-
Nchi tatu za Ulaya zapinga ustawi wa Iran katika sekta ya anga za mbali
Jan 28, 2024 23:31Katika taarifa ya pamoja, Ujerumani, Ufaransa na Uingereza, ambazo kidiplomasia zinajulikana kama Troika ya Ulaya, zimelaani hatua ya Iran wiki iliyopita ya kurusha satalaiti ya Soraya au Thurayya katika mzunguko wa kilomita 750 kutoka ardhini kwa kutumia roketi ya "Qaim 100".
-
Iran yatuma angani satalaiti tatu kwa mafanikio
Jan 28, 2024 10:01Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imefanikiwa kutuma angani satalaiti tatu kwa mpigo zilizotengenezwa na wataalamu wa hapa nchini.
-
Kan'ani: Mashirika ya 'haki za binadamu' ya Magharibi hayana tena itibari
Jan 28, 2024 09:54Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema mashirika yanayojidai kuwa ya kutetea haki za binadamu katika nchi za Magharibi yamepoteza itibari na uhalali wao kwa kufumbia macho jinai za kutisha zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Tehran: Iran na Pakistan hazitaruhusu maadui waharibu uhusiano wao wa kindugu
Jan 28, 2024 04:24Kufuatia shambulio lililowalenga raia wa Pakistan ndani ya Iran, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema Tehran na Islamabad hazitavumilia chokochoko za kuharibu uhusiano wa nchi hizo mbili.
-
Kukuza uhusiano na nchi za Afrika, moja ya mihimili ya sera za kigeni za Iran
Jan 28, 2024 01:05Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameutaja msingi wa uhusiano wa Tehran na nchi za Kiafrika kuwa ni mungamano wa kiroho baina ya mataifa hayo na kwamba uhusiano huo ni moja ya mihimili mikuu ya siasa za nje za Iran.
-
Kan'ani: Msingi wa Israel umejengwa kwa kutegemea mabavu na ubaguzi
Jan 27, 2024 08:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa jibu la kiuhasama lililotolewa na utawala wa Kizayuni wa Israel mkabala wa hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) linaonyesha namna msingi wa utawala huo ulivyojengwa kwa kutegemea vitendo vya mabavu na ubaguzi; na wakati huo huo unadhihirisha namna utawala huo usivyoheshimu kanuni na sheria za kimataifa.
-
Iran yaipongeza Afrika Kusini kwa ushindi wake katika mahakama ya ICJ dhidi ya Israel
Jan 27, 2024 03:01Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amepongeza mafanikio ya kidiplomasia ya Afrika Kusini katika Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu na kuwataka mawaziri wenzake wa mashauri ya kigeni duniani kuunga mkono hatua hiyo ya Afrika Kusini.
-
Raisi: Msingi wa uhusiano wa Iran na Afrika ni maslahi ya pamoja
Jan 25, 2024 07:43Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uhusiano wa Iran na Mali pamoja na nchi nyingine za Afrika si wa kisiasa na kidiplomasia tu, bali umejengeka katika msingi wa maslahi ya pande mbili na pande kadhaa.
-
Marais wa Iran na Uturuki wasaini hati 10 za ushirikiano
Jan 25, 2024 03:36Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki zimetia saini hati 10 za ushirikiano kwa lengo la kuzidisha uwekezaji, ushirikiano wa kiuchumi na masuala ya kieneo.
-
Wairani wajitokeza kwa wingi kuwaaga mashahidi wa shambulizi la kigaidi la Israel
Jan 22, 2024 08:38Shughuli ya kuwaaga mashahidi wa shambulizi la kigaidi la Israel nchini Syria imefanyika hapa Tehran kwa kuhudhuriwa na viongozi wa ngazi ya juu, familia za mashahidi hao na umati mkubwa wa wananchi Waislamu wa Iran.