-
Qalibaf asisitizia umoja wa Waislamu katika kadhia ya Palestina
Sep 15, 2024 04:02Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesisitizia haja ya Waislamu kote duniani kuwa na umoja na mshikamano katika suala la Palestina.
-
Iran: Mafanikio yetu katika uga wa teknolojia ni pigo kwa maadui
Sep 15, 2024 03:59Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, hatua ya satelaiti ya utafiti ya Iran iliyopewa jina la "Chamran-1" kurushwa katika anga za mbali kwa mafanikio ni pigo kwa maadui wanaoliwekea taifa hili vikwazo visivyo na mantiki.
-
Azma ya Iran na Iraq ya kuimarisha uhusiano wa pande mbili
Sep 13, 2024 08:16Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na viongozi wa Iraq wamesisitiza nia na azma ya serikali za Tehran na Baghdad kwa ajili ya kuimarisha uhusiano wa pande mbili na ushirikiano wa kieneo.
-
Radiamali ya Iran kwa vikwazo vya nchi za Ulaya dhidi ya Shirika la Ndege la Iran Air
Sep 12, 2024 23:00Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran ameichukulia kauli ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani kuhusiana na kufutwa makubaliano ya pande mbili ya kutoa huduma za anga kwa Iran kuwa ni ugaidi wa kiuchumi wa nchi za Magharibi dhidi ya taifa la Iran.
-
Kuongezeka mauzo ya bidhaa za Iran nchini Iraq
Sep 12, 2024 08:04Shirika la Maendeleo ya Biashara la Iran limetangaza kuwepo ongezeko kubwa la mauzo ya Iran nchini Iraq katika miezi ya karibuni.
-
Iran yaazimia kuimarisha uhusiano na Burkina Faso
Sep 12, 2024 07:37Balozi wa Iran nchini Burkina Faso, Mojtaba Faqihi amekutana na Abubakar Nakanabo, Waziri wa Uchumi na Fedha wa taifa hilo la Afrika Magharibi na kujadili umuhimu wa kupanua ushirikiano wa pande mbili katika nyuga za kiuchumi, kiufundi na kibiashara.
-
Rais wa Iran awasili eneo la Kurdistan la Iraq katika siku ya pili ya ziara yake nchini humo
Sep 12, 2024 04:11Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili katika eneo la Kurdistan la Iraq katika siku ya pili ya ziara yake ya kuitembelea nchi hiyo.
-
Rais wa Iran na Waziri Mkuu wa Iraq wafanya mkutano na waandishi wa habari Baghdad
Sep 11, 2024 23:41Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika mkutano na waandishi wa habari akiwa pamoja na mwenyeji wake Waziri Mkuu wa Iraq: "tunapaswa kutekeleza makubaliano ya ushirikiano wa kiusalama kati ya Iran na Iraq ili kukabiliana na magaidi na maadui".
-
Shahram Irani: Iran haiogopi kukabiliana na dola lolote
Sep 10, 2024 03:36Kamanda wa Jeshi la Majini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa nchi hii imefikia kiwango cha nguvu za aina yake ambazo zinaifanya iweze kuchukua hatua mkabala wa hujuma na makabiliano mbalimbali dhidi yake.
-
Iran: Hatuna nafasi yoyote katika vita vya Russia na Ukraine
Sep 08, 2024 08:34Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu haina mchango wowote katika vita vinavyoendelea kati ya Russia na Ukraine, na daima imekuwa ikikariri wito wake wa mazungumzo ya kuutafutia ufumbuzi mzozo huo.