-
UNESCO yailaani Israel kwa mauaji ya wanahabari wa Iran
Jul 18, 2025 09:58Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) limelaani mauaji ya wafanyakazi wawili wa vyombo vya habari wa Iran wakati wa mashambulizi ya anga ya Israel kwenye makao makuu ya Shirika la Utangazaji la Iran, IRIB mjini Tehran mwezi uliopita.
-
Jibu la suali la leo; nini sababu ya waziri wa zamani wa mambo ya nje wa US kukosoa sera ya Trump kuhusiana na Iran?
Jul 18, 2025 08:53Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Anthony Blinken, amekosoa mwelekeo wa rais wa nchi hiyo Donald Trump kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran; na licha ya kuibua madai mengine mapya amesema: Iran bado haijaamua kuunda silaha za nyuklia na imetekeleza ahadi zake katika JCPOA.
-
Intelijensia: US inajifanya inataka kuzungumza na Iran wakati inajiandaa kwa vita
Jul 18, 2025 01:39Afisa mmoja mwandamizi wa kisiasa wa Iran ameiambia Press TV kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitaingia kwenye mazungumzo mapya na Marekani kwa kutumia mfumo au ajenda ya hapo awali, baada ya funzo ililopata kutokana na mazungumzo ya hapo kabla.
-
Wabunge wa Iran waziasa nchi 44 ziiwekea Israel vikwazo
Jul 17, 2025 11:20Wanachama wa Kamati ya Mahakama na Sheria ya Bunge la Iran wametoa wito kwa makumi ya nchi duniani kuchukua hatua za kuiwekea Israel vikwazo kutokana na utawala huo "kukiuka kanuni za kimataifa na haki za binadamu."
-
Kamanda wa IRGC: Tupo tayari kuendeleza vita pale vilipoishia
Jul 17, 2025 11:04Meja Jenerali Mohammad Pakpour, Kamanda wa Vikosi vya Ardhini vya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) ametangaza kwamba majeshi ya Iran yamejipanga kikamilifu kushambulia tena, akiwaonya maadui kwamba uchokozi wowote ujao utakabiliwa na jibu la haraka, na kuendeleza vita hivyo pale vilipoishia.
-
Iran yakanusha ‘madai hewa’ ya US kuhusu hali ya Yemen na Bahari Nyekundu
Jul 17, 2025 07:19Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ametupilia mbali tuhuma zilizotolewa hivi karibuni na Marekani dhidi ya Iran kuhusu hali ya Yemen na Bahari Nyekundu akisema "hazina msingi wowote" na akalaani ushiriki wa kijeshi wa Washington katika hujuma dhidi ya Yemen.
-
Iran: US inatumia vikwazo kuwanyamazisha wanaokosoa mauaji ya halaiki Gaza
Jul 17, 2025 02:03Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baghaei amesema Marekani inajaribu kuwanyamazisha wakosoaji wa mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel huko Gaza kwa kuwawekea vikwazo.
-
Nini lengo la Umoja wa Ulaya katika kuzidisha vikwazo dhidi ya Iran?
Jul 16, 2025 23:05Umoja wa Ulaya, ukifuata nyayo za Marekani, umeendeleza siasa za kuzidisha mashinikizo dhidi ya Iran katika nyanja mbalimbali katika muhula wa pili wa uongozi wa Donald Trump kwa shabaha ya kuilazimisha Tehran isalimu amri mbele ya matakwa ya kupindukia mipaka ya nchi za Magharibi.
-
Bunge: Marekani itimize masharti ya Iran iwapo inataka kuendelea na mazungumzo
Jul 16, 2025 10:54Bunge la Iran limetoa taarifa na kutangaza kwamba, Jamhuri ya Kiislamu katu haiwezi kufanya mazungumzo na Marekani kama ilivyokuwa kabla ya uchokozi wa hivi karibuni, na kwamba hakuna mazungumzo mapya na Marekani yanapaswa kufanyikakabla ya masharti ya Tehran kutimizwa.
-
Kiongozi Muadhamu: Israel iliikimbilia Marekani kulilia usitishaji vita na Iran
Jul 16, 2025 08:42Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema Israel ililazimika "kusalimu amri na kuing'ang'ani Marekani" kwa kukata tamaa, wakati wa vita vya hivi karibuni vya siku 12 dhidi ya Iran, na kuthibitisha kuwa haina na uwezo wa kukabiliana na Jamhuri ya Kiislamu pekee.