Mar 15, 2018 14:55
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, kusimama imara na mafanikio ya Iran katika kukabiliana na hujuma za mrengo mkubwa wa kisiasa, kifedha, kijeshi, kiusalama na kiutamaduni wa Marekani na Israel, kunatokana na baraka za kuwepo imani na ucha-Mungu baina ya matabaka ya wananchi na vijana wa Iran.