-
Jen. Mousavi: Iran imeivurumishia Israel makombora 30 ya balestiki
Mar 14, 2026 07:18Kamanda wa Kikosi cha Anga za Mbali cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran IRGC amesema asilimia kubwa ya makombora 30 ya balestiki yaliyovumishwa na Jamhuri ya Kiislamu usiku wa Lailatul Qadr yalipiga shabaha zilizokusudiwa kwa usahihi mkubwa.
-
Wataalamu wa haki wa UN walaani mashambulizi ya US, Israel dhidi ya Iran
Mar 14, 2026 06:59Kundi moja la wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa limelaani vikali mashambulizi na jinai zinazofanywa na Marekani na Israel dhidi ya wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Lebanon.
-
Mamilioni ya Wairani washiriki maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds licha ya kudondoshewa mabomu na US, Israel
Mar 13, 2026 10:06Mamilioni ya wananchi wa Iran katika pembe zote za nchi wameshiriki katika maandamano makubwa ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds Ijumaa, huku tawala za kitwaghuti za Marekani na Israel zikiendelea kushambulia kwa mabomu miji mbali mbali ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Russia: Iran ina haki ya kujitetea mbele ya mashambulizi ya Marekani, Israel
Mar 13, 2026 07:36Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina haki ya kujitetea na kukabiliana na hujuma za Marekani na Israel na ametoa wito wa kusitishwa mashambulizi ya Marekani na Israel na kurejea kwenye meza ya mazungumzo.
-
IRGC yashambulia meli nyingine ya mafuta ya US Ghuba ya Uajemi
Mar 13, 2026 07:27Kikosi cha Majini cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran IRGC kimetangaza habari ya kushambulia meli nyingine ya mafuta Marekani katika Ghuba ya Uajemi.
-
Larijani: Asia Magharibi itatumbukia gizani US ikishambulia mtandao wa umeme wa Iran
Mar 13, 2026 06:59Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran ametoa onyo kali akijibu vitisho vipya vilivyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu kushambulia giridi ya taifa ya umeme wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Waisraeli 2,700 wajeruhiwa katika mashambulizi ya kisasi ya Iran
Mar 13, 2026 06:43Ripoti ya Wizara ya Afya ya utawala wa Kizayuni wa Israel imesema Waisraeli zaidi ya 2,700 wamejeruhiwa katika mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yaliyoanza Februari 28.
-
Rais wa Iran atangaza masharti ya kusitishwa vita vya kutwishwa vya US, Israel
Mar 12, 2026 07:21Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian ametangaza masharti kadhaa ya kuhitimisha vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu; huku tawala mbili hizo za kigaidi zikiendelea kushambulia maeneo muhimu ya kiraia kama shule, hospitali, makazi ya watu, na turathi za kihistoria za nchi hii.
-
Araghchi aonya UN: Kunyamazia kimya uvamizi wa US, Israel kutashadidisha taharuki katika eneo
Mar 12, 2026 06:53Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres kuwa, kufumbia macho au kutochukua hatua za maana mkabala wa vitendo vya kivamizi vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kutafungua njia ya kushadidi ukosefu wa utulivu na taharuki katika eneo.
-
Pezeshkian amhutubu Trump: Wavamizi huja na kwenda, lakini Iran itabaki
Mar 11, 2026 08:04Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amekosoa vikali vitisho vya kukaririwa vya Rais wa Marekani, Donald Trump kwamba ataisambaratisha Iran, akisiitiza kuwa, wavamizi na waharibifu mithili Trump walikuja na wakaondoka, lakini Iran imeendeelea kubakia.