-
Iran: Marekani inataka kushadidisha taharuki katika eneo
Sep 26, 2024 00:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, Marekani pamoja na Israel zinafuatilia kuyumbisha uthabiti na usalama wa eneo la Magharibi mwa Asia, na kupanua mvutano na mgogoro katika eneo hili.
-
Tuhuma na misimamo ya kurudiwarudiwa ya Marekani kwa ulimi wa Joe Biden katika Umoja wa Mataifa
Sep 26, 2024 00:28Jumanne ya wiki hii, rais wa Marekani, Joe Biden, alitoa hotuba yake ya mwisho katika kikao cha 79 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York na kukariri madai ya uongo ya siku zote dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na dhidi ya kambi ya Muqawama. Rais wa Marekani alidai kuwa eti serikali yake inapigania kuleta amani na utulivu katika ukanda wa Asia Magharibi.
-
Rais wa Iran: Amani inapasa kuchukua nafasi ya vita duniani
Sep 23, 2024 23:58Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, amani na usalama vinapaswa kuchukua nafasi ya vita na umwagaji damu duniani. Rais Masoud Pezeshkian amesema hayo alipoona na wakurugenzi waandamizi wa vyombo vya habari vya Marekani mjini New York na kubainisha kwamba, Iran sio kama vyombo vya habari vya dunia vinavyoinyesha na tuko tayari kuishi kwa amani na usalama na dunia nzima.
-
Akthari ya wananchi wa Marekani wanataka nchi yao irejee katika mapatano ya JCPOA
Sep 23, 2024 22:49Watu wengi nchini Marekani wanataka Washington irudi katika Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA). Hii ni kwa mujibu wa uchunguzi wa maoni uliofanyika huko Marekani.
-
Nasser Kanani: Israel haitarejea katika kipindi cha kabla ya Kimbunga cha al Aqsa
Sep 23, 2024 08:26Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameutaja mlingano wa kistratijia katika eneo baada ya operesheni dhidi ya Uzayuni ya Kimbunga cha Al-Aqsa kuwa ulikuwa kwa manufaa ya Wapalestina na makundi ya muqawama. Amesema utawala wa Israel hautarejea katika hali uliyokuwa nayo kabla ya Kimbunga cha al Aqsa.
-
Mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Saudi Arabia wakutana na kushauriana mjini New York
Sep 23, 2024 03:41Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia wamezungumzia hali mbaya ya Ukanda wa Gaza iliyosababishwa na kuendelea kwa mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na utawala katili wa Kizayuni.
-
Rais Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran: Hatupendi vita, tunatetea haki zetu
Sep 18, 2024 02:43Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Iran haijawahi kuwa, na wala haitakuwa mwanzishaji vita vyovyote vile na akabainisha kwamba: "wiki ijayo tutatetea haki za wananchi wa Iran katika Umoja wa Mataifa".
-
Tehran, Beirut zajadili jinai mpya ya kigaidi ya Israel huko Lebanon
Sep 17, 2024 23:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amelaani vikali hujuma mpya ya kigaidi ya utawala wa Kizayuni iliyowalenga raia wasio na hatia nchini Lebanon.
-
Araghchi: Iran haijaipa Yemen makombora
Sep 17, 2024 04:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekanusha vikali madai yasiyo na msingi ya Wamagharibi kuwa eti Yemen imepokea makombora kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Kiongozi Muadhamu: Kuna udharura wa kulinda utambulisho wa Umma wa Kiislamu
Sep 16, 2024 08:49Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kulinda utambulisho wenye thamani wa Umma wa Kiislamu ni dharura na kuongeza kuwa: "Kadhia ya 'Umma wa Kiislamu" haipaswi kusahaulika hata kidongo.