-
Jenerali Salami: Vita vijavyo vitaashiria mwisho wa uhai wa Israel
Aug 08, 2021 03:29Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ameukumbusha utawala wa Kizayuni juu ya uwezo mkubwa wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon katika mapambano na vita vya nchi kavu na kuonya kuwa, hatua yoyote ghalati itakayopelekea kuibuka vita vipya, haitakuwa na matokeo mengine isipokuwa kufutwa Israel katika uso wa dunia.
-
Iran: Mauaji ya Hiroshima ni kumbukumbu ya jinai za US dhidi ya binadamu
Aug 08, 2021 03:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema mashambulizi ya mabomu ya atomiki yaliyofanywa na Kikosi cha Anga cha Jeshi la Marekani dhidi ya miji ya Hiroshima na Nagasaki nchini Japan katika Vita Vya Pili Vya Dunia ndiyo jinai kubwa zaidi dhidi ya binadamu iliyowahi kuhuhudiwa katika uso wa dunia.
-
Qalibaf: Vita vya 'Upanga wa Quds' viliwapa izza Waislamu
Aug 06, 2021 20:37Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema vita vya siku 12 vya 'Upanga wa Quds' huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu viliwapa izza na kuwapandisha hadhi Waislamu kote duniani.
-
Raisi: Kuna fursa nzuri za kuimarisha uhusiano wa Iran na Tanzania, Zanzibar
Aug 06, 2021 10:28Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuna fursa nyingi na nzuri za kuboresha na kustawisha kiwango cha uhusiano baina ya Iran kwa upande mmoja na Tanzania na Zanzibar kwa upande mwingine.
-
Sera za kigeni za serikali ya Raeisi; ushirikiano erevu na ulimwengu, mtazamo maalumu kwa majirani
Aug 06, 2021 05:20Rais wa nane wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amebainisha katika hotuba yake ya kwanza mara baada ya kuapishwa kuhusiana na utendaji wa serikali mpya ya Iran kuhusiana na sera za kigeni kwa ajili ya kudhamini maslahi ya kitaifa katika uga wa kieneo na kimataifa.
-
Raeisi ataka kuimarishwa uhusiano wa Iran na nchi za Afrika
Aug 05, 2021 08:05Rais wa Iran amesema kiwango cha uhusiano kati ya Jamhuri ya Kiislamu na nchi za Afrika ikiwemo Ghana hakiridhishi na kwamba kuna haja ya kuimarishwa zaidi mahusiano hayo.
-
Moscow: Taarifa kuhusu shambulizi dhidi ya meli ya Mercer Street zinakinzana
Aug 05, 2021 02:37Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa amepinga tuhuma zilizotolewa hivi karibuni na utawala wa Kizayuni wa Israel na nchi za Magharibi dhidi ya Iran kuhusu shambulizi lililolenga meli ya Mercer Street na kusema, taarifa hizo zinakinzana na zimetegemea dhana na tetetsi.
-
Iran yasikitishwa na moto mkubwa wa misituni ulioikumba Uturuki
Jul 30, 2021 22:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameeleza masikitiko yake kufuatia moto mkubwa unaoendelea kuteketeza misitu nchini Uturuki.
-
Safari ya Qalibaf mjini Damascus; ukurasa mpya wa uhusiano wa kiuchumi kati ya Iran na Syria
Jul 30, 2021 22:09Katika safari yake ya karibuni nchini Syria, Mohammad Baqer Qalibaf, Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran ameonana na kuzungumza na rais, waziri mkuu, waziri wa mambo ya nje na wafanyabiashara wa nchi hiyo.
-
Wamarekani wanaanza vita vya kinafsi dhidi ya rais mteule wa Iran
Jul 29, 2021 02:38Kundi moja la maseneta wa chama cha Republican nchini Marekani limemtumia barua Rais Joe Biden likimtaka azuie rais mteule wa Iran, Ayatullah Sayyid Ebrahim Raeisi na maafisa wengine wa Iran kuingia nchini humo kwa ajili ya kushiriki mkutano wa kila mwaka wa Umoja wa Mataifa.