-
Maandamano ya kuwaunga mkono Wagaza yafanyika Iran, Yemen
May 31, 2025 02:23Maelfu ya watu walimiminika barabarani na mitaani katika miji yote ya Iran baada ya Swala ya Ijumaa kushiriki maandamano ya kitaifa ya "Ijumaa ya Ghadhabu", wakitangaza uungaji mkono wao usioyumba kwa Wapalestina wa Gaza, na kulaani mauaji ya kimbari ya Israel katika eneo hilo lililozingirwa.
-
Muqawama walaani matamshi ya mbunge wa US anayetaka Gaza ipigwe mabomu ya nyuklia
May 25, 2025 07:10Makundi ya Muqawama ya Palestina ya Hamas na Jihadul Islami yamemlaani vikali mbunge wa chama cha Republican nchini Marekani, Randy Fine kutokana na matamshi yake ya kutaka kufanyika shambulio la nyuklia katika Ukanda wa Gaza.
-
Mbunge wa US ataka Gaza iangamizwe kwa nyuklia kama Hiroshima
May 23, 2025 11:55Mbunge wa jimbo la Florida wa chama cha Republican, Randy Fine ameashiria shambulio la bomu la nyuklia la Marekani dhidi ya Japan wakati wa Vita vya Pili vya Dunia na kutoa wito wa kuangamizwa Gaza kwa silaha za nyuklia.
-
Je, kwa nini Trump amenyamazia kimya mauaji ya kimbari huko Gaza, huku akidai yametokea Afrika Kusini?
May 23, 2025 05:57Akizungumza siku ya Jumatano katika kikao chenye mvutano na Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, Rais Donald Trump wa Marekani alichukua hatua ya kushanga kwa kumuonyesha video ya kiongozi mmoja wa mrengo wa kulia wa Afrika Kusini aliyetoa wito wa kuuawa wakulima weupe ili kuthibitisha madai yake kuhusu kile kinachodaiwa kuwa mauaji ya kimbari dhidi ya wazungu wa nchi hiyo.
-
Demokrasia ya BBC; "Uhuru wa kujieleza" ni kwa wapinzani wa Iran tu!
May 21, 2025 06:55Gary Lineker, mtangazaji mashuhuri na maarufu wa BBC, amefutwa kazi na shirika hilo baada ya miaka 26 ya utumishi kwa sababu tu ya kuwaunga mkono watu wanaodhulumiwa wa Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Sisi katika mkutano na afisa wa US, ataka kusitishwa mapigano Gaza
May 19, 2025 07:09Rais wa Misri Abdel-Fattah al-Sisi jana Jumapili alitoa wito wa kufikiwa makubaliano ya usitishaji vita mara moja katika Ukanda wa Gaza, na kuruhusu kuingia misaada ya kibinadamu katika eneo hilo lililozingirwa.
-
Israel imewaua wanahabari 219 wa Palestina Gaza ndani ya miezi 19
May 19, 2025 07:07Maafisa wa Palestina wamesema kuwa, wanajeshi wa Israel wamewauwa shahidi takriban waandishi wa habari 219 na wafanyakazi wa vyombo vya habari tangu vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo kuanza katika Ukanda wa Gaza zaidi ya miezi 19 iliyopita.
-
Misri na Djibouti zalaani mashambulizi mapya ya Israel katika Ukanda wa Gaza
Apr 24, 2025 10:47Rais wa Misri, Abdel-Fattah al-Sisi na mwenzake wa Djibouti, Ismail Omar Guelleh wametangaza uungaji mkono wao kwa juhudi za kumaliza vita katika Ukanda wa Gaza, na kulinda usalama wa baharini katika Bahari Nyekundu.
-
ICJ yaafikiana na Israel kuakhirisha kesi ya mauaji ya halaiki Gaza kwa miezi 6
Apr 18, 2025 06:45Katika hatua inayotia wasiwasi, Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) imeafiki ombi la kuakhirisha kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini dhidi ya Israel, kuhusu kampeni ya kikatili na ya kijeshi ya utawala huo wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza.
-
Kushindwa mhimili wa vita wa Kizayuni na Marekani katika vita huko Yemen na Gaza
Apr 14, 2025 10:59Licha ya mashambulizi yanayoendelea kufanywa na mhimili wa Kizayuni na Marekani dhidi ya Yemen na Gaza, bado vikosi vya jeshi la Yemen na Muqawama wa Palestina vinaendelea kukabiliana na wavamizi hao.