-
Iran: Marekani imepuuza sheria za haki za binadamu kwa kuunga mkono utawala wa Kizayuni
Dec 15, 2024 07:54Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema katika ripoti yake ya kila mwaka kuwa: Marekani imepuuza sheria za kimataifa na maamuzi yote ya taasisi za haki za binadamu kwa uungaji mkono wake mkubwa na usio na kikomo kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Iran na Qatar zasisitiza kuzuiwa mashambulio ya Israel dhidi ya miundomsingi ya Syria
Dec 12, 2024 07:38Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Qatar wamesisitiza juu ya ulazima wa kufanyika juhudi na kuchukuliwa hatua za dhati ili kusimamisha mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya miundomsingi ya Syria na kukalia kwa mabavu maeneo zaidi ya nchi hiyo na utawala huo ghasibu.
-
Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan
Dec 12, 2024 02:58Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mauaji ya Khalil-ur-Rehman Haqqani, waziri wa masuala ya wakimbizi wa serikali ya kundi la Taliban nchini Afghanistan.
-
Tuhuma mpya za Troika ya Ulaya dhidi ya mpango wa amani wa nyuklia wa Iran
Dec 10, 2024 23:16Troika ya Ulaya (Ujerumani, Ufaransa na Uingereza) ya Jumatatu ya tarehe 9 Disemba ilikariri madai yenye utashi wa kisiasa kuhusu mpango wa amani wa nyuklia wa Iran.
-
Iran yalaani jinai na uvamizi wa mfululizo wa Israel dhidi ya Syria
Dec 10, 2024 03:03Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali uvamizi na mashambulizi ya mara kwa mara wa utawala wa Kizayuni dhidi ya miundombinu ya Syria ambapo Israel imeteka na kukalia kwa mabavu maeneo mengine ya Syria katika kipindi cha siku chache zilizopita.
-
Iran: Mpango wa amani wa nyuklia wa Iran uko uwazi na chini ya usimamizi wa IAEA
Dec 08, 2024 04:33Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, mradi wa amani wa nyuklia wa Iran uko wazi na unafanyika chini ya usimamizi wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Iran yaitaka Ukraine iache kuwaunga mkono na kuwasaidia magaidi eneo la Asia Magharibi
Dec 06, 2024 22:56Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imeitaka Ukraine iache kuunga mkono magaidi katika eneo la Asia Magharibi.
-
Mkutano wa mawaziri wa nchi zinazouza gesi duniani waanza Tehran
Dec 06, 2024 08:39Mkutano wa 26 wa nchi zinazouza gesi duniani umeanza shughuli zake hapa mjini Tehran.
-
Mufti wa Tanzania apongeza uamuzi wa Iran wa kuanzisha Akademia ya Qur'ani Dar Es Salaam
Dec 05, 2024 23:49Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania ameipongeza Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa uamuzi wake wa kuanzisha Akademia ya Qur'ani ya Dar al-Nur na kuahidi kutoa ushirikiano unaohitajika katika uwanja huo.
-
Iran yapinga madai ya 'Troika ya Ulaya' kuhusu kadhia ya nyuklia
Dec 04, 2024 23:27Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amemtumia barua Katibu Mkuu wa umoja huo na Baraza la Usalama akisema kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi ya Tehran hazina msingi wowote na zina malengo ya kisiasa. Amir Saeid Iravani ameeleza hayo kufuatia tuhuma zilizotolewa na wawakilishi wa Troika ya Ulaya dhidi ya Tehran. Troika hiyo inajumuisha Ufaransa, Uingereza na Ujerumani.