-
HAMAS yakataa pendekezo la kuweka silaha chini
Apr 17, 2025 12:40Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeripotiwa kupinga pendekezo la utawala haramu wa Israel la kusitisha vita kwa muda wa wiki sita katika Ukanda Gaza, sambamba na kulitaka kundi hilo la muqawama kuafiki kupokonywa silaha.
-
Hamas yaitisha maandamano ya 'mshikamano wa kimataifa' kulaani jinai za Israel Gaza
Apr 17, 2025 02:31Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imetoa wito wa dharura kwa watu wa dunia kushiriki kikamilifu katika maandamano ya wiki moja ya kushinikiza kusitishwa kwa kampeni ya kutisha ya Israel ya mauaji ya halaiki katika Ukanda wa Gaza.
-
Mkuu wa majeshi ya Israel akiri: Hamas haijashindwa vitani
Apr 15, 2025 07:30Mkuu mpya wa jeshi la Israel ameonya kuwa, vikosi vya jeshi la utawala huo wa Kizayuni vinakosa nguvu kazi na rasilimali za kutimiza malengo ya kujitanua ya utawala huo katika Ukanda wa Gaza uliozingirwa, na kusema kuwa Hamas inaendelea kuudhibiti ukanda huo, mwaka mmoja na nusu baada ya kuzuka kwa vita hivyo.
-
Hamas: Kila anayeweza ashike silaha kukabiliana na njama ya Trump kuhusu Gaza
Apr 02, 2025 03:05Mjumbe wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema akizungumzia mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kuwaondoa Wapalestina Ukanda wa Gaza kwamba: "Mtu yeyote anayeweza kushika silaha anapaswa kuchukua hatua katika uwanja huu."
-
Jinai za kinyama za Israel za kuwaua Wapalestina hata katika Siku ya Idi zalaaniwa vikali
Mar 31, 2025 07:41Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeendelea kuwaua watu wa Ghaza hata katika wakati huu wa Sikukuu ya Idul-Fitri na kutoonyesha heshima yoyote kwa Sikukuu hiyo.
-
Kiongozi mwandamizi wa HAMAS: Muqawama na Silaha zake, kwetu sisi ni mstari mwekundu
Mar 31, 2025 06:59Bassem Naim, kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: "kwetu sisi tukiwa ni taifa linalokaliwa kwa mabavu, Muqawama na silaha zake ni mstari mwekundu na ni suala la uwepo wetu na uhai wetu".
-
Ujumbe wa HAMAS wa Sikukuu ya Idul Fitr
Mar 30, 2025 11:11Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa ujumbe wa Sikukuu ya Idul Fitr kwa kuyataka mataifa ya Kiislamu na Kiarabu kuongeza juhudi na uungaji mkono kwa Wapalestina ili kukomesha jinai za Israel na kuondolewa mzingiro kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Radiamali ya Hamas kufuatia kuuliwa shahidi "Abdel-Latif al-Qanoua" katika hujuma ya Israel
Mar 28, 2025 02:29Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imeashiria katika taarifa yake kuhusu kuuawa shahidi Abdel-Latif al-Qanoua Msemaji wa harakati hiyo katika shambulio la utawala wa Kizayuni na kutangaza kuwa: "Kuwalenga kwa masambulizi viongozi wa harakati ya Hamas na wasemaji wake kamwe hakuwezi kuvunja irada yetu.
-
Kukiri jamii ya ujasusi ya Marekani kwamba Hamas haijashindwa huko Gaza
Mar 28, 2025 02:27Ripoti kuhusu vitisho ambayo hutolewa kila mwaka na jamii ya masuala ya ujasusi ya Marekani imekiri kwamba kundi la muqawama wa Palestina la Hamas huko Gaza halijashindwa bado na kwamba linaendelea kudumisha nguvu, wapiganaji na miundombinu yake.
-
Hamas yataka walimwengu wajitokeze kwa wingi kuiunga mkono Palestina Siku ya Quds
Mar 27, 2025 11:09Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imetoa mwito wa kuhamasishwa walimwengu kujitokeza kwa wingi katika siku za Ijumaa, Jumamosi na Jumapili ili kuonyesha mshikamano na Gaza na al-Quds wakati huu ambapo Israel, kwa uungaji mkono wa Marekani, inaendelea na vita vyake vya mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina Gaza, mkabala wa kimya cha dunia.