-
Hamas yalaani shambulizi la kikatili dhidi ya shule katika mji wa Gaza
Dec 20, 2025 12:54Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imelaani shamulizi la kikatili la Israel dhidi ya shule moja katika mji wa Gaza lililouwa Wapalestina kadhaa. Hamas imeitaja hujuma hiyo kuwa jinai ya kivita ya makusudi na ukiukaji wa wazi wa mapatano ya kusitisha mapigano.
-
HAMAS: Israel imekiuka vipengele vyote vya usitishaji vita, makubaliano yako hatarini kuvunjika
Dec 17, 2025 06:39Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina HAMAS ameushutumu utawala wa kizayuni wa Israel kwa ukiukaji mkubwa na uliopangwa wa makubaliano ya kusitisha vita, akionya kwamba kuendelea kwa mwelekeo huo kunayaweka makubaliano hayo katika hatari ya kuvunjika kikamilifu.
-
Hamas yalaani mauaji ya kamanda wake, raia Gaza
Dec 14, 2025 09:13Kiongozi wa ngazi ya juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas katika Ukanda wa Gaza, Khalil al-Hayya, katika taarifa yake ya video leo Jumapili amethibitisha kuwa, kamanda mwandamizi wa harakati hiyo, Raed Saed ni miongoni mwa watu watano waliouawa shahidi katika shambulio la Israel huko Gaza.
-
Hamas: Israel inakiuka majukumu ya awamu ya 1 ya makubaliano ya kusitisha mapigano
Dec 11, 2025 12:14Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeilaani vikali Israel kwa kutotimiza wajibu wake katika makubaliano ya kusitisha mapigano huko Gaza, wakati harakati hiyo ya Palestina imetekeleza majukumu yake yote kwa mujibu wa awamu ya kwanza ya makubaliano hayo.
-
HAMAS: Tuko tayari kukabidhi silaha kwa utawala wa Wapalestina ikiwa Israel itaondoka kikamilifu Ghaza
Dec 08, 2025 02:34Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, iko tayari kukabidhi silaha zake katika Ukanda wa Ghaza kwa mamlaka ya utawala ya Wapalestina itakayosimamia uendeshaji wa eneo hilo, kwa sharti kwamba uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu wa jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel ukomeshwe kikamilifu.
-
Qatar yakanusha kuisaidia kifedha HAMAS, yasema mawasiliano yao yalianza miaka 13 nyuma
Dec 08, 2025 02:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amesema mawasiliano baina ya Doha na harakati ya Hamas yalianza miaka 10 hadi 13 iliyopita kwa lengo la kurahisisha juhudi za kusitisha mapigano na kupeleka misaada ya kibinadamu Ghaza.
-
Hamas: Mwisho wa Abu Shabab ndio hatima isiyoepukika ya kila msaliti
Dec 05, 2025 10:50Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeonya kwamba mauaji ya mshirika wa Israel na kiongozi wa genge lenye uhusiano na Daesh, Yasser Abu Shabab, ni hatima isiyoepukika ya kila mtu anayechagua kulisaliti taifa na nchi yake na kushirikiana na utawala ghasibu wa Israel.
-
Baada ya Israel kuwaua Wapalestina wengine 24 Ghaza, HAMAS yataka wapatanishi, hasa US iingilie kati
Nov 23, 2025 07:05Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limefanya mashambulizi makali ya anga katika maeneo tofauti ya Ukanda wa Ghaza, na kuwaua shahidi Wapalestina wasiopungua 24, wakiwemo watoto, katika mwendelezo wa ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa tangu wiki sita zilizopita kwenye eneo hilo la Palestina lililoteketezwa kwa vita.
-
Chuo Kikuu cha Harvard: Gen Z wa Marekani wanaifadhilisha Hamas kuliko Israel
Nov 18, 2025 07:49Matokeo ya utafiti mpya yanaonyesha kuwa asilimia 60 ya Kizazi kipya, Gen-Z nchini Marekani wanapendelea Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina "Hamas" kuliko utawala wa Kizayuni wa Israel katika vita vya Gaza.
-
Kwa nini Hamas na makundi ya muqawama ya Palestina yanapinga azimio lililopendekezwa na Marekani?
Nov 17, 2025 10:52Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetangaza katika taarifa yake kwamba makundi na harakati za Palestina zimewasilisha waraka kuhusu rasimu ya azimio la Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kusisitiza kuwa wamepinga vikali azimio hilo lililopendekezwa na Marekani kupitia waraka huo.