenye medani za kupambana na ugaidi nchini Syria.
-
Iran: Tupo tayari kutuma dawa na timu ya madaktari Palestina
Jul 24, 2017 07:09Msaidizi Maalumu wa Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge) katika Masuala ya Kimataifa amesema Iran iko tayari kutuma dawa ili kuwasaidia haraka raia wa Kipalestina waliojeruhiwa hivi karibuni na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni katika msikiti wa al Aqsa.
-
Iran: Kama si juhudi za Hizbullah, genge la Daesh lingekuwa limezitwaa nchi za Kiarabu
Jul 19, 2017 14:13Msaidizi Maalumu wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kimataifa amesema kuwa, lau kama si msaada wa harakati ya Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon, katika kupambana na kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) nchini Syria, basi kundi hilo lingekuwa linapeperusha bendera zake katika nchi za Kiarabu.
-
Dunia yalaani hatua ya Israel kuufunga Msikiti wa al-Aqsa
Jul 15, 2017 12:56Nchi za Kiislamu duniani zinaendelea kulaani hatua ya utawala haramu wa Israel ya kuufunga Msikiti wa al Aqsa katika mji wa Quds Tukufu (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu baada ya oparesheni ya Wapalestina dhidi wanajeshi wa Kizayuni karibu na msikiti huo.
-
Amir-Abdollahian: Mazungumzo ndio njia pekee ya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa Bahrain
May 21, 2017 13:47Msaidizi Maalumu wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kimataifa amesema katika radiamali yake kwa hukumu ya mwaka mmoja iliyotolewa na mahakama ya Bahrain dhidi ya Ayatullah Issa Qassemi mwanazuoni mashuhuri wa nchi hiyo kwamba, hatua hiyo ya ghadhabu ya kimahakama haisaidii chochote katika kuupatia ufumbuzi mgogoro wa nchi hiyo.
-
Utawala haramu wa Israel hauna nafasi aktika mustakabali wa Mashariki ya Kati
Apr 28, 2017 14:40Katibu Mkuu wa Kongamano la Kimataifa la Kuunga Mkono Intifadha ya Palestina amesema: "Maadui hatimaye watasalimu amri kuhusu utatuzi wa kisiasa wa kadhia ya Syria na kwa yakini utawala haramu na wa kigaidi wa Israel hauna nafasi katika mustakabali wa Mashariki ya Kati."
-
Abdollahian: Kukombolewa mji wa Palmyra ni ishara kuwa magaidi wamefikia mwisho wao
Mar 03, 2017 07:39Msaidizi maalumu wa Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu nchini Iran (Bunge) katika masuala ya kimataifa amesema kuwa, kukombolewa kikamilifu mji wa kihistoria wa Palmyra katika mkoa wa Homs, magharibi mwa Syria, ni ishara ya wazi kwamba magaidi wamefikia mstari wa mwisho wa uhai wao.
-
Amir-Abdollahian: Waislamu wanaunga mkono azimio la kupinga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni Palestina
Mar 02, 2017 07:46Katibu Mkuu wa Mkutano wa Kimataifa wa Kuunga Mkono Palestina amesema kuwa, nchi za Kiislamu kwa pamoja zinaunga mkono azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la kupinga ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi unaofanywa na utawala haramu wa Israel huko Palestina.
-
Rais Bashar al-Assad: Iran ni muungaji mkono mkuu wa taifa la Syria
Jan 26, 2017 13:35Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, Iran imekuwa muungaji mkono mkuu wa taifa la Syria katika kipindi chote cha mgogoro wa nchi hiyo uliodumu kwa miaka sita sasa.
-
Abdollahian: Aleppo inaelekea kusafika kutokana na uepo wa makundi ya kigaidi
Nov 29, 2016 14:03Hossein Amir-Abdollahian, msaidizi maalumu wa Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (bunge), katika masuala ya kimataifa, amesema kuwa hivi sasa mji wa Aleppo, kaskazini mwa Syria unaelea kusafika kutokana na uepo wa makundi ya kigaidi na kitakfiri.