Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i120040-iran_yailaani_daesh_(isis)_kwa_kumuua_waziri_wa_serikali_taliban_afghanistan
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mauaji ya Khalil-ur-Rehman Haqqani, waziri wa masuala ya wakimbizi wa serikali ya kundi la Taliban nchini Afghanistan.
(last modified 2024-12-12T02:58:39+00:00 )
Dec 12, 2024 02:58 UTC
  • Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mauaji ya Khalil-ur-Rehman Haqqani, waziri wa masuala ya wakimbizi wa serikali ya kundi la Taliban nchini Afghanistan.

Ismail Baqaei amelaani vikali shambulio hilo la kigaidi lililotokea jana Jumatano mjini Kabul na kumuua waziri wa masuala ya wakimbizi wa serikali ya Taliban nchini Afghanistan Khalil-ur-Rehman Haqqani na watu wengine kadhaa.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran pia ametoa mkono wa pole kwa familia za wahanga wa shambulio hilo la kigaidi la Daesh na kuwaombea dua za kupona haraka majeruhi wa shambulizi hilo.

Ismael Baqaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran

 

Duru rasmi za serikali zimetangaza kuwa, Khalil-ur-Rehman Haqqani, Waziri wa Masuala ya Wakimbizi wa Serikali ya Taliban huko Afghanistan, ameuawa katika mripuko wa bomu ndani ya wizara hiyo.

Msemaji wa Jeshi la Polisi mjini Kabul, Khalid Zadran amethibitisha mauaji ya waziri huyo wa masuala ya wakimbizi wa serikali ya Afghanistan katika mripuko uliotokea kwenye Msikiti wa wizara hiyo jana Jumatano ambapo kundi la Taliban limesema kuwa shambulio hilo limefanywa na watu woga ambao wametoka nje ya sheria.