-
Kwa nini Hamas na makundi ya muqawama ya Palestina yanapinga azimio lililopendekezwa na Marekani?
Nov 17, 2025 07:22Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetangaza katika taarifa yake kwamba makundi na harakati za Palestina zimewasilisha waraka kuhusu rasimu ya azimio la Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kusisitiza kuwa wamepinga vikali azimio hilo lililopendekezwa na Marekani kupitia waraka huo.
-
HAMAS: Silaha za Muqawama haziwezi kujadiliwa kabla ya kuundwa kwanza nchi ya Palestina
Nov 12, 2025 08:40Osama Hamdan, kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, amesisitiza kwamba, silaha za Muqawama ni suala lisiloweza kujadiliwa kabla ya kuundwa nchi dola ya Palestina na akabainisha kuwa, lengo la kisiasa la Muqawama litabaki kuwa ni kuikomboa ardhi, kuundwa nchi huru ya Palestina ambayo mji mkuu wake ni Baitul-Muqaddas na kuwepo hakikisho la kurejea wakimbizi.
-
HAMAS: Lengo la safari ya rais wa Israel Afrika ni kubadilisha misimamo ya nchi zinazounga mkono Palestina
Nov 10, 2025 02:48Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa safari ya rais wa utawala ghasibu wa kizayuni katika nchi za Afrika ni jaribio la kutaka kubadilisha msimamo wa nchi hizo wa zinazopinga ukoloni na kuunga mkono haki za watu wa Palestina.
-
Hamas yapinga kutumwa jeshi la kigeni Gaza mbadala wa jeshi vamizi la Israel
Nov 05, 2025 03:39Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas katika Ukanda wa Gaza imesema kuwa haiwezakani kutumwa kikosi cha kijeshi cha kigeni katika eneo hilo ambacho kitahudumu kama mbadala wa jeshi vamizi la Israel.
-
Hamas: Israel lazima igharamie ujenzi mpya wa Gaza
Oct 21, 2025 08:01Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas, Mousa Abu Marzouk ametoa wito kwa Israel kufadhili kikamilifu ukarabati na ujenzi mpya wa Ukanda wa Gaza, akitaja uharibifu mkubwa na haki za Wapalestina zaidi ya milioni mbili ambao wamepoteza makazi yao, makazi na riziki.
-
Kushner: Hamas 'inatekeleza kwa nia njema' makubaliano ya usitishaji vita Ghaza
Oct 20, 2025 07:15Mkwe wa Rais Donald Trump wa Marekani, Jared Kushner, ambaye ni mmoja wa wapatanishi wake wakuu katika mpango wa kusitisha mapigano Ghaza, amesema harakati ya Palestina ya Hamas imekuwa "ikitekeleza kwa nia njema" makubaliano hayo, akiashiria taarifa zilizopokelewa kutoka kwa wapatanishi wa kikanda waliohusika katika mazungumzo ya usitishaji huo wa vita.
-
HAMAS: Hatutajifunga kukabidhi silaha mpaka yatakapofanyika mazungumzo zaidi
Oct 18, 2025 23:12Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesisitiza kuwa haitajifunga moja kwa moja kukabidhi silaha na inatumai usitishaji vita na utawala wa kizayuni wa Israel utadumu kwa muda wa miaka mitatu hadi mitano ili kuijenga upya Ghaza.
-
Taa ya kijani ya Trump kwa Israel; Je vita vya Gaza vitaanza tena?
Oct 17, 2025 22:59Rais Donald Trump wa Marekani ameionyesha Israel taa ya kijani ili ianzishe tena vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Hamas yaonya; Israel inaendelea kuchuja orodha ya mateka
Oct 13, 2025 06:12Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas kuushutumu utawala ghasibu wa Israel kwa 'kutia mkono' orodha ya mateka wa Kipalestina, na kukwepa kutekelezwa masharti na vipengee vya makubaliano ya usitishaji vita Gaza, licha ya ahadi zake kwa wapatanishi wa kimataifa.
-
Hamas yawakabidhi kwa Msalaba Mwekundu huko Gaza mateka 7 wa kwanza wa Israel
Oct 13, 2025 03:10Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (ICRC) limetangaza kukabidhiwa mateka saba wa kwanza wa Israel katika Ukanda wa Gaza.