-
Colombia yawatimua wanadiplomasia wa Israel kwa kuvamiwa msafara wa Sumud, yasema Trump ni wa kufungwa jela
Oct 01, 2025 23:55Colombia imewafukuza wanadiplomasia wa utawala wa kizayuni wa Israel kwa uchokozi uliofanywa na utawala huo ghasibu wa kuuvamia kijeshi msafara wa kimaataifa wa meli unaojulikana kama Sumud uliokuwa ukielekea Ukanda wa Ghaza kwa ajili ya kufikisha misaada ya kibinadamu; sambamba na hilo, serikali ya Bogota imehimiza rais wa Marekani Donald Trump afungwe jela kwa ushiriki wa Washington katika mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na jeshi la kizayuni katika eneo hilo la ardhi ya Palestina.
-
Trump awaita 'wapumbavu' washirika wa Marekani wa Ulaya walioitambua nchi ya Palestina
Sep 30, 2025 03:34Rais wa Marekani Donald Trump amewashambulia vikali kwa kuwaita wapumbavu washirika wakuu wa Ulaya wa nchi hiyo ikiwemo Uingereza na Ufaransa kwa kuitambua rasmi nchi ya Palestina.
-
China haina wasiwasi, bali inashangaa; mbona Marekani inang'ang'ania kurejea Afghanistan?
Sep 29, 2025 04:02China imetangaza kwamba, njama za madola yaliyosababisha mgogoro wa Afghanistan za kujaribu kurejea nchini humo na kuweka kambi zao za kijeshi ni hatari kwa usalama wa ukanda mzima.
-
Kwa nini Trump anaishupalia jamii ya kimataifa iamini uwongo wake kuhusu Iran?
Sep 27, 2025 07:40Rais wa Marekani kwa mara nyingine tena amekariri katika houba aliyoitoa katika Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa madai yake ya uwongo na yasiyo na msingi dhidi ya Iran.
-
Politico: Trump amewaambia viongozi wa nchi za Kiislamu hatairuhusu Israel iutwae Ukingo wa Magharibi
Sep 25, 2025 03:11Tovuti ya habari ya Politico imeripoti kuwa, katika mkutano wa faragha aliofanya Rais wa Marekani Donald Trump na viongozi wa nchi kadhaa za Kiarabu na Kiislamu, rais huyo wa Marekani aliwaahidi viongozi hao kwamba, hatamruhusu waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu autwae kikamilifu Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu na utawala huo.
-
Russia yajibu mapigo kwa Trump baada ya kuiita 'chui wa karatasi', yasema chaguo pekee ni vita
Sep 25, 2025 00:42Ikulu ya Kremlin imetangaza kuwa Russia haina "mbadala" isipokuwa kuendelea kupigana vita, huku ikijibu mapigo kwa mabadiliko ya ghafla yaliyoonyeshwa dhidi ya nchi hiyo na Rais wa Marekani Donald Trump mkabala wa Ukraine kwa kufikia hadi ya kuiita Moscow "chui wa karatasi".
-
Trump azishambulia China na India kwa kuziita 'wafadhili wakuu' wa vita vya Ukraine
Sep 25, 2025 00:42Rais wa Marekani Donald Trump amezituhumu India na China kuwa "zinafadhili kifedha" vita vya Ukraine kupitia uagizaji wa nishati kutoka Russia. Trump ametoa shutuma hizo katika hotuba yake kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa unaoendelea mjini New York.
-
Kwa nini Waziri Mkuu wa India amewataka wananchi kutumia bidhaa za ndani?
Sep 24, 2025 07:38Waziri Mkuu wa India amewataka wananchi wa nchi hiyo kuacha kutumia bidhaa kutoka nje na badala yake watumie bidhaa za ndani kufuatia kushtadi mivutano katika uhusiano wa nchi hiyo na Marekani.
-
White House: Trump atakutana na viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu kujadili kadhia ya Ghaza
Sep 23, 2025 03:27Msemaji wa ikulu ya White House Karoline Leavitt ametangaza kuwa rais wa Marekani Donald Trump anatazamiwa kufanya mkutano na viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu kujadili kadhia ya Ghaza.
-
Trump atoa vitisho dhidi ya Afghanistan endapo Taliban haitaikabidhi US kituo cha anga cha Bagram
Sep 20, 2025 23:54Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kuchukua hatua kali ambazo hakuzitaja iwapo serikali ya Taliban nchini Afghanistan itakataa kukabidhi kituo cha jeshi la anga cha Bagram, ambacho kilitelekezwa wakati majeshi ya Marekani. yalipoondoka kifedheha katika ardhi ya nchi hiyo.