-
Dkt. Velayati: Kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel ni khiyana kwa wananchi wa Palestina
Sep 14, 2020 02:41Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Mwamko wa Kiislamu amelaani hatua ya Bahrain ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel na kusisitiza kuwa, hatua hiyo ni upuuzaji na khiyana kwa malengo ya wananchi madhulumu wa Palestina.
-
Machaguo iliyonayo Palestina kwa ajili ya kukabiliana na kuanzishwa uhusiano na Israel
Sep 14, 2020 02:36Baada ya Imarati na Bahrain kuutambua rasmi utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na kuwa tayari kuanzisha uhusiano wa kawaida wa kidiplomasia na utawala huo ghasibu unaoikalia Quds tukufu kwa mabavu, suali linaloulizwa hivi sasa ni, hatua gani Palestina inaweza kuchukua kwa ajili ya kukabiliana na mwenendo huo?
-
Picha za watawala wa Bahrain na Imarati zachomwa moto Ghaza, Palestina
Sep 13, 2020 07:41Wakazi wa Ukanda wa Ghaza huko Palestina wamechoma moto picha za watawala wa Bahrain na Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) kutokana na nchi hizo mbili za Kiarabu kutangaza uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Iran: Kuanzisha uhusiano na Israel ni fedheha na kujidhalilisha
Sep 12, 2020 11:31Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imekosoa hatua ya kuanzishwa uhusiano rasmi wa kidiplomasia kati ya Bahrain na utawala haramu wa Israel na kusisitiza kuwa, kitendo hicho ni cha fedheha na kudhalilisha.
-
Mapatano ya Aal Khalifa na utawala wa Kizayuni, chachu ya mapambano ya wananchi wa Bahrain
Sep 12, 2020 11:01Ikiwa umepita karibu mwezi mmoja tangu Imarati na utawala wa Kizayuni wa Israel zifikie mapatano ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia, Rais Doald Trump wa Marekani ametangaza kwamba Bahrain na utawala wa Kizayuni pia zimekubaliana kuanzisha uhusiano kama huo.
-
Sheikh Issa Qassem: Wafuatao nyayo za Imam Hussein AS wanakabiliana na mtihani mkubwa
Aug 30, 2020 07:39Kiongozi wa juu wa kidini wa Waislamu wa madhehebu ya Shia wa nchini Bahrain amesema, kupambana na ufanyaji mapatano na Israel ni mfano mmojawapo wa mapambano ya Imam Hussein AS dhidi ya Yazid.
-
Safari ya Mike Pompeo kusini mwa Ghuba ya Uajemi na kukaririwa madai yasiyo na msingi wowote
Aug 28, 2020 06:29Marekani daima ikiwa na lengo la kuendeleza uwepo wake wa kijiopolitiki katika eneo la Ghuba ya Uajemi imekuwa ikitumia vizingizio visivyokuwa na maana hususan kupiga kwake ngoma ya kueneza chuki chidi ya Iran.
-
Wabunge wa Ufaransa wataka Bahrain ifutilie mbali hukumu ya kunyongwa vijana wawili wa nchi hiyo
Jul 28, 2020 11:26Wabunge wa Ufaransa wameuandikia barua utawala wa Aal Khalifa wa Bahrain wakiutaka ufutilie mbali hukumu ya kunyongwa vijana wawili wa nchi hiyo.
-
Sheikh Isa Qassim: Uislamu unahujumiwa nchini Bahrain
Jul 28, 2020 04:42Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Bahrain Sheikh Isa Ahmed Qassim ametahadharisha kuhusu njama zinazofanywa na maadui kwa ajili ya kupotosha na kuhariibu sura safi ya Uislamu na kusema kuwa, dini ya Uislamu inahujumiwa na kushambuliwa nchini Bahrain.
-
Jumuiya 16 za kimataifa zaiandikia barua Bahrain na kuitaka isiwanyonge raia
Jul 23, 2020 13:00Jumuiya 16 za kimataifa zimemuandikia barua mfalme wa Bahrain Hamad bin Isa bin Salman al-Khalifa zikimtaka azuie utekelezaji wa adhabu ya kifo dhidi ya vijana wawili kwa kosa la kuwashambulia polisi.