-
Iran: Wanachama wa UN hawana wajibu wa kuheshimu maazimio batili dhidi ya Tehran
Sep 28, 2025 22:56Iran imesema madai yaliyotolewa na Marekani na nchi za Ulaya kuhalalisha kurejeshwa kwa maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya nchi hii hayaziwajibishi nchi wanachama wa UN kuzingatia na kuheshimu hati za umoja huo zilizobatilishwa hapo awali.
-
Kamanda wa Iran: Uchokozi wowote dhidi yetu utajibiwa haraka
Sep 28, 2025 07:32Kamanda Mkuu wa Jeshi wa Iran, Meja Jenerali Amir Hatami amesisitiza kuwa, taifa hili limejiweka sawa na tayari kutoa jibu zito na la haraka dhidi ya vitisho na vitendo vyovyote vya uhasama vya maadui dhidi yake.
-
Safavi: Marubani zaidi ya 16 wa Israel waliuawa katika vita vya siku 12
Sep 28, 2025 07:32Mshauri mkuu wa masuala ya kijeshi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema kuwa, zaidi ya marubani 16 wa Israel waliangamizwa katika vita vya siku 12 vilivyotwishwa Iran na utawala wa Kizayuni.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Israel ni utawala unaodharaulika na uliotengwa pakubwa duniani
Sep 28, 2025 03:52Ayatullah Sayyid Ali Khamenei Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ameitaja Israel kama utawala unaochukiwa zaidi duniani.
-
Kwa nini Trump anaishupalia jamii ya kimataifa iamini uwongo wake kuhusu Iran?
Sep 27, 2025 07:40Rais wa Marekani kwa mara nyingine tena amekariri katika houba aliyoitoa katika Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa madai yake ya uwongo na yasiyo na msingi dhidi ya Iran.
-
Iran: Kura ya 'snapback' ni batili, haina mashiko ya kisheria
Sep 26, 2025 23:38Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesisitiza kuwa, juhudi za mataifa matatu ya Ulaya ya Uingereza, Ufaransa, na Ujerumani za kuhuisha vikwazo vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu kwa kutumia utaratibu unaojulikana kama snapback' ni "batili na hazina mashiko yoyote ya kisheria."
-
Rais Pezeshkian: Mazungumzo hayana maana ikiwa vikwazo vitarejeshwa
Sep 25, 2025 23:01Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa mazungumzo ya kidiplomasia hayatakuwa na maana iwapo kundi la nchi tatu za Ulaya E3 linaloundwa na Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zitarejesha tena vikwazo dhidi ya Tehran.
-
Iran yaonyesha taswira za ndani ya kinu cha nyuklia cha Israel, taarifa nyeti za wanasayansi na wataalamu 189 wa kijeshi
Sep 25, 2025 03:33Kwa mara ya kwanza, Wizara ya Usalama ya Iran imeonyesha hadharani picha na taswira nyeti za ndani ya kinu cha nyuklia cha Dimona cha utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Kamanda wa Iran: Israel haina ubavu wa kuanzisha vita bila ya msaada wa Marekani na NATO
Sep 25, 2025 00:10Kamanda mwandamizi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, utawala wa kizayuni wa Israel hauna uwezo wa kupigana bila ya kusaidiwa na shirika la kijeshi la NATO na Marekani, jambo linalodhihirisha kuwa makabiliano yanayoweza kutokea ni ya mpambano dhidi ya "ubeberu wa kimataifa."
-
Pezeshkian: Jithada za kuzuia uhusiano mwema kati ya nchi za Kiislamu hazitafanikiwa
Sep 23, 2025 08:27Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria jitihada za maadui za kuzusha hitilafu na mgawanyiko baina ya nchi za Kiislamu; na kushindwa kuasisiwa uhusiano wenye matunda katika eneo hasa kati ya Iran na Jamhuri ya Azerbaijan.