-
UN: Tangu Mei, Wapalestina 1,500 wameuawa Ghaza wakihangaika kupata msaada wa chakula
Aug 05, 2025 07:11Umoja wa Mataifa umesema Wapalestina 1,500 wameuawa huko Ghaza tangu mwezi Mei hadi sasa wakati wanahangaika kutafuta msaada wa kibinadamu.
-
Nyaraka za UK: Mubarak aliidhinisha mpango wa US na UK wa 'kumdhalilisha' Saddam Kuwait
Aug 03, 2025 05:40Nyaraka za siri za Uingereza zilizowekwa hadharani hivi karibuni zimefichua kwamba rais wa zamani wa Misri, Hosni Mubarak, aliunga mkono mpango wa Marekani na Uingereza wa kumshinda kijeshi na kumdhalilisha Saddam Hussein wakati wa Vita vya Ghuba ya Uajemi, huku akitabiri pia kwamba kushindwa huko kijeshi kungepelekea kuanguka kiongozi huyo wa Iraq.
-
Sweden: Ukraine lazima iseme 'ndiyo' kwa ndoa za jinsia moja kama sharti la kujiunga na EU
Aug 02, 2025 11:48Waziri Mkuu wa Sweden Ulf Kristersson amesema, Ukraine inapaswa kutoa ulinzi kamili wa kisheria kwa 'mashoga', ikiwa ni pamoja na wa ndoa za jinsia moja, kama sehemu ya juhudi zake za kupigania kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya,
-
Trump akasirishwa na matamshi ya Medvedev
Aug 01, 2025 02:46Akijibu indhari iliyotolewa hivi karibuni na rais wa zamani wa Russia kwa White House, Rais wa Marekani amesema kuwa: " Mwambie Medvedev achunge maneno yake".
-
Waziri Mkuu wa Hungary: Tishio la kutokea Vita Vikuu vya Tatu vya Dunia linazidi kuongezeka
Jul 27, 2025 09:55Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban amesema tishio la kuzuka Vita Vikuu vya Tatu vya Dunia linazidi kuongezeka na kwamba Jamii ya Kimataifa inapaswa ifanye kila iwezalo kulizuia.
-
Kwa nini Marekani imejiondoa rasmi UNESCO?
Jul 23, 2025 08:58Marekani ilitangaza Jumanne, Julai 22, kwamba imejiondoa rasmi katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO.
-
Jibu kwa swali la leo; kwa nini Trump amewatishia tena wanachama wa BRICS?
Jul 21, 2025 12:49Rais wa Donald Trump Marekani amekariri tena tishio lake la kuzitoza ushuru wa ziada nchi wanachama wa kundi la BRICS.
-
Trump kuzisakama nchi maskini za Afrika kwa ushuru wa 10%
Jul 16, 2025 08:45Rais wa Marekani, Donald Trump anapania kupanua ajenda yake ya ushuru, akitangaza mipango ya kutoza ushuru mpya wa forodha wa zaidi ya asilimia 10 kwa bidhaa zinazoagizwa nchini humo kutoka mataifa madogo, ikiwa ni pamoja na kadhaa ya bara Afrika na eneo la Caribbean.
-
Borrell amkemea Netanyahu kwa kutaka Trump apewe Tuzo ya Amani ya Nobel
Jul 10, 2025 06:09Mkuu wa zamani wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell amekemea pendekezo la waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu la kutaka rais wa Marekani Donald Trump atunukiwe Tuzo ya Amani ya Nobel, akilielezea hilo kuwa ni hatua iliyochukuliwa na "mtu anayeaminika kuwa mhalifu wa kivita" kwa ajili ya "muuzaji wake mkuu wa silaha".
-
Rais wa Afrika Kusini ajibu bwabwaja na vitisho vya Trump
Jul 08, 2025 13:39Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amejibu matamshi ya vitisho na ubabe ya Rais wa Marekani, Donald Trump ambaye hivi karibuni alitishia kuongeza ushuru wa asilimia kwa nchi ambazo zinajiegemeza na kufungamana na "sera za kupambana na Marekani" za jumuiya ya kiuchumi ya BRICS.