-
Araghchi: Mashauriano ya Beijing yamefanikiwa; Iran yathamini “ushirikiano wa kimkakati” na China
Sep 17, 2026 12:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameelezea mashauriano yake mjini Beijing kama “yaliyofanikiwa,” akizungumzia maudhui ya safari yake katika mji mkuu huo wa China, ambapo alikutana na mwenzake, Wang Yi.
-
China yatoa onyo kwa Japan, yakosoa mazoezi ya pamoja ya kijeshi inayofanya kila mara na Marekani
Sep 15, 2026 10:36China imekosoa hatua ya Japan ya kutangulia kupanga silaha za kimkakati za ushambuliaji na vilevile kwa mazoezi ya kijeshi inayoendelea kufanya kila mara kwa kushirikiana na Marekani na Australia, ikisema, vitendo hivyo vinaongeza hatari ya makabiliano katika eneo hilo.
-
China yapinga vitisho vya Marekani na vikwazo haramu dhidi ya nchi zinazofanya biashara na Iran
Aug 26, 2026 03:27China imepinga vitisho vya Marekani vya kuziwekea vikwazo nchi zinazofanya biashara na Iran, ikisema kuwa ushirikiano wa Beijing na Tehran unafanyika kwa mujibu wa sheria za kimataifa na haupaswi kuvurugwa.
-
Russia yaanza mazoezi ya nyuklia ya siku 3 huku Putin akitarajiwa nchini China kwa ziara ya siku mbili
May 20, 2026 02:57Russia imezindua mazoezi makubwa ya silaha za nyuklia yanayohusisha makumi ya maelfu ya wanajeshi, huku mapigano na Ukraine yakizidi kuwa makali na Rais Vladimir Putin akielekea China kwa ziara ya siku mbili.
-
Kiongozi wa Wachache wa Seneti ya Marekani: Safari ya Trump nchini China Ilikuwa fedheha tupu
May 16, 2026 11:59Chuck Schumer, Kiongozi wa Wachache katika Seneti ya Marekani, amesema kwamba safari ya Rais Donald Trump nchini China haikuwa na mafanikio yoyote kwa watu wa Marekani na ilikuwa fedheha kamili.
-
China yaionya Marekani kuhusu mauzo ya silaha kwa Taiwan
May 14, 2026 03:20China kwa mara nyingine tena imepinga vikali hatua ya Marekani kuzidisha himaya na uungaji mkono wake wa kijeshi kwa Taiwan sambamba na ziara ya Rais Trump mjini Beijing.
-
China yakataa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran, yaapa kulinda kampuni zake
May 12, 2026 03:59China imepinga vikali vikwazo vipya vilivyowekwa na Marekani dhidi ya kampuni zake tatu kwa madai ya kusaidia shughuli za kijeshi za Iran, na imeahidi kulinda biashara zake dhidi ya hatua hizo ambazo imezitaja kuwa za upande mmoja na zisizo halali.
-
China yalaani vita dhidi ya Iran, yataka usitishaji kamili wa mapigano
May 07, 2026 08:03China imemkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, kwa mazungumzo mjini Beijing, huku Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi, akivitaja vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kuwa “visivyo halali” na kutoa wito wa kusitishwa kabisa kwa mapigano.
-
Ripoti: Ajali ya ndege ya China mwaka 2022 iliyoua watu 132 huwenda ilikuwa ya makusudi
May 05, 2026 11:39Televisheni ya CNN imeripoti kuwa, ikiwa imepita zaidi ya miaka minne baada ya ndege ya abiria ya Boeing 737-800 kuanguka mlimani kusini mwa China na kuua watu wote 132 waliokuwa ndani yake, data iliyotolewa hivi karibuni "imeashiria kwambs upo uwezekano mtu aliyekuwa katika chumba cha marubani alizima usambazaji wa mafuta katika injini kwa makusudi.
-
Beijing yasisitiza kuendelezwa juhudi za usuluhishi ili kurejesha amani Magharibi mwa Asia
Mar 20, 2026 07:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China amesema kuwa mashambulizi yanayoendelea katika eneo la Magharibi mwa Asia yamevuruga usafirishaji wa baharini na kwamba Beijing itaendeleza juhudu za usuluhishi ili kufanikisha usitishaji vita na kukomesha uhasama ili kurejesha amani na utulivu katika eneo la Magharibi mwa Asia haraka iwezekanavyo.