-
Amri ya Trump ya kupunguza idadi ya askari wa Marekani nchini Ujerumani
Jun 07, 2020 11:55Uhusiano wa Marekani na Ujerumani katika mtazamo mpana wa kupungua uhusiano kati ya nchi za Ulaya na Marekani umekumbwa na mvutano hasa baada ya kuingia madarakani Rais Donald Trump.
-
"Trump anaongoza magaidi waliovaa tai huko White House"
Jun 06, 2020 11:40Msaidizi maalumu wa Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) katika masuala ya kimataifa amesisitiza kuwa, wananchi waliostaarabika wa Iran wanamtambua vyema mkuu wa magaidi waliovaa tai katika Ikulu ya Marekani, White House.
-
Mauaji ya George Floyd yaporomosha vibaya umaarufu wa Trump nchini Marekani
Jun 06, 2020 11:29Wimbi la maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi na unyanyasaji watu wasio wazungu linaendelea nchini Marekani huku kiwango cha umaarufu wa rais wa nchi hiyo, Donald Trump kikiporomoka vibaya na kufikia asilimia 44.
-
Spika wa Bunge la Iran amjibu Trump kwa aya ya Qurani Tukufu
Jun 06, 2020 08:11Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameashiria ujumbe wa Twitter wa Rais Donald Trump wa Marekani ambaye ametoa pendekezo la kufanyika duru mpya ya mazungumzo ya nyuklia na Tehran na kusisitiza kuwa, muqawama ndio njia pekee ya kumshinda adui.
-
Javad Zarif ajibu ujumbe wa Trump aliyeitaka Iran kuketi kwenye meza ya mazungumzo Marekani
Jun 06, 2020 02:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amejibu pendekezo la Rais Donald Trump wa Marekani kwa Tehran kwa ajili ya kufanya mazungumzo mapya akisema kuwa, Iran au pande nyingine za mapatano ya nyuklia ya JCPOA, hazijawahi kuondokwa kwenye meza ya mazungumzo.
-
Malalamiko ya UN dhidi ya ubaguzi wa rangi wa kitaasisi nchini Marekani
Jun 05, 2020 05:57Ubaguzi wa rangi na kizazi na ukandamizaji uliochupa mipaka dhidi ya watu wasio wazungu hasa wenye asili ya Afrika huko Marekani una historia ndefu na ulianza tangu ilipoasisiwa nchi hiyo karne tatu zilizopita. Ubaguzi huo daima umekuwa ni sifa inayochukiza ya jamii ya Marekani. Licha ya Wamarekani wenye asili ya Afrika kuendesha mapambano makali ya kupigania haki zao, lakini hadi leo hii wanaendelea kuwa wahanga wa ubaguzi, ukatili na ukandamizaji usio na kifani.
-
Obama ataka mageuzi Marekani, Pelosi ajiunga na waandamanaji dhidi ya ubaguzi wa rangi
Jun 04, 2020 12:46Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama ametoa wito wa kufanyika marekebisho katika mfumo wa jeshi la polisi la nchi hiyo na kusisitiza kuwa, waandamanaji wanaopinga ubaguzi wa rangi wanapaswa kuwanyima utulivu wanaoshikilia madaraka.
-
Wasiwasi wa Pentagon na hata Republican kwa hatua ya Trump ya kutumia wanajeshi kukandamiza waandamanaji Marekani
Jun 04, 2020 12:41Maandamano makubwa ambayo hayajawahi kutokea mfano wake huko Marekani yamemtia kiwewe na kumuweka kwenye hali ngumu rais wa nchi hiyo mwenye majigambo na majivuno mengi, Donald Trump na kumfanya atoe amri ya kutumiwa jeshi, suala ambalo limelalamikiwa na Wizara ya Ulinzi, lakini hata wanachama wenzake ndani ya chama cha Republican nao hawakubaliani na uamuzi wake wa kutumia nguvu za kijeshi kukandamiza waandamanaji.
-
Hata 'Mbwa Kichaa' akosoa mienendo ya Trump; zaidi ya 10,000 wakamatwa katika maandamano Marekani
Jun 04, 2020 07:55Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis maarufu kwa jina la "Mbwa Kichaa" ametangaza kuwaunga mkono wananchi wa Marekani wanaondamana kulaani ubaguzi wa rangi na mienendo ya kikatili ya polisi ya Marekani hususan dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Afrika.
-
Tishio la Trump la kutuma jeshi la taifa katika majimbo ya Marekani kukabiliana na wapinzani wa ubaguzi
Jun 03, 2020 12:32Malalamiko na maandamano makubwa ambayo hayajawahi kushuhudiwa katika miji na majimbo ya Marekani dhidi ya mauaji ya kutisha yaliyofanywa na polisi dhidi ya raia mweusi wa nchi hiyo, George Floyd huko katika jimbo la Minnesota yamezusha machafuko makubwa na kumtia kiwewe rais wa nchi hiyo, Donald Trump na serikali yake.