-
Upinzani Bahrain wataka kutimuliwa nchini humo vikosi vya jeshi la Marekani
Apr 07, 2022 01:57Kundi moja la upinzani nchini Bahrain limelaani uwepo wa vikosi vya majini vya Marekani nchini humo na kusisitiza kuwa, wakati umefika wa kufunga kambi ya kijeshi na kuwafukuza wanajeshi wa US katika nchi hiyo ya Ghuba ya Uajemi.
-
Machi 14, 2022; mwaka wa 11 wa uvamizi wa kijeshi wa Saudia huko Bahrain
Mar 16, 2022 00:35Mnamo Machi 14, 2011, Saudi Arabia iliivamia rasmi Bahrain chini ya kivuli cha Ngao ya Kisiwa, uvamizi ambao sasa umeingia katika mwake wake wa 11.
-
Wabahrain waandamana kulaani safari ya mkuu wa majeshi ya Israel
Mar 11, 2022 08:08Wananchi wa Bahrain wamefanya maandamano ya kulaani safari ya Luteni Jenerali Aviv Kochavi, Mkuu wa Majeshi ya Israel nchini humo, sanjari na kulaani hatua ya utawala wa Aal-Khalifa wa nchi hiyo ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel.
-
Mfalme wa Bahrain atembelea Saudia mkesha wa mwaka wa 11 wa kampeni ya kijeshi
Mar 05, 2022 02:44Katika hali ambayo siku 10 zijazo itatimia miaka 10 tokea utawala wa Saudi Arabia utume wanajeshi wake Bahrain katika kampeni ya kukandamiza wananchi, mfalme wa Bahrain Hamad bin Isa Aal Khalifa ametembelea Saudia na kufanya mazungumzo na watawala wa Riyadh.
-
Bendera za Israel zateketezwa kwa moto Bahrain kulaani safari ya Bennett
Feb 17, 2022 02:37Waandamanaji wenye hasira nchini Bahrain wameteketeza kwa moto bendera za utawala wa Kizayuni wa Israel wakilaani safari ya siku mbili ya Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel, Naftali Bennet katika nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi.
-
Al Wifaq: Safari ya Bennet mjini Manama ni hiyana ya utawala wa Aal Khalifa kwa wananchi wa Bahrain
Feb 16, 2022 11:53Jumuiya ya kitaifa na Kiislamu nchini Bahrain ya Al-Wifaq imeitaja safari ya Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni huko Manama mji mkuu wa Bahrain kuwa ni hiyana ya utawala wa Aal Khalifa kwa watu wa nchi hiyo na kusisitiza kuwa, safari hiyo inakiuka maadili na ni kitendo chenye lengo la kuyachochea mataifa ya Kiarabu na Kiislamu.
-
Safari ya Waziri Mkuu wa Israel Bahrain katika siku ya kumbukumbu ya mwamko wa Februari 14
Feb 16, 2022 11:04Naftali Bennett Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel hivi karibuni amefanya safari huko Bahrain kwa mwaliko rasmi wa Mfalme Hamad bin Isa wa nchi hiyo, ikiwa ni katika kumbukumbu ya mwaka wa 11 wa mwamko wa watu wa nchi hiyo dhidi ya utawala wa kidikteta wa Aal Khalifa.
-
Mwaka wa 11 wa mwamko wa wananchi; mpasuko kati ya ukoo wa Al Khalifa na watu wa Bahrain waongezeka
Feb 14, 2022 12:31Februari 14, 2022 inasadifiana na kumbukumbu ya miaka 11 ya mwamko na vuguvugu la watu wa Bahrain dhidi ya utawala wa Al Khalifa.
-
Sheikh Qassim: Waislamu wakabaliane na mwenendo wa kuanzishwa uhusiano na Israel
Feb 14, 2022 07:44Kiongozi wa Waislamu wa Kishia nchini Bahrain ametoa wito wa kusimama kidete Waislamu katika kukabiliana na mwenendo wa kuanzishwa uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
-
Al-Wifaq: Wananchi wa Bahrain wataendelea kudai haki zao kwa njia ya amani
Jan 13, 2022 11:41Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Mwafaka wa Kiislamu na Kitaifa nchini Bahrain (Al Wifaq) amesema kuwa, wananchi wa nchi hiyo wataendelea kudai haki zao kwa njia ya amani na kwamba, katu hawatasalimu amri katika njia hiyo.