-
HRW: Magharibi inaendelea kuipatia Israel silaha wakati inajadili kupeleka misaada Ghaza
Mar 18, 2024 07:43Wakati wabunge katika nchi nyingi za Magharibi wanajadili ni kwa kiwango gani utawala wa Kizayuni wa Israel unaweza ukawa unakwamisha upitishaji misaada ya kuokoa maisha ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza, mauzo ya silaha ambayo yanachangia vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendeshwa na utawala huo dhidi ya eneo hilo lililowekewa mzingiro yangali yanaendelea kumiminika.
-
Jaribio la Marekani eti la kusimamisha vita huko Gaza, mbinu ya kugeuza maoni ya umma
Mar 15, 2024 12:55Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amezungumzia matukio ya hivi karibuni katika eneo la Asia Magharibi hususan Ukanda wa Gaza na kueleza kuwa hakuna anayeamini madai ya Washington ya kujaribu kusimamisha vita vya Gaza.
-
Mashambulio pacha ya jeshi la Kizayuni yaua Wapalestina 29 waliokuwa wakingojea msaada wa chakula Ghaza
Mar 15, 2024 04:27Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limewaua shahidi Wapalestina wapatao 29 wakati wakisubiri msaada katika mashambulizi mawili tofauti lililofanywa dhidi ya Ukanda wa Ghaza uliozingirwa.
-
Kiongozi Muadhamu: Kilele cha istiqama ya wananchi wa Ghaza kinatokana na kuielewa na kuifanyia kazi Qur'ani Tukufu
Mar 12, 2024 23:18Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, usomaji wa Qur'ani ni sanaa takatifu na inabidi lengo lake kuu liwe ni kuwafundisha watu na jamii maana na ujumbe uliomo kwenye Qur'ani na kuandaa mazingira ya kuzingatiwa aya za Kitabu hicho Kitakatifu kama ambavyo pia kilele cha istiqama ya wananchi wa Ghaza kinatokana na kuielewa na kuifanyia kazi Qur'ani Tukufu.
-
Wapalestina watano wauawa na misaada wa kudondoshwa kutoka angani, Gaza
Mar 09, 2024 08:19Wapalestina watano wameuawa na vifurushi vya misaada vilivyodondoshwa na ndege za Marekani na washirika wake kwenye Ukanda wa Gaza unaozingirwa na Israel, huku mamlaka ya Gaza ikilishutumu zoezi hilo kuwa ni "propaganda tupu" na sio huduma ya kibinadamu.
-
Mtaalamu wa UN: Mpango wa Biden wa kujenga bandari Ghaza ni wa 'maonyesho' ya uchaguzi
Mar 09, 2024 03:50Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa wa Haki amepuuzilia mbali mpango wa Rais wa Marekani wa kuanzisha bandari inayodaiwa kuwa na lengo la kuwezesha kuingizwa misaada katika Ukanda wa Ghaza, ulioteketezwa kwa vita vya mauaji ya kimbari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vikungwa mkono kwa hali na mali na serikali ya Washington.
-
Kuhani wa Kiyahudi ahamasisha Wazayuni wafanye mauaji ya kimbari Ghaza
Mar 09, 2024 03:43Kuhani mwanamgambo na mhubiri wa mahubiri ya Kizayuni ya utoaji vitisho, Eliyahu Mali, ametoa wito wa kufanywa mauaji ya kimbari ya Wapalestina waliowekewa mzingiro huko Ghaza, akidai kuwa kufanya hivyo kunaendana na Halakha, yaani sheria ya Kiyahudi.
-
Mwendesha Mashtaka wa ICC atuhumiwa kuonyesha undumilakuwili wa wazi kuhusiana na Ghaza
Mar 08, 2024 23:27Shirika la kutetea haki za binadamu la Euro-Med Human Rights Monitor (Euro-Med) limesema Karim Khan, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ameonyesha "undumilakuwili" katika kukabiliana na uhalifu wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina huko Ghaza.
-
Biden ajitoa kimasomaso: Maafa ya sasa ya vifo vya raia Ghaza ni makubwa zaidi kuwahi kutokea huko
Mar 08, 2024 06:51Rais Joe Biden wa Marekani hatimaye amekiri kuwa hali isiyo ya kawaida na ambayo haijawahi kushuhudiwa ndiyo inayotawala katika vita vya kinyama vinavyoendelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ukanda wa Ghaza uliowekewa mzingiro.
-
Kuongezeka uungaji mkono wa wananchi wa Marekani kwa Wapalestina
Mar 05, 2024 04:12Matokeo ya uchunguzi wa maaoni uliofanywa na jarida la Wall Street Journal yanaonyesha kuwa, wananchi wengi wa Marekani hawaridhishwi na utendaji kazi wa Rais Joe Biden katika vita vya Gaza.