-
Misimamo ya kugongana ya Washington kuhusu sababu za kumuua kigaidi Luteni Soleimani
Jan 14, 2020 00:58Tarehe 3 Januari 2020, Marekani ilifanya jinai na ugaidi mkubwa wa kumuua kidhulma Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu tena akiwa mgeni rasmi wa serikali ya Iraq.
-
Trump na madai ya kizandiki ya kuwaunga mkono wananchi wa Iran
Jan 13, 2020 04:27Ijapokuwa tangu Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yalipopata ushindi mwaka 1979 Marekani siku zote imekuwa ikiamiliana kiuadui na kiuhasama na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, lakini Donald Trump, rais afriti aliyeko madarakani hivi sasa nchini humo, yeye ametia fora na kufurutu mpaka, kwa uadui ambao haujawahi kushuhudiwa, anaoifanyia Iran na wananchi wake.
-
Akthari ya Wamarekani hawaungi mkono namna Trump anavyoamiliana na Iran
Jan 12, 2020 21:07Utafiti mpya wa maoni uliofanywa na shirika la Ipsos likishirikiana na kanali ya televisheni ya ABC News ya Marekani unaonyesha kuwa, aghalabu ya wananchi wa Marekani hawaungi mkono sera ghalati za Rais Donald Trump dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran; muendelezo wa sera za mashinikizo ya juu kabisa
Jan 11, 2020 04:43Katika zama za utawala wa Rais Donald Trump, serikali ya Marekani imekuwa ikifuatilia sera za mashinikizo ya juu kabisa dhidi ya Iran na katika fremu hiyo mnamo Mei 8 2018, Washington ilitangaza kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA na baada ya hapo ikaweka vikwazo shadidi zaidi dhidi ya Iran. Pamoja na kuwa vikwazo hivyo havijafikia malengo yaliyokusudiwa, Marekani inasisitiza kuendeleza sera yake ya kushadidisha vikwazo.
-
Ulaya yapinga ombi la Trump la kujiondoa JCPOA
Jan 11, 2020 01:21Umoja wa Ulaya sambamba na nchi tatu za Ulaya za Ufaransa, Ujerumani na Uingereza zinazojulikana kama Troika ya Ulaya, ni waungaji mkono wa mapatano ya kimataifa ya nyuklia maarufu kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA.
-
Majibu ya kutapatapa ya Trump baada ya Iran kupiga kwa makombora kambi za Marekani + Video
Jan 09, 2020 07:20Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetekeleza kivitendo ahadi yake ya kutoa jibu kali kwa jinai ya Marekani ya kumuua kigaidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.
-
Uingereza yakataa ombi la Trump la kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA
Jan 09, 2020 04:32Serikali ya Uingereza imekataa ombi la Rais Donald Trump wa Marekani la kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kusema makubaliano hayo yana umuhimu kwa London katika upande wa masuala ya kiusalama.
-
Zarif: Uwepo wa kishetani wa Marekani Asia Magharibi unaelekea kufika ukingoni
Jan 07, 2020 00:58Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria kujitokeza mamilioni ya Wairani katika mazishi ya mashahidi wa jinai ya hivi karibuni ya Marekani na kusema: "Uwepo wa kishetani wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi unaelekea kufika ukingoni."
-
Zarif: Tishio la Trump dhidi ya maeneo ya kiutamaduni ya Iran ni jinai ya kivita
Jan 05, 2020 23:17Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amejibu tishio alilotoa Ras wa Marekani dhidi ya wananchi wa Iran kupitia ukurasa wake wa Twitter na kusisitiza kuwa: Tishio hilo dhidi ya maeneo ya kiutamaduni ni jinai ya kivita.
-
Vitisho vipya vya Trump kutokana na wahka wa ulipizaji kisasi wa Iran
Jan 05, 2020 23:13Hatua ya kijinai na iliyo kinyume cha sheria ya Marekani ya kumuua shahidi Jenerali Qassem Soleimani na Abu Mahdi al Muhandis Naibu Mkuu wa Harakati ya Hashdu sh-Sha'abi ya Iraq pamoja na shakhsia wengine huko mjini Baghdad, imekabiliwa na radiamali kali kutoka kwa Iran ambayo imesisitizia kulipiza kisasi kikali kwa Marekani.